Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Katika
taarifa za ukaguzi zilizotolewa kwenye Mahakama zilizokaguliwa asilimia kubwa
ilioneshwa namna mashauri ya mirathi yalivyoshughulikiwa kwa Mahakama zote za
wilaya hasa Mahakama ya Rungwe, Kyela na Mahakama ya Mkoa wa Songwe vile vile
na Mahakama zake za Mwanzo
Akifanya
kaguzi hizo kwa nyakati tofauti Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya
Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akiwa ameambatana na Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama
Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Hakimu Mfawidhi Mkoa wa Mbeya Mhe. Zawadi
Laizer pamoja kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya Bw. Alintula Ngalile
Jopo
hilo la ukaguzi hivi karibuni ilipokea taarifa za ukaguzi Mahakama ya Wilaya ya
Rungwe na Kyela na Mahakama zake za Mwanzo zikiwemo Mahakama ya Mwanzo Kiwila,
Ikama, Tukuyu Mjini, Katumba, Ipinda, Kyela Mjini na Busale.
Aidha,
taarifa hizo zilionesha kufanya vizuri zaidi kwenye kushughulikia mashauri ya
Mirathi ambayo kwa mwaka huu kikanda ndiyo ilikua kipaumbele na kulingana na
mikakati iliyowekwa ikiwemo kutangaza kwenye vyombo habari na makanisani na
kwenye ofisi za kata ilisaidia kuwafikia wadau wengi.
“Inatakiwa
Mahakama kufuatilia mirathi na kuhakikisha inalipwa kwa wakati na kupata
mrejesho baada ya mchakato mzima wa ulipaji kukamilika,” alisema Mhe. Tiganga
akiwa Wilayani Rungwe na Kyela
Aidha,
Mhe. Tiganga alipokea taarifa za hali ya majengo na changamoto zake kwani kuna
majengo ya baadhi ya Mahakama si yakulizisha mengi ni chakavu na baadhi kutokua
na hadhi.
“Ni
muhimu kusimamia viwanja vya Mahakama na kuvitambua mipaka yake kwani vikiachwa
bila uangalizi ni rahisi kuvamiwa na watu, tuainishe mipaka yake na tuvitafutie
hati.” Alisisitiza Mhe. Tiganga
“Nawapongeza
Mahakimu kwa kumaliza kesi na kahakikisha magereza halijai mahabusu” alisema Mhe.
Tiganga akiwa katika gereza la wilaya Kyela, vile vile alipata wasaa
wakutembelea jengo jipya la Magereza kwa wafungwa wanawake.
Wakati
huohuo, Mhe. Tiganga alipongeza Mahakimu kwa kuzingatia matumizi ya TEHEMA na
uendeshaji wa mashauri kwa njia ya mtandao na kuwasisitiza Mahakimu kuendelea
kutumia mifumo ya kimtandao ya Mahakama kuendeshea kesi.
Akiwa
wilayani Rungwe Mhe. Tiganga na timu yake walipokelewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi
wa Wilaya ya Rungwe Mhe. Jackson Banobi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya
Kyela Mhe. Andrew Njau.
Kwa
upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde akiwa na
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Judith Lyimo walipokea taarifa ya
ukaguzi ya Mahakama Mkoa wa Songwe, Mahakama za Wilaya na Mwanzo.
“Hongereni
kwa kushughulikia mashauri ya mirathi vizuri naona namba ya ulipaji na ufungaji
wa mashauri haya unaenda vizuri, cha kufanya ili tupige hatua zaidi inatakiwa
kupunguza milolongo ya kudai mirathi ili tuendelea kushughulikia kwa wakati,” alisema
Mhe. Kalunde akiwa na watumishi wa Mahakama mkoa Songwe.
Aidha,
Mhe. Kalunde aliwasisitiza Mahakimu walio na mashauri machache kuongeza ubora
wa kazi katika usikilizaji wa mashauri na uandishi wa maamuzi hasa kwa Mahakimu
wa Mahakama za Mwanzo.
Akiwa
Mkoa wa Songwe Mhe. Kalunde alipokelewa na Hakimu Mfawidhi wa Mkoa wa Songwe
Mhe. Francis Kishenyi pamoja na Mtendaji wa Mahakama ya Mkoa Songwe Sostenes
Mayoka.
Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Mahakama Mkoa wa Songwe, kulia ni
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akisaini Kitabu cha wageni katika ofisi ya Hakimu Mkazi
Mfawidhi Wilaya Rungwe.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni