Jumatatu, 13 Oktoba 2025

TANZIA; MTUMISHI WA MAHAKAMA AFARIKI DUNIA

 TANZIA


Marehemu Patrick Michael Masenge enzi za Uhai wake.

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wake wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Musoma Mhe. Patrick Michael Masenge mwenye cheki namba 113357034 aliyekuwa ameajiriwa kwa nafasi ya Hakimu Mkazi II Mahakama ya Mwanzo Bunda Mjini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Musoma Bw. Leonard John Maufi, marehemu Patrick amefikwa na umauti tarehe 10. Oktoba, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu. Marehemu Patrick aliajiliwa na Mahakama mnamo tarehe 28 Mwezi wa 10 Mwaka, 2024

Taratibu za mazishi zinaendelea kuratibiwa na Mahakama kwa kushirikiana na familia.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni