Alhamisi, 27 Machi 2025

JAJI MFAWIDHI MTWARA AFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI LINDI

Na Hilari Herman-Mahakama, Lindi

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Elias Kakolaki amefanya ziara ya siku mbili ya kikazi katika Mahakama zilizopo Mkoa wa Lindi kuanzia tarehe 24 na 25 Machi, 2025 huku akiwapongeza watumishi kwa kuchapa kazi kwa bidii.

Ikiwa ni mara yake ya kwanza kwa Jaji huyo kutembelea Mahakama za ngazi mbalimbali katika Mkoa huo tangia alipopangiwa majukumu ya kikazi kama Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mtwara miezi michache iliyopita.

Lengo la ziara ya Jaji Mfawidhi huyo ni kujitambulisha kwa watumishi kuzungumza na watumishi wa Mkoa wa Lindi na kujionea mazingira yanayotumika kutekeleze majukumu yao ya kila siku. Vilevile, kujua hali ya magereza katika mkoa huo na pia kuifahamu miradi ya ujenzi inayoendelea katika Mkoa huo.

Akizungumza na watumishi kwa nyakati tofauti tofauti wakati wa ziara hiyo. Mhe. Kakolaki apotembelea Mahakama za Wilaya ya Kilwa, Ruangwa, Lindi Mjini na Nachingwea aliwataka watumishi kuwa waadilifu wanaotekeleza majukumu yao kwa weledi na kwa kuwajibika. “Tukifanikiwa kutekeleza majukumu yetu kwa kugusa nyanja hizo tatu hakika tutakuwa tumeishi kauli mbiu ya Mahakama ya Tanzania ya Uadilifu, Ueledi na Uwajibikaji,” alisisitiza.

“Naomba kila mtumishi atambue kuwa yeye ni Kiongozi katika Kada yake, kwa nafasi yako unao wajibu na mchango mkubwa katika zoezi zima la utoaji haki kwa wananchi hivyo basi kila mmoja wetu akatoe huduma ilyobora kwa unyenyekevu, uadilifu, Lugha nzuri na kuzingatia maadili ya kazi zetu. Hii itasaidia kuboresha taswira ya Mahakama ya Tanzania na kurejesha imani ya wananchi na jamii kwa Mahakama,” alisema Jaji Kakolaki.

Aidha, Mhe. Kakolaki aliwaasa watumishi huo kuachana na matumizi ya karatasi, na hivyo kujikita zaidi katika matumizi ya mifumo ya TEHAMA huku akiwasisitiza Mahakimu kuongeza kasi katika kutumia mifumo ya uratibu wa mashauri ikiwa ni mfumo wa e-CMS (e-case management system) kwa Mahakama za Wilaya na Mahakama ya Hakimu Mkazi na mfumo wa kuratibu mashauri kwa Mahakama za mwanzo (primary court APP) ikiwa ni sambamba na matumizi ya mifumo mingine yote iliyoanzishwa na Mahakama ya Tanzania.

Vilevile, sanjari na kuwataka Mahakimu kutumia mifumo ya kitehama katika usikilizaji wa mashauri, pia aliwasisitiza Mahakimu hao kuongeza kasi ya usikilizaji wa Mashauri ili kutozalisha mashauri yenye umri mrefu (backlog).

Aidha, aliwataka Mahakimu kutoa dhamana kwa Mahabusu ambao wamekidhi vigezo vya dhamana ili kutimiza haki yao ya kisheria ya kupata uhuru huo. Kwa kufanya hivyo itapunguza msongamono usiowalazima magerezani na itaongeza nguvu kazi ya uzalishaji na maendeleo kwa taifa.

 Mhe. Kakolaki aliwataka watumishi kujiendeleza zaidi kielimu kwani  itawasaidia kujiimarisha  kimaslahi huku  akitoa wito wa kuleana kielemu yaani (Mentorship)  na zoezi hilo la kuleana kielemu litafunguliwa rasmi kwa kanda hii ya Mtwara hivi karibuni na kusisitiza kuwa zoezi hilo linagusa kada zote hivyo kila mmoja kwa nafasi yake awe tayari kumsaidia mwenzake.

Mhe. Jaji Kakolaki pia alitembelea miradi mitatu ya ujenzi inayoendelea katika Mkoa huo ikiwa ni pamoja na mradi wa Ujenzi wa kituo kidogo  Jumuishi Lindi cha utoaji haki (IJC), Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Mitandi iliyopo wilayani Kilwa na Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Ndomoni  iliyopo wilayani Nachingwea.

Katika ziara hiyo Mhe. Kakolaki amewataka wakandarasi wanaoendelea na ujenzi wa Miradi hiyo kuongeza kasi ili majengo hayo yakamilike kwa wakati na kutumika katika kutoa huduma ya haki kwa wananchi.

Sambamba na hilo, Mhe. Kakolaki aliambatana na viongozi mbalimbali wa ngazi za juu wa Mahakama Kanda ya Mtwara na Mkoa wa Lindi wakiwemo, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Seraphine Nsana, Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Bw. Yusuph Issa Msawanga na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Godfrey Mbeyela.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Elias Kakolaki akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Watumishi wa Mahakama za Lindi wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki wakati wa ziara hiyo.

Watumishi wa Mahakama za Lindi wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki wakati wa ziara hiyo.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano akiwasilisha taarifa ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Elias Kakolaki (hayupo pichani).


Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Godfrey Mbeyela akifafanua jambo wakati wa ziara ya Mhe.Jaji Mfawidhi (hayupo pichani) kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Bw. Yusuph Issa Msawanga.


Watumishi wa Mahakama mbalimbali kwa nyakati tofauti tofauti Mkoa wa Lindi wakisikiliza kwa makini ujumbe unaowasilishwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki (hayupo pichani).

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Elias Kakolaki akiteta na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa (hawapo pichani).

Watumishi wa Mahakama mbalimbali kwa nyakati tofauti tofauti Mkoa wa Lindi wakisikiliza kwa makini ujumbe unaowasilishwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki (hayupo pichani).

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki akiandika maneno katika ubao wa kumbukizi  ulipo katika Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki (wa pili kushoto) akikagua miradi ya ujenzi wa kituo jumuishi Lindi.

Ujenzi wa jengo la Mahakama Kituo Jumuishi Lindi hatua ilipofikia mpaka sasa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali alipokagua gereza la Wilaya ya Lindi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki akipanda mti katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi.


Watumishi wa Mahakama za Lindi wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki wakati wa ziara hiyo

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni