Alhamisi, 26 Machi 2026

SONGWE YAJIVUA RASMI KUTOKA MAHAKAMA KUU KANDA YA MBEYA

Na. IMAN PATSON – Mahakama, Songwe

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga jana tarehe 25 Machi, 2026 alikabidhi rasmi eneo jipya la kiutawala la Mahakama Kuu Masjala Ndogo Kanda ya Songwe kwa Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo Mhe. Gabriel Malata, katika hafla iliyofanyika katika Jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.

Aidha, Mhe. Tiganga alifanya ukaguzi wa jengo hilo jipya ambapo alipitia miundombinu ya jengo na vifaa vya Ofisi na kisha kufanya makabidhi kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Songwe Mhe. Malata.

Mhe. Tiganga alipongeza wakandarasi wa Jengo hilo kwa kazi nzuri waliofanya na pia aliwasihi wafanyakazi wa jengo hilo kumalizia kazi iliyobakia kwa muda mfupi ili kazi zingine za kimahakama ziweze kuendelea.

Aidha, baada ukaguzi huo Mhe, Tiganga alifanya kikao cha kuagana na watumishi wa Mahakama Kanda ya Songwe na kuwashukuru kwa ushiriakiano alioupata kutoka kwao na aliwaahidi kuwa ataendelea kutoa ushirikiano wakati wote atakapo hitajika. Vilevile, aliwakumbusha umuhimu wa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi Mhe. Malata aliwasisitiza watumishi kuhusu suala la nidhamu, kuthaminiana, upendo, ulinzi wa miundombinu, vitendea kazi wa vya Ofisi na utendaji wa kazi mzuri kwa watumishi wote ili kuwezesha kutoa huduma bora ya haki kwa wananchi.

Mhe. Malata Uongozi wa Mahakama kwa kumteua kuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Songwe na kuahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha haki inatolewa kwa wananchi kwa wakati mapema ipasavyo.

Kufuatia makabidhiano hayo, Mhe. Tiganga aliambatana na Naibu Msajili Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu pamoja na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (kulia) akifanya makabidhiano na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (kushoto) kuashiria shughuli rasmi za Mahakama Kuu, Kanda ya Songwe.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo Kanda ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa kwanza kushoto) akionesha hati ya makabidhiano.

Muonekano wa Jengo la Mahakama Kuu Masjala Ndogo Kanda ya Songwe lilipofikia.

Mhandisi wa jengo jipya la Kituo Jumuishi cha Utoaji haki Kanda Songwe Bw. Victor akielezea maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo lilipofikia na akiahidi kuwa kufikia Aprili 1, 2026 jengo hilo litakua lipo tayari kwa matumizi.

Viongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe mara baada ya makabidhiano, wa tatu kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa tatu kulia), Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu (wa pili kushoto), Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Mhe. Joyce Minde (wa pili kulia), Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Bw. Sostenes Mayoka (wa kwanza

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni