Na ABDALLAH SALUM, Mahakama-Iringa
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru ameongoza Kikao cha Menejimenti ya Kanda hiyo na kutoa
rai kwa Mahakimu wa Kanda hiyo kutovuka mwaka huu na mashauri ya mlundikano
kwenye vituo vyao hasa Mahakama za
Mwanzo.
Akizungumza
katika Kikao cha Menejimenti cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2024/2025 kilichofanyika
jana tarehe 08 Julai, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Iringa, Mhe. Ndunguru ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kikao hicho alisema
uwepo wa mashauri ya mlundikano hauleti tija kwa Mahakama hizo.
Aidha,
Mhe. Ndunguru aliwataka wajumbe wa kikao hicho kufanya kazi kwa bidii na
uadilifu pamoja na kuwatia moyo watumishi walio chini yao wanaofanya kazi ndani
ya Mikoa ya Iringa na Njombe.
“Ni
vema kuwasimamia watumishi na kuwaongoza katika utendaji wa majukumu ya kila
siku pamoja kuwakumbuka watumishi ambao wapo chini yenu kwa mambo mazuri ili
waweze kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu,” alisema Jaji Ndunguru.
Vilevile,
Mhe.Ndunguru aliwataka wajumbe hao kufanya kazi kwa ubunifu ili waweze kukabiliana
na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utendaji wao wa kazi na
kuhakikisha chochote kinachokwamisha utendaji kazi kinatatuliwa kwa kubuni
mbinu mbadala.
Lengo
la kufanyika kwa kikao hicho ni kutathmini
utendaji kazi wa Mahakama za Mikoa ya Iringa na Njombe inayounda Kanda
ya Iringa.
Wajumbe wa kikao hicho walipokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za kimahakama na utawala ambazo maazimio mbalimbali yaliwekwa kwa ngazi zote za Mahakama za Mkoa wa Iringa na Njombe ili kuhakikisha huduma za haki zinawafikia wananchi kwa wakati.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni