Jumanne, 27 Septemba 2022

JAJI MKUU AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA UBALOZI WA UINGEREZA

Na Faustine Kapama-Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma leo tarehe 27 Septemba, 2022 amekutana na Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge na kufanya naye mazungumzo mafupi kuhusu mambo mbalimbali ya kimahakama, ikiwemo uwepo wa programu ya kujenga mfumo endelevu wa mapambano dhidi ya rushwa nchini.

Jaji huyo ambaye aliongozana na maafisa kutoka Ubalozi wa Uingereza, akiwemo Mshauri wa Utawala, Bw. Simon Charters na Mtaalamu wa Mashtaka, Bi. Claire Harris alifika ofisini kwa Jaji Mkuu katika jengo la Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha na kumweleza kuhusu programu hiyo.

Programu hiyo inayofadhiliwa na Ubalozi wa Uingereza inahusisha shughuli mbalimbali, ikiwemo kufanya mafunzo ya kuwajengea uwezo Majaji na Mahakimu, matumizi sahihi ya adhabu kwa mujibu wa mwongozo wa utoaji wa adhabu (Sentencing Mannual) na uendeshaji wa kongamano la wadau wa sheria kuhusu mambo kadhaa ya haki jinai katika kipindi cha Wiki ya Sheria (Law Week Symposium).

Hivyo, Jaji Nic alijitambulisha kwa Jaji Mkuu kama mtaalamu ambaye amekuja kuomba kazi ya kutekeleza pragramu hiyo kama ilivyopendekezwa na Ubalozi wa Uingereza kwa Mahakama ya Tanzania kuingia naye mkataba aweze kutoa uzoefu wake katika maeneo hayo matatu, ikiwemo hilo la kuwajengea uwezo Majaji na Mahakimu kusikiliza mashauri ya rushwa kubwa (grant corruption cases).

Kwa upande wake, Jaji Mkuu alifurahia ujio wa Jaji Mstaafu huyo na kumweleza kuwa Mahakama ya Tanzania ipo tayari kushirikiana naye kwenye hayo maeneo. Akizungumzia kuhusu kongamano alilolitaja Jaji Nic, Mhe. Prof. Juma alimweleza mgeni wake kuwa imekuwa utamaduni kwa Wiki ya Sheria kukutanisha wadau mbalimbali wa Mahakama.

Aliwataja baadhi ya wadau hao kama Ofisi ya Mwendesha Mashtaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu na wengine wengi. Hivyo akaridhia mchakato huo ukamilike ili watumishi wa Mahakama waweze kupata uzoefu kwenye maeneo hayo kwa lengo la kuboresha utendaji wa kazi.

Naye Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo, ambaye ndiye Kiongozi wa Timu kwenye suala hilo alifika ofisini kwa Jaji Mkuu akiogozana na wageni hao pamoja na watumishi wengine wawili wa Mahakama, akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Stephen Magoha na Afisa Utumishi, Bw.  Nkuruma Katagira, na kueleza lengo kuu la ujio wao.

Jaji Kihwelo kwa mara nyingi amekuwa akiratibu ushirikiano wa kitaaluma kupitia IJA na kwenye mradi wa programu ya kujenga mfumo endelevu wa mapambano dhidi ya rushwa nchini (BSAAT) amekuwa kama kiunganishi muhimu katika kusimamia mafunzo ya Majaji na Mahakimu kwa kushirikiana na taasisi zile ambazo zinatumia mradi huo.

Hivi karibuni, Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kilichopo mkoani Tanga kiliendesha mafunzo yaliyowaleta pamoja Mahakimu 43 kuhusu namna bora ya utoaji wa adhabu na utekezaji wa amri za Mahakama.

Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo hicho kupitia ufadhili wa Programu ya Kitaifa ya Kuzijengea Uwezo Taasisi za Umma Tanzania zinazohusika na Kuzuia na Kupambana na Rushwa (BSAAT) yalilenga kuwajengea uwezo Mahakimu hao kutekeza jukumu la utoaji haki kwa wananchi.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (kulia) akimpokea mgeni wake,Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge alipowasili ofisini kwake leo tarehe 27 Septemba, 2022 kwa mazungumzo mafupi. 

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (kulia) akisalimiana na Mshauri wa Utawala, Bw. Simon Charters alipowasili ofisini kwake.

Mtaalamu wa Mashtaka kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bi. Claire Harris  (kushoto) akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alipowasili ofisini kwake.
Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge akisaini kitabu cha wageni.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akieleza jambo wakati alipokuwa anazumgumza na Ujumbe kutoka Ubalozi wa Uingereza.
Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge akisisitiza jambo.

Mshauri wa Utawala kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bw. Simon Charters akieleza jambo. 

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo akifafanua jambo.
Mtaalamu wa Mashtaka kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bi. Claire Harris (katikati) akimweleza jambo Jaji Mkuu wa Tanzania (hayupo kwenye picha). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Stephen Magoha na kulia ni Afisa Utumishi, Bw.  Nkuruma Katagira.
Mazungumzo yakiendelea.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge (kushoto) na Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (kulia).
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge (kushoto),  Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (kulia) na Mtaalamu wa Mashtaka kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bi. Claire Harris (wa pili kushoto).
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge (kushoto), Mtaalamu wa Mashtaka kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bi. Claire Harris (wa pili kushoto), Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (kulia) na Mshauri wa Utawala kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bw. Simon Charters (wa pili kulia).


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mstaafu wa Uingereza, Mhe. Nic Madge (wa pili kushoto), Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (wa pili kulia), Mshauri wa Utawala kutoka Ubalozi wa Uingereza, Bw. Simon Charters (wa tatu kulia),Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Stephen Magoha (kushoto) na kulia ni Afisa Utumishi, Bw.  Nkuruma Katagira (kulia).










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni