Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga amefungua mafunzo
maalum ya Usihi na Usuluhishi kwa Naibu Wasajili na Mahakimu Wakazi kutoka
katika Kanda mbalimbali za Nyanda za Juu Kusini ikiwemo Mahakama Kuu Kanda ya
Mbeya, Iringa, Njombe, Sumbawanga, Songwe na Katavi.
Mafunzo
hayo yaliyofunguliwa tarehe 24 Machi, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mahakama
Kuu Kanda ya Mbeya. Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhe. Tiganga
alisema kuwa usuluhishi unalenga kuimarisha upatikananaji wa haki mapema
ipasavyo na kwa gharama nafuu.
“Usuluhishi
ni nguzo muhimu sana katika utoaji haki, kwani hupunguza migogoro baina ya
wanajamii na kupunguza gharama kwa wadaawa katika kutatua migogoro yao,”
alisema Mhe. Tiganga.
Kwa
upande wake, Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama
Lushoto (IJA) Mhe. Gloria Shuma akizungumza na washiriki alisema kuwa, mafunzo hayo yatakayodumu kwa muda wa siku
tatu yana lengo mahususi la kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani na kupunguza
athari za upatikanaji wa vidonda na makovu ambayo ni matokeo ya migogoro katika
jamii.
Aidha,
washiriki walieleza kuwa matarajio yao
katika mafunzo hayo ni kujifunza kwa kubadilishana uzoefu baina yao namna ya
kufanya usihi na usuluhishi, kujifunza namna ya kuwa wasuluhishi bora na
kubaini changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wa usuluhishi na namna ya
kuzitatua kwa pamoja.
Mafunzo
hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Mafunzo ya Utumishi wa Umma ya mwaka
2013, Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania pamoja na sera ya Mafunzo ya
Mahakama ya Tanzania ya mwaka 2019.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waheshimiwa Naibu Wasajili na Waheshimiwa Mahakimu Wakazi kutoka katika Kanda mbalimbali za Nyanda za Juu Kusini wanaoshiriki mafunzo hayo.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga (katikati) akiwa
kwenye picha ya pamoja na Viongozi ambao ni Naibu Wasajili wanaoshiriki Mafunzo
ya Usuluhishi kutoka Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
Sehemu
ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na
wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Sehemu
ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na
wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Sehemu
ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na
wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga (aliyesimama kwenye podium) akifungua mafunzo
hayo maalum kwa Waheshimiwa Naibu Wasajili na Waheshimiwa Mahakimu Wakazi.
Naibu
Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu (kushoto) akiwa sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo
Sehemu
ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na
wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Sehemu
ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na
wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Hakimu
Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Momba ambaye pia ni mwezeshaji Mhe. Raymond Kaswaga akitoa mada kwenye mafunzo hayo ya Usuluhishi
Sehemu ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mada zinazotolewa na wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.
Mratibu
wa mafunzo hayo Mhe. Gloria Shuma (kulia) kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) akifuatilia mafunzo hayo, kushoto ni Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya
Mhe. Franco Msuja
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni