Na Iman Mzumbwe -
Mahakama, Songwe
Siku
ya Kimataifa ya Majaji na Mahakimu wanawake
ambayo husherehekewa tarehe 10 Machi kila Mwaka imewanufaisha wanafunzi
wa Shule ya Msingi Nuru iliyopo Wilaya Mbozi
Mkoani Songwe kwa Mahakimu Wanawake wilayani hapo kuadhimisha siku hiyo kwa kutoa
elimu kuhusu makosa ya kimtandao na unyanyasaji wa kijinsia katika jamii.
Akizungumza
katika zoezi hilo Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima
alitoe elimu kwa wanafunzi hao ya namna unyanyasaji kwa watoto unavyoweza
kuleta madhara kubwa katika jamii.
“Nitoe
rai kwenu wanafunzi kutojihusisha na vitendo visivyokuwa vya kiungwana na
vinavyokiuka maadili mema kama vile kulawitiana, kupiga picha utupu na
kushikana sehemu za siri, kufanya hivyo ni kosa la kijinai na adhabu yake ni
kifungo au faini au vyote kwa pamoja endapo mtu huyo atathibitika kufanya
hivyo,” alisema Mhe. Malima.
Aidha,
aliwataka wanafunzi hao kuwa wasiogope kutoa taarifa pindi wanapoona vitendo
hivyo kwani kufanya hivyo kutapunguza matendo hayo maovu vitendo hivyo vya
unyanyasaji.
Vilevile,
ni vema muonapo vitendo hivyo vya ukatili mnaweza kutoa taarifa maeneo kama
vile polisi, kwa wazazi, walimu, viongozi wa Serikali za mtaa na maeneo mengine
muhimu kulingana na wapi tukio limefanyika.
Naye,
Hakimu Mkazi Mahakama ya mwanzo Vwawa mjini, Mhe. Linah Okello alitoa elimu juu
ya makosa ya kimtandao jinsi yanavyoweza kuleta athari katika jamii hasa matumizi
ya simu za mkononi, umuhimu wa usajili wa laini za simu kupitia Mamlaka ya NIDA,
matumizi ya namba ya simu iliyosajiliwa kwa jina la mtu mwingine na matumizi
mabaya mitandao ya kijamii kama facebook, whatsapp na mitandao mingine ya
kijamii yanavyoweza kuchochea unyanyasaji na ukatili wa kijinsia.
Mhe.
Okello aliwaasa wanafunzi hao kuwa, kwa kutumia vibaya mitandao ya kijamii
kunaweza kusabisha au kumshawishi mtu akaanza kujihusisha na tabia mbaya za
unyanyasaji kama vile kulawiti, kujipiga picha zisizokuwa na maadili katika
jamii kama za utupu.
Aidha,
Mhe. Okello aliwatahadharisha wanafunzi hao kuwa, matumizi mabaya ya simu yanaweza
kusababisha mtu kufunguliwa kesi ya jinai kwa kosa ambalo hajalifanya yeye,
mathalani kuazima simu ya mtu mwingine pamoja kwa matumizi binafsi na kusajili laini
kwa kutumia namba ya NIDA ya mtu mwingine.
“Niwasihi
muendelee kuwa mabalozi kwa watoto wengine, wazazi, walezi na watu wengine
katika jamii kwa kufanya hivyo kutasidia kupunguza vitendo na makosa ya bila
kujua kama ni matendo ya unyanyaji wa kinjinsia yanayotokea katika jamii,”
alisisitiza Mhe. Okello.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Shule hiyo Bw. Festo John Mpepo alisema amefurahishwa na
zoezi hilo la utoaji elimu kwa wanafunzi wa shule hiyo, aliongeza kuwa, ni
nafasi ya pekee kwao na elimu hiyo itasidia kuepukana na vitendo ambavyo ni vya
unyanyasaji wa kijinsia.
“Nami nitoe rai kwa wanafunzi wangu watumie elimu hii kutusaidia kuielimisha jamii inayotuzunguka juu ya unyanyasaji wa kijinsia na matumizi mabaya ya mitandao yanayoweza kusababisha makosa ya jinai ya kimtandao katika jamii zetu,” alisema Mkuu huyo wa Shule.
Mkuu wa shule ya Bw. Festo John Mpepo akitoa shukurani kwa Mahakimu Wanawake wakiwa na baadhi ya Walimu waliokuwa wakiuliza maswali na kupata ufafanuzi zaidi kutoka kwa mahakimu hao
Mahakamu Wanawake wakiwa kwenye picha ya pamoja, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima (kushoto) Hakimu Mkazi Mahakama ya mwanzo Vwawa mjini, Mhe. Linah Okello (Kulia) ambao ni wawezeshaji wa zoezi la utoaji elimu katika shule ya msingi Nuru Wilaya ya Mbozi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni