Jumatatu, 27 Oktoba 2025

MAKAO MAKUU YA MAHAKAMA YAWAAGA WATUMISHI WASTAAFU

Na. Innocent Kansha na Halima Mnete, Mahakama

Mahakama ya Tanzania Makao Makuu na Mahakama ya Rufani jijini Dodoma tarehe 25 Oktoba, 2025 walifanya hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu wa Mahakama ikiwa ni ishara ya kuwaenza watumishi hao kwa utumishi wao uliotukuka na kuwapongeza kwa jitihada zao za kuitumikia Serikali kwa kipindi chote cha utumishi wao.

Akinzungumza katika hafla hiyo Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Bw. Victor Kategere alisema Mahakama ya Rufani ilikuwa na watumishi waliostaafu ambao walikuwa awajaagwa na Taasisi rasmi hivyo napenda kuwapongeza kwa utumishi wao kupitia hafla hii maalumu.

“Baada ya kukaa na kutafakari tumeona siku hii ya leo ni nzuri ili tuweze kuwaaaga wenzetu. Lakini tu nitoe historia ndogo kwamba mwaka jana kama mwezi wa 10 Viongozi wa madereva waliniambia tunataka kuwaaga madereva wenzetu ambao wamestaafu na bahati nzuri walikuwa wameshajiandaa ili niliwaomba wahairishe tujipange ili tuweze kulitekeleza kwa pamoja kwa muda utakao kuwa muafaka na leo tumeweza kulifanikisha kwa pamoja,” alisema Mtendaji wa Mahakama ya Rufani.

Mtendaji huyo ameongeza kuwa hafla hiyo ina lengo la kutambua mchango wa tatumishi hao wastaafu ambao kwa kipindi chote walikuwa waadilifu na wachakazi ambao walitumikia Mahakama, Umma, Serikali na Taifa kwa ujumla kwa zaidi ya miaka 30.

“Sasa tukio lenyewe ndo hili imefika muda wenyewe wa kuwaaga rasmi wenzetu itakumbukwa kwamba si madereva pekee nathani kuna watumishi wengine waliostaafu katika kipindi hicho ambao baadae watatambushwa ili tuwaone,” aliongeza Mtendaji.

Aidha, hafla hiyo ilitumika kuwakaribisha pia watumishi wa Mahakama ya Rufani walihamia Makao Makuu ya Mahakama na Rufani jijini Dodoma ikiwa ni ishara ya kuwakaribisha na kuwapongeza watumishi wote waliojaliwa kuhamia Dodoma kutoka Dar es salaam, mikoa mingine na Taasisi zingine.

Akito neno kwa niaba ya watumishi waliostaafu Mwandishi Mwendesha Ofisi Bi. Mameltha Simon Lumelezi alisema, mioyo yao inafuraha ya kupindukia kama wastaafu tuliolitumikia Taifa kwa uadilifu mkubwa sana hadi kufika hatua hii.

“Mimi nimetumika kwa miaka 35, nawaasa watumishi waendelee kuchapa kazi mpaka Mungu atakapowafikisha kama hapa tulipofika ni furaha sana kumaliza utumishi. Shukrani zingine ziwaendee viongozi wetu Mtendaji Mkuu, Wasajili, Majaji ambao hawapo hapa na watumishi wenzetu na watumishi wa Mahakama ya Rufani na Mahakama nyingine kwa sababu wengine tumeanzia mahakama mbali mbali. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu mzuri mliokuwa mnatuonyesha wakati tuko kazini na kutuita kuja kutuaga,” alisema Bi. Mameltha.

Wastaafu hao walioagwa katika hafla hiyo walikuwa ni Bw. Innocent Mgecha Dereva Mwandamizi, Bi. Siamini S. Magenge Msaidizi wa Ofisi, Bi. Joyce Shemdoe Mwandishi Mwendesha Ofisi, Bw. Samaidi Titi Sungu Msaidizi wa Ofisi, Bw. Romwald Dereva Mwandamizi, Bw. Joseph Chengula Dereva Mwandamizi, Bw. Thomas Mbwilo Dereva Mwandamizi, Bw. Donald Mwachisu Dereva Mwandamizi, Bw. Goha Muhoja Dereva Mwandamizi na Bw. Lema.

Watumishi Wastaafu wa Mahakama ya Rufani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Bw. Victor Kategere na Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani Mhe. Emmanuel Mrangu wakati wa hafla ya kuwaaga.

Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Bw. Victor Kategere akitoa neno la kuwakaribisha washiriki wakati wa hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu.

Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 
Sehemu ya watumishi wapya wa Mahakama ya Rufani waliokaribishwa na walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 
Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 
Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 


Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani walioshiriki kwenye hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu. 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Rufani wakikata keki ikiwa ni ishara ya kuwapongeza na kuwaaga watumishi wastaafu. 

Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Bw. Victor Kategere akitoa neno la shukurani kwa  washiriki wakati wa hafla ya kuwaaga watumishi wastaafu, kushoto ni Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani Mhe. Emmanuel Mrangu.

Watumishi Wastaafu wa Mahakama ya Rufani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Bw. Victor Kategere na Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani Mhe. Emmanuel Mrangu wakati wa hafla ya kuwaaga.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni