Jumatano, 29 Oktoba 2025

JAJI MKUU MAHAKAMA YA TANZANIA ASHIRIKI ZOEZI LA UPIGAJI KURA UCHAGUZI MKUU 29 OKTOBA, 2025

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 29 Oktoba, 2025 ameungana na Watanzania wengine nchini kutimiza haki yake ya Kikatiba kwa kushiriki katika zoezi la upigaji kura wa Rais, Wabunge na Madiwani katika Kituo cha kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Mhe. Masaju aliwasili katika viwanja vya Kituo hicho majira ya Saa 2 Asubuhi na kupokelewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ambaye pia ni Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk.

Yafuatayo ni matukio katika picha, Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akishiriki katika zoezi la Upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akiwa katika zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akidumbukiza karatasi ya kupigia kura mara baada ya kushiriki katika zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akiendelea na zoezi la upigaji kura katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akipakwa wino maalum kama ishara ya kumaliza zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Wasimamizi wa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani katika Kituo cha Kupigia kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma wakimhudumia Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju katika hatua za awali alipowasili kushiriki katika zoezi la upigaji kura.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akipokelewa na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk alipowasili kupiga kura katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma leo tarehe 29 Oktoba, 2025.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kushoto) akifurahia jambo na na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk mara baada ya kukamilisha zoezi la upigaji kura katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma leo tarehe 29 Oktoba, 2025.

(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni