Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Menejimenti
Kanda na Mahakama Mkoa wa Mbeya imekutana na kufanya kikao cha robo ya nne mwaka
2024/2025 ikiwa ni mwendelezo wa vikao vya menejimenti kwa kila robo ya mwaka kutathmini
utendaji kazi wa Mahakama Kanda na mkoa Mbeya.
Aidha,
vikao hivyo vilivyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya
na kuongozwa na Mwenyekiti wa vikao hivyo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga, huku katibu wake akiwa Mtendaji
wa Mahakama Kuu Kanda Mbeya Bi. Mavis Miti.
Akisoma
taarifa ya maazimo ya kikao kilichopita cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025
katibu wa kikao hicho Bi. Mavis Miti aliwasilisha maazimio na utekelezaji wa
maazimio hayo kwa wajumbe ikiwa ni ushughulikiaji wa mashauri ya mirathi,
matumizi ya TEHEMA kwa watumishi wa Mahakama hasa katika uendeshaji wa mashauri
kwa njia ya mtandao na kusajili mashauri kwa njia hiyo.
Vilevile,
Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya Bi. Mavis Miti na Mtendaji wa Mahakama Mkoa wa
Songwe Bw. Sostenesi Mayoka walitoa taarifa ya hali ya majengo ya baadhi ya
Mahakama kuwa katika hali ambayo siyo nzuri ambayo inahatarisha usalama wa
watumishi, pia hali ya ukosefu wa watumishi katika Mahakama za Mwanzo za Kanda
hiyo ya Mbeya.
Kwa
upande wake, Mhe. Joachim Charles Tiganga aliwapongeza wajumbe kwa kufanyaji
kazi mzuri katika vipaumbele walivyoazimia hasa katika kushughulikia mashauri
ya mirathi kwa wakati na kuwahimiza wanaodai mirathi kurudi kufunga mashauri
yao ya mirathi pamoja na matumizi ya Mahakama mtandao katika kusajili na kuendesha
mashauri kwa njia hiyo.
Mhe.
Tiganga aliwataka wajumbe waendelee kufanya kazi kwa bidii na kushirikiana kwa
kila ngazi katika kutekeleza majukumu na maazimio waliyojiwekea ili kufikia
malengo ya kile tunachokifanya.
“Ningependa
kutoa rai kwa wajumbe tuliopo hapa tufanye kazi kwa bidii na weledi na kuongeza
ubunifu ili kukabiliana na changamoto katika sehemu zetu kazi”
Mhe.
Tiganga pia aliwapongeza kwa jitihada wanazofanya Mahakimu katika utoaji wa
hukumu na kupunguza mahabusu magerezani ikiwa ni malengo yaliyowekwa toka kikao
cha robo ya kwanza ya Mwaka 2024/2025.
Wajumbe
wa vikao hivyo walipokea taarifa za Mirathi kwa ngazi zote za Mahakama na
taarifa za utekelezaji wa shughuli za kimahakama na kiutawala na kupitia
maazimio mbalimbali yaliyowekwa kwa robo ya tatu na kufahamu utekelezaji wa
maazimio hayo hasa katika kupunguza mashauri ya mlundikano, kutovuka na madeni
ya wazabuni, na utoaji wa mafunzo kwa watumishi wa Mahakama.
Miongoni wa wajumbe walioshiriki vikao hivyo ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Tanzania kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Hakimu Mfawidhi Mahakama Mkoa Mbeya Mhe. Zawadi Laizer na Hakimu Mfawidhi Mahakama Mkoa wa Songwe Mhe. Francis Kishenyi pamoja na Mahakimu wa Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim C. Tiganga (katikati), Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe.Aziza Temu (Kulia) na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti Kushoto wakiongoza vikao vya Menejimenti Kanda na Mkoa wa Mbeya.
Sehemu ya wajumbe wakifuatilia kikao cha menejimenti kanda
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni