Jumatatu, 1 Septemba 2025

JAJI MANYANDA ASISITIZA KUTUNZA VITENDEA KAZI VYA TEHAMA

Na Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe, Fredrick Manyanda amewataka watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga kutumia na kutunza vitendea kazi vya TEHAMA vilivyopo ili kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia.

Mhe. Manyanda aliyasema hayo tarehe hivi karibuni wakati wa kikao cha watumishi kilichofanyika katika ukumbi uliopo Mahakama Kuu Sumbawanga alipokuwa akifungua kikao hicho cha siku moja.

“Tuwe na utamaduni wa kuwa na vikao vya mara kwa mara kwani vikao vinasaidia kutatua changamoto zetu kwa umoja, pia tuwe wabunifu, tujiongeze pale tunapokuwa na changamoto na tufanye kazi kwa bidi.

Aidha, Mwenyekiti wa Kikao hicho Mhe. Manyanda aliongeza kuwa, katika zama za teknolojia ni vizuri vitendea kazi vya TEHAMA viendane na Mifumo ya TEHAMA iliyopo mahakamani hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kutumia na kutunza vitendea kazi hivyo.

Kwa upande wake, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano alihimiza kila mtumishi kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia miongozo na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na viongozi.

Naye, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu E. Essaba alisema Mahakama inaendelea kutatua changamoto mbalimbali za watumishi ikiwemo kulipa shahiki mbalimbali za watumishi kama vile nauli za likizo na pia kuwapeleka watumishi wa Kada mbalimbali kuhudhulia semina, mafuzo na makongamano mbalimbali yanayotekea ili kuwajengea uwezo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na watumishi kutoka Mahakama Kuu Sumbawanga, Mahakama ya Hakimu Mkazi Rukwa na Mahakama ya Wilaya Sumbawanga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda akiongoza kikao hicho cha watumishi

Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano akizungumza wakati wa kikao cha watumishi

Msaidizi wa Kumbukumbu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Sumbawanga Bw Ipyana Mwambebule akizungumza wakati wa kikao
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe, Lilian Ndelwa akizungumza wakati wa kikao

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu E.Essaba akifafanua jambo wakati wa kikao cha watumishi




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni