Jumatano, 1 Februari 2023

RAIS MHE.DKT. SAMIA AAGIZA KUIMARISHWA KWA NJIA YA USULUHISHI

Na Tiganya Vincent-Mahakama -Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema ni muhimu njia ya usuluhishi ili iweze kutatua migogoro kwa haraka inapotokea.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 1 Februari 2023 katika Viwanja vya Chinangali , jijini Dodoma wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini ambayo kauli mbiu  yake ni; ‘Umuhimu wa utatuzi wa Migogoro kwa njia ya Usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu: Wajibu wa Mahakama na Wadau.’

Mhe. Dkt. Samia amesema hatua hiyo itasaidia kuvutia na kulenga kuwajengea imani kwa wafanyabiashara na wawekezaji juu ya usalama wa mali zao.

Ameongeza kuwa, ni muhimu utaratibu wa usuluhishi ukapewa kipaumbele na uwe endelevu katika kutatua migogoro ambayo haitaji wahusika kuwa  wanasheria.

Aidha, Mhe. Dkt. Samia ameagiza kupitia taratibu na kuzifanyia marekebisho Sheria zote zinazochelewesha kesi na upatikanaji haki ili zisiwe vikwazo katika kuharakisha maendeleo nchini.

Ameongeza kuwa ni vema mafunzo ya kusimamia taratibu za usuluhishi yakatolewa kwa vyombo ambavyo vimepewa majukumu ya kusimamia usuluhishi ili wananchi wengi watumie njia hiyo badala  ya kukimbilia Mahakamani na kutumia muda mwingi na gharama nyingi.

Wakati huo huo Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.Prof. Ibrahim Hamis Juma amewataka viongozi wa dini kutatua migogoro kwa njia usuluhishi kwa kuzingatia  taratibu zao badala ya kukimbizia masuala yao Mahakamani na kuanika siri zao.

Amesema siku kizi kumeibuka tatizo la viongozi wa dini wanapokuwa na migogoro kukimbilia Mahakamani badala ya kusuluhisha Katiba au Mabaraza yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya sheria nchini leo tarehe 01 Feberuari, 2023 katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma amesema ni muhimu kutumia njia ya usuluhishi ili kutatua migogoro kwa haraka inapotokea.

Sehemu ya Viongozi Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioshiriki katika kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchi.


Sehemu ya Mawakili wa Serikali, Wakujitegemea na wananchi walioshiriki katika kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchi.


Sehemu ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walioshiriki katika kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchi.

Meza Kuu ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakiwa kwenye picha ya pamoja na Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania wakati wa hafla ya kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchini.


Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu washuhudia gwaride la heshima lililokaguliwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (hayupo pichani) wakati wa shughuli ya kitaifa ya kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchi.

Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu wakifuatilia hotuba ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa shughuli ya kitaifa ya kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchi.

Meza Kuu ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania wakati wa hafla ya kuadhimisha kilele cha siku ya sheria nchini.

(Picha na Innocent Kansha- Mahakama)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni