Jumatatu, 5 Agosti 2024

MKANDARASI UJENZI WA MAHAKAMA YA MWANZO IZIGO AKABIDHIWA ENEO LA MRADI

Na AHMED MBILINYI – Mahakama, Bukoba

Makabidhiano ya eneo kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Izigo katika Wilaya ya MulebaMkoa wa Kagera yalifanyika hivi karibuni na kushuhudiwa na Wawakilishi kutoka Makao Makuu ya Mahakama na Viongozi wengine.

Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza tarehe 17 August, 2024. Viongozi walioshuhudia makabidhiano hayo ni Mhandisi Peter Mrosso, Mkadiriji Majenzi (QS) Deogratius Lukansola, Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Bw. Lothan Simkoko na Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Muleba, Mhe. Daniel Nyamkerya.

Wengine ni Afisa Tawala Mwandamizi Mahakama Kuu Bukoba, Bw. Rojas Rwanyumba, Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Muleba, Bi. Edventina Semba, Msanifu Majenzi Mshauri (Consultant), Bw. Shempemba Elibariki kutoka Kampuni ya Norman and Dawbarn, Mkandarasi, Bw. Laurent Ambros pamoja na timu yake Kutoka kampuni ya Clalon Technologies. 

Mwenyekiti wa kikao hicho cha makabidhiano, Msanifu MajenziBw. Elibariki alielezea kuwa mradi huo ni wa muda wa miezi sita na utaanza rasmi tarehe 17 August, 2024 na unatarajiwa kukamilika tarehe 16 February, 2025.

Bw. Elibariki alimesisitiza mambo mbalimbali kwa Mkandarasi wa Mradiikiwemo kuzingatia muda kwani mradi huo unatekelezwa kwa fedha za Benki ya Dunia. Alisema pia kuwa uzalishaji taka uzingati kanuni zake katika kuziharibu.

Msanifu Majenzi pia alimsisitiza Mkandarasi kuzingatia mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wake pamoja na vibarua atakaowatumia, kujisajili Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), kutembelea Ofisi ya Manispaa kuonana na Mhandisi wa Manispaa na kuwaona Idara ya Zimamoto kabla ya kuanza shughuli za ujenzi.

Kwa upande wake, Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba aliahidi kuwapa ushirikiano Wakandarasi na kufanya mawasiliano na Taasisi zote zinazohusika kutoa vibali ndani ya Mkoa wa Kagera.

Mshauri Elekezi Msanifu Majenzi kutoka Kampuni ya Norman and Dawbarn, Bw. Shempemba Elibariki akimkabidhi nyaraka Mkandarasi, Bw. Laurent Ambros Kutoka Kampuni ya Clalon Technologies. Nyuma ni Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Bw. Lothan Simkoko.

Mshauri Elekezi Msanifu Majenzi, Bw. Shempemba Elibariki (mwenye shati rangi ya bluu bahari)kutoka Kampuni ya Norman and Dawbarn akionyesha wadau michoro na nyaraka nyinginezo za ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Izigo.

Mwenyekiti wa kikao, Mshauri Elekezi Msanifu Majenzi, Bw. Shempemba Elibariki kutoka Kampuni ya Norman and Dawbarn (mwenye shati rangi ya bluu bahari) akiongoza kikao, wa kwanza kushoto ni Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Bw. Lothan Simkoko.

Kiwanja cha ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Izigo kilichopo Kijiji cha Itoju, Kata ya Izigo,Wilaya ya Muleba katika Mkoa wa Kagera.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni