Jumamosi, 6 Agosti 2022

WAAJIRIWA WAPYA WA MAHAKAMA WAENDELEA KUPIGWA MSASA NA IJA; WAPATIWA MADA MBALIMBALI

 

     Mhe. Balozi Charles Sanga akiwasilisha mada ya Uzalendo kwa washiriki wa Mafunzo elekezi yanayoendelea kufanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto. Amewataka kuwa Wazalendo na kuzingatia sheria na kanuni za kazi.

Mwanasaikolojia nguli, Bi. Sadaka Gandi akisisitiza jambo kwa Makatibu Mahususi alipokuwa akitoa mada ya jinsi ya kukabiliana na msongo wa mawazo (Stress Management). Amewataka washiriki hao kuwa makini katika utekelezaji wa majukumu yako kwa kutokufanya kazi kwa hisia pamoja na kubadili mitazamo.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Mahakama ya Tanzania, Bi. Beatrice Patrick akiwasilisha mada kwa Makatibu Mahsusi kuhusu Maadili na Stahiki mbalimbali kwa Wutumishi wa Umma katika mafunzo elekezi yanayoendelea katika kutolewa katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Japhet Manyama akiwapitisha washiriki katika mada ya Tamaduni za kimahakama kwenye mafunzo yanayoendelea Chuoni IJA-Lushoto.

Afisa Tehama Mwandamizi,  Bw. Allan Machella akiwafafanulia washiriki juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii na kuwaasa kutotumia mitandao hiyo kutoa taarifa za Ofisi. Aidha, ametoa picha ya mifumo na hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuelekea Mahakama Mtandao 'e-Judiciary'.

 Bw. Hassan Kilenza, Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora akiwasilisha mada ya Maadili na Mienendo ya Utumishi wa Umma kwa washiriki wa mafunzo elekezi yanayoendelea katika Chuo cha Uongozi wa Mahakam Lushoto.

   Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Mhe. Sekela Mwaiseje akitoa Mada kwa Waajiriwa wapya wa Mahakama (hawapo katika picha).

Washiriki wa Mafunzo wakifuatilia Mada inayotolewa na Mwezeshaji (hayupo katika picha).
Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Ufuatiliaji, Mahakama ya Tanzania, Bw. Sebastian Lacha akitoa mada ya Mpango Mkakati wa Mahakama kwa Washiriki wa mafunzo elekezi yanayotolewa kwa Waajiriwa wapya wa Mahakama.
Mshauri wa Masuala ya Kijamii, Bw. Simon Loishiye  akiwasihi Washiriki juu ya kudhibiti mihemko/hisia za kimwili alipokuwa akitoa mada katika Mafunzo Elekezi kwa waajiriwa wapya wa Mahakama ya Tanzania yanayoendela katika Chuo cha Mahakama Lushoto.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni