Na Faustine Kapama-Mahakama, Iringa
Timu ya Mahakama ya
Tanzania (Mahakama Sports) imekomba makombe matatu na medali tatu katika
mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI)
ambayo yamehitimishwa leo tarehe 14 Octoba, 2023 mkoani hapa baada ya kushinda
kwenye michezo mbalimbali.
Mahakama Sports imeshika
nafasi ya pili kwenye mchezo wa Kamba Wanawake, ikashika nafasi hiyo pia kwenye
Kamba Wanaume na nafasi ya pili kwenye Riadha Wanawake mita 3,000.
Kwenye Riadha Mahakama
Sports pia imeshika nafasi ya pili mita 400 na nafasi kama hiyo kwenye kwenye
mchezo wa Tufe na ikanyakua mshindi wa pili kwenye Bao.
Katika michezo ya Kamba
na Bao Mahakama Sports ilikabidhiwa makombe kwa kila mchezo, huku washindi
katika riadha na tufe wakivalishwa medali.
Kabla ya kukabidhiwa
zawadi hizo kulifanyika michezo miwili ya fainali ya kuvuta kamba kwa Wanaume
na Wanawake, huku Mahakama Sports ikikabiliana vilivyo na Ikulu na Uchukuzi, mtawalia,
na kufanikiwa kushika nafasi ya pili kwenye kila mchezo.
Ulikuwa mchezo wa Kamba
Wanawake ulioanza, huku Uchukuzi ambao walikuwa na nyuso tofauti na wale waliokuwa
wamesajiliwa awali kushiriki kwenye mashindano hayo walifanikiwa kuwavuta
Mahakama Sports kwenye mivuto yote miwili.
Baada ya mchezo huo
kumalizika, ikafuata Kamba Wanaume iliyowashirikisha watoto wa Baba mmoja, Ikulu
na Mahakama na mchezo huo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili kwani katika mvuto
wa kwanza hakuna aliyemtambia mwenzake.
Ikulu walifanikiwa
kushinda katika mvuto wa pili baada ya viatu vya baadhi ya wachezaji wa Mahakama
Sports kuchanika, hivyo kuwafanya wapoteze uimara wa kuhimili mchezo.
Akizungumza baada ya michezo
hiyo ya fainali kumalizika, Mwenyekiti wa Mahakama Sports Wilson Dede amesema
kuwa kazi iliyowaleta Iringa wameikamilisha na wametimiza kwa asilimia kubwa
ahadi waliyokuwa wameitoa.
“Tuliahidi kurudi
nyumbani na vikombe, nadhani umeona tumeshavichukua tayari Kazi moja ikimalizika inaanzisha nyingine. Tutafanya
tathmini kuangalia wapi tulipojikwaa ili turekebishe kwa ajili ya mashindano
mengine yajayo,” amesema.
Katika mashindano hayo ya
SHIMIWI yaliyoanza Septemba 29, 2023, Mahakama Sports ilishiriki katika michezo
mbalimbali, ikiwemo Kamba Wanaume na Wanawake, Mpira wa Miguu Wanaume,
Netiboli, Bao, Karata, Tufe na Riadha.
Kwenye mchezo wa Kamba, Bao
wanaume, Tufe na riadha imeshika nafasi ya pili kwenye kila mchezo, huku kwenye
Netiboli na Mpita wa Miguu Wanaume ikashika nafasi ya nne, huku Karata ikiishia
kwenye makundi.
Wachezaji wa Kamba Kamba
Wanaume walioiwakilisha kwenye mashindano hayo walikuwa Leonard Kazimzuri,
Joseph Chokela, Cletus Yuda, Luyuga Luyuga, Patrick Mundwe, Denis Kipeta,
Abdulmumin Mbaraka, John Charles, Kumbukeni Mtete na Martin Mushi, Hemed
Semith, Emmanuel Dasian, Ashel Chaula, Willy Mwaijibe, Mussa Komba na Marko
Mochiwa.
Kwa upande wa Kamba
Wanawake walikuwepo Judy Mwakyalabwe, Zahara Suleiman, Beatrice Dibogo, Melina
Mwinuka, Rebeca Mwakabuba, Tumaini Kizito, Namweta Mcharo, Joyce Simba,
Sarafina Mkumbo na Mariam Mayalla, Winiel Mahumbuga, Witness Lyasato, Veronica
Rajabu, Eunice Lugiana na Janeth Mapunda.
Katika mchezo wa Netiboli,
timu ilishika nafasi ya nne na Mahakama iliwakilishwa na Tatu Mawazo, Filomena
Haule, Upendo Gustaf, Nyangi Kisangeta, Eunice Chengo, Sophia Songoro,
Shan Ally, Agness Mwanyika, Nuru Nchimbi, Malkia Nondo, Talita Kayuli, Ruth
Kibona na mchezaji kiongozi akiwa Theodosia Mwangoka.
Upande wa timu ya Mpira wa Miguu ambayo nayo imeshika
nafasi ya nne, Mahakama iliwakilishwa na Fahamu Kibona, Michael Turuka, Nasoro Mwampamba,
Gisbert Chentro, Rashid Mbwana, Akida Mzee, Kelvin Muhagama, Frank Obadia,
Seleman Magawa, Martin Mpanduzi, Seif Shamte, Abdi Sasamaro, Emmanuel Mwamole,
Juma Mbega, Davis Munubi, Timoth Mwakisamba, Gabriel Tabana, Nkruma Kitagile na
Ramadhan Seif.
Timu ya Riadha iliundwa na Justa Tibendelana, Upendfo Gustaf, Mwajabu Bwire, Hemed Mtoa na Asante Nasary.
Benchi
la ufundi liliongozwa na Kocha Mkuu Spear Mbwembe, Kocha Msaidizi Said Albea,
Mwalinu wa Netiboli Paul Mathias, Timu Meneja Shaibu Kanyachole, Meneja wa
Vifaa Eliya Ngule na Daktari Janeth Mapunda.
Viongozi ambao
waliambatana na Timu ni Mwenyekiti Wilson Dede, Makamu Mwenyekiti Fidelis
Choka, Katibu Mkuu Robert Tende, Katibu Mkuu Msaidizi Theodosia Mwangoka, Mweka
Hazina Rajab Ally, Timu Meneja Antony Mfaume, Afisa Michezo Nkrumah Katagile,
Mjumbe Mwakilishi wa SHIMIWI Taifa Shaibu Kanyochole na Mjumbe Rajabu Mwaliko.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni