TANZIA
Bi. Happiness Amos Majule enzi za uhai wake.
Mahakama ya
Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake Bi. Happiness
Amos Majule, aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Mahakama ya Wilaya ya
Meatu.
Kifo hicho kilichotokea mnamo
tarehe 09 Februari, 2026 siku ya Jumatatu katika hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini
Mwanza alipokuwa amelazwa kwa matibabu.
Marehemu Bi.happiness A.
Majule alizaliwa tarehe 11 April, 1969 na aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania
tarehe 04 Juni 1992 katika nafasi ya Msaidizi wa Ofisi.
Hadi umauti unamkuta, Bi
happiness alikuwa akihudumu katika Mahakama ya Mwanzo Kisesa.
Aidha, Bi. Happyness Amos
Majule anatarajiwa kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele mnamo tarehe 13
Februari, 2026 huko mkoani Singida Wilaya ya Iramba Kijiji cha Ulemo.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA
LIHIMIDIWE.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni