Na. Evelina Odemba - Morogoro
Mahakama ya Tanzania,
Kanda ya Morogoro, tarehe 24 Januari, 2022 imezindua Wiki ya Sheria ambapo Jaji
Mfawidhi, Mhe. Paul Ngwembe amewahakikishia Watanzania kuwa hawatabaki nyuma
katika kutekeleza jukumu ya utoaji haki na wapo tayari kwenda na mabadiliko
yatokanayo na Mapinduzi ya Nne ya Viwanda.
Akizungumza mara baada
ya kushiriki matembezi yaliyoadaliwa kuzindua Wiki ya Sheria ambayo
imeazimishwa na Mahakama ya Tanzania katika maeneo ya Kanda mbalimbali kote
nchini. Mhe. Ngwembe amesema kuwa Mahakama Mkoani Morogoro haipo nyuma kwenye
mabadiliko ya kiteknolojia yanayoendelea hivi sasa.
“Tayari tumefunga
televisheni tatika gereza la Mahabusu ambapo mashauri mbalimbali yameanza
kusikilizwa kupitia mtandao (video conference) huku mahabusu akiwa gerezani na
Hakimu akiwa Mahakan. Jambo hili inaokoa muda na gharama za kuwasafirisha
Mahabusu kufika Mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa,” amesema.
Aidha Jaji Mfawidhi
huyo aliongeza kuwa kwa sasa nakala za hukumu hutolewa siku ya kusomwa kwa
hukumu na ili kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa Mahakama imenunua Kompyuta
Mpakato kwa Waheshimiwa Mahakimu kote nchini kuwarahisishia kuandika hukumu kwa
wakati.
Mhe. Ngwembe alitumia
fulsa hiyo kuwakaribisha wananchi wote kufika katika vituo vya kutolea elimu
ili waweze kujifunza maswala mbalimbali yanayohusu Mahakama pamoja na wadau
wake.
Alivitaja vituo hivyo
kuwa ni viwanja vya Mahakama Kuu- Kituo Jumuishi( IJC)- Kihonda -Morogoro,
viwanja vya shule ya msingi kiwanja cha Ndege, Soko kuu la Kingalu, stendi kuu
ya mabasi Msamvu na soko la Chamwino.
Uzinduzi huo wa Wiki ya
Sheria unaenda sambamba na maonesho yaliyoandaliwa na wadau mbalimbali ambao
kwa takribani siku tano watakuwa wakitoa elimu ya sheria pamoja na huduma za
kisheria kwa wananchi bila malipo yoyote.
Akizungumza kwa niaba
ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, ambaye alitegemewa kuwa Mgeni Rasmi wakati wa
uzinduzi huo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro Bi. Lucy John alitoa pongezi
kwa uongozi wa Mahakama ya Tanzania kwa kubuni kauli mbiu ambazo zimekuwa
zikitambua changamoto mbalimbali wanazopitia wananchi.
Aliongeza kuwa kauli
mbiu hizo zimekuwa zikitumiwa na Mahakama katika kuboresha huduma zake. Alisema
kuwa ni dhahiri kuwa kujengwa kwa Vituo Jumuishi vya Utoaji Haki katika maeneo
mbalimbali nchini utarahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati.
Katika uzinduzi huo
Mgeni rasmi pia alipata nafasi ya kutembelea mabanda ya wadau Mbalimbali ambayo
yameshiriki kuadhimisha wiki hii kwa kutoa huduma kwa wananchi. Miongoni mwa
washiriki ni ofisi ya wanasheria wa serikali, wanasheria wa kujitegemea, polisi, Rita, TARURA, TANROA na wengine
Maadhimisho ya wiki ya
sheria yalianza rasmi mnamo mwaka 1997 ikiwa na malengo ya kuwaleta wananchi
wote karibu na Mahakama, kutoa elimu ya sheria kwa wananchi, sambamba na
wanasheria hutoa huduma ya kisheria kwa wananchi bila malipo ikiwa ni njia ya
kurudisha mchango wao kwa jamii.
Maadhimisho haya kila
mwaka huambatana na kauli mbiu ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni “zama za Mapinduzi ya nne ya viwanda: safari
ya maboresho kuelekea Mahakama Mtandao.”
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Said Kalunde (kushoto) na Mhe. John Chaba wakiwasili katika Kituo cha kutolewa elimu ya sheria kwa wananchi mara baada ya kushiriki matembezi ya Wiki ya Sheria.
Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mwasiliano (TEHAMA) wa Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro, Bw. Tamimu Hussein akitoa maelezo namna ya kusajili mashauri kwa njia ya mtandao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni