Na LIGHTNESS KABAJU-Mahakama, Kazi
Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi imefanya Kikao
cha Baraza la Wafanyakazi jana tarehe 28 Machi, 2025 mjini Morogoro ili kujadili
mambo mbalimbali yanayohusu wafanyakazi.
Kikao hicho kilifunguliwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo
ambaye pia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe.
Dkt. Yose Joseph Mlyambina.
Katika kikao hicho, Katibu wa Baraza alikuwa Bw.
Robert Mchocha na Katibu Msaidizi, Bw. Aloyce Lyimo, wote wakiwa Watumishi wa Mahakama
Kuu kutoka Divisheni hiyo.
Aidha, Wajumbe
wengine wa Baraza la Wafanyakazi katika kikao hicho walikuwa ni Watumishi wa Mahakama
Kuu Divisheni ya Kazi pamoja na wajumbe wengine kutoka Chama cha Wafanyakazi wa
Serikali na Afya (TUGHE).
Kikao kilianza kwa kuainisha agenda zilizoandaliwa wajumbe
walipata wasaa wa kujadili hoja mbalimbali zilizokusanywa na kupata mchakato
unaoendelea katika kutatua changamoto za
Wafanyakazi bila kuathiri utendaji kazi mahala pa kazi.
Naye Katibu Mkuu wa TUGHE wa Mahakama ya Tanzania, Bw.
Michael Masubo alipokea hoja hizo zilizojadiliwa na kupitishwa na Wajumbe kwa
ajili ya kuziwasilisha katika sehemu husika.
Vilevile katika kikao hicho, Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni
ya Kazi, Bw. Jumanne Muna aliwasilisha na kuwapitisha Wajumbe kwenye taarifa ya
utendaji kazi.
Kadhalika,Mhasibu Mkuu wa Mahakama hiyo, Bi. Joyce
Mulugu aliwasilisha bajeti ya Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kwa mwaka
2025/2026.
Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, Bw. Jumanne Muna akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwenye Baraza hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni