Na Naumi Shekilindi-Mahakama, Simiyu
Katika
kutekeleza nguzo ya tatu ya Mpango Mkakati wa Mahakama (2020/21– 2024/25),
Mahakama Mkoa wa Simiyu imefanikiwa kuanzisha Club ya Sheria na kutoa elimu kwa
wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bariadi.
Mahakimu
wanne pamoja na wanafunzi wa wanaosoma sheria kutoka vyuo mbalimbali hivi
karibuni walitoa mada kadhaa kuhusu sheria kwa wanafunzi wapatao 300 kutoka Shule
ya Sekondari Bariadi.
Timu
hiyo ya kutoa elimu iliongozwa na Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya Bariadi, Mhe. Mary Nyangusi, ambaye aliwaeleza juu ya muundo wa
Mahakama na Mpango Mkakati wa Mahakama, hasa katika kutekeleza nguzo ya tatu.
“Lengo
kuu la kuanzisha Club za Sheria mashuleni ni kuwajengea uwezo wanafunzi waweze
kutambua haki zao za msingi, waweze kuwa na uelewa mzuri juu ya sheria na
kuwahamasisha kupenda kusoma sheria. Tumelazimika kuja na wanafunzi wanaosoma
sheria kwa vitendo kutoka vyuo mbalimbali ili muweze kuhamasika zaidi,” alisema.
Mkuu
wa Shule ya Sekondari Bariadi, Bw. Godfrey Masunga alifurahi
kuanzishwa kwa Club ya Sheria shuleni kwake, kwani ndio ilikua kiu kubwa kwa
wanafunzi wake. “Nimefurahi sana kwa ujio wenu, kwani vijana wangu watajifunza
mambo mengi kuhusu sheria na haki zao kiujumla,” alisema Bw. Masunga.
Wanafunzi
kutoka shule hiyo, baada ya kupata elimu hiyo waliuliza maswali mbalimbali,
ikiwemo kutaka kujua kwa nini mshtakiwa akiachiwa huru ndani ya mwezi mmoja
haruhusiwi kupiga kura na njia zinazotumika kumkamata mtu anayedaiwa kufanya mauaji
na kukimbia je ya nchi.
Pia
wanafunzi walitaka kujua vitu gani kwenye Katiba ya Tanzania vinahitaji
kufanyiwa marekebisho, kwanini sheria isianze kufundishwa kuanzia elimu ya chin.
Maswali hayo yalijibiwa kwa usahihi na timu nzima iliohudhuria kikao hicho cha
uzinduzi wa Club ya Sheria.
Naye Afisa Tawala wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, akifunga mkutano huo aliwaomba wanafunzi na walezi wa Club hiyo kutembelea Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya Bariadi ili kujionea namna Mahakama hizo zinavyofanya kazi.
Mahakimu wa Mahakama ya Wilaya na Mahakama ya Mwanzo Bariadi wakiwa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Bariadi pamoja na mwanafunzi anayejifunza kwa vitendo katika Mahakama ya Mwanzo Somanda.
Wanafunzi
wa Shule ya Sekondari Bariadi wakisikiliza kwa makini elimu inayotolewa na timu
ya Mahakama juu ya sheria.
Mkuu
wa Shule ya Sekondari Bariadi,
Bw. Godfrey Masunga akiwakaribisha watumishi wa Mahakama waliokuja kutoa
elimu na kuanzisha Club ya Sheria shuleni hapo.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni