Jumatatu, 30 Machi 2026

MENEJIMENTI YA MAHAKAMA SONGEA YAFANYA KIKAO CHA ROBO YA TATU YA MWAKA

Na NOEL SYLIVESTER – Mahakama, Songea

Menejimenti ya Mahakama, Kanda ya Songea, tarehe 26 Machi 2026 ilifanya kikao cha tathmini ya utendaji kazi kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa  Saint Vicent, wilayani Nyasa na kilifunguliwa rasmi na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha, ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho.

Katika kikao hicho, taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mahakama kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2026 iliwasilishwa na Mtendaji wa Mahakama Kanda ya Songea, Bw. Allan Mwela, ambaye alihudumu pia kama Katibu wa kikao.

Akiwasilisha taarifa hiyo, Bw. Mwela alieleza masuala mbalimbali ikiwemo utawala bora, uwajibikaji pamoja na usimamizi wa rasilimali. Aligusia pia nguzo ya kwanza inayohusu utawala na usimamizi wa uendeshaji wa shughuli za Mahakama.

Naye Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya  Songea, Mhe. Lilian Rugalabamu, aliwasilisha taarifa inayohusu utoaji wa haki kwa wakati ambayo iligusia masuala ya usimamizi wa mashauri na usimamizi wa mashauri kwa njia ya mtandao (VC).

Kwa upande mwingine, Afisa Rasilimaliwatu wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea, Bi. Paulina Kapinga, aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mahakama kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2026.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha.

Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea, Mhe. Lilian Rugalabamu.

Mtendaji wa Mahakama Kanda ya Songea, Bw. Allan Mwela.

Afisa rasilimaliwatu, Bi.Paulina Kapinga (aliyesimama).

Habari hii imehaririwa na FAUSTNE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.


 

 

 

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni