Na FRANCISCA SWAI - Mahakama Musoma
Wafungwa na Mahabusu
katika Magereza tofauti ndani ya Mkoa wa Mara, wameipongeza Mahakama ya Tanzania,
Kanda ya Musoma, kwa namna inavyotoa huduma zake.
Pongezi hizo zimetolewa wakati
wa ukaguzi wa Magereza uliofanywa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya.
Katika ziara hiyo, Mhe.
Mtulya alitembelea na kukagua Magereza ya Tabora B, Gereza Mugumu na Gereza
Musoma. Aliambatana na Wadau wa Haki Jinai kwa ajili ya kusikiliza na kutatua
changamoto.
Pamoja na pongezi hizo, Wafungwa
na Mahabusu waliibua na kujibiwa changamoto zao mbalimbali, hasa wanazokutana
nazo kutoka kwa Wadau kuhusiana na namna wanavyokamatwa, upelelezi unavyofanyika
na uletaji wa mashahidi mahakamani.
Naye Mkuu wa Gereza la Musoma,
Afande John Murya, alimshukuru Jaji Mtulya kwa namna Mahakama inavyowapa
ushirikiano. Alieleza kuwa katika Gereza hilo wanaendelea na ujenzi wa jengo
litakalotumika kwa ajli ya Mahakama Mtadao (Virtual Court).
Aidha, katika ukaguzi huo
Mhe. Mtulya alitoa pongezi kwa Jeshi la Magereza kwa namna wanavyokaa na Wafungwa
na Mahabusu hao na namna wanavyowasaidia kwa kuwapa elimu juu ya masuala
mbalimbali ya kisheria na kijamii.
Zaidi aliwapongeza kwa
ushirikiano wao katika matumizi ya Mahakama Mtandao ili kuhakikisha utoaji wa
haki unafanywa kwa wakati kwakuwa jukumu la utoaji haki ni la pamoja kati ya
Mahakama na Wadau wake wote.
Jaji Mfawidhi pia
aliwaasa Wafungwa na Mahabusu hao pale watakapomaliza kutumkia adhabu zao,
wakawe raia wema, wazingatie sheria na taratibu za nchi ili kuleta amani na
ustawi kwa Taifa na familia zao.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya (mbele) akiwa anasisitiza
jambo katika taarifa iliyosomwa kwake na Kaimu Mkuu wa Gereza la Wafungwa Tabora
B, Afande Majuto Mabele (wa kwanza kulia kwa Mhe. Mtulya) pamoja na Viongozi,
Wadau na Watumishi wa Mahakama.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya (mbele) akiwa anafuatilia
na kusisitiza taarifa iliyotolewa na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe.
Monica Ndyekobora (aliyesimama), wakati wa kujadili changamoto za Wafungwa
katika kikao chake na watumishi wa Mahakama Serengeti pamoja na Wadau wa Haki
Jinai walipotembelea Gereza la Wafungwa Tabora B.
Jengo linaloendelea na ujenzi kwa ajili ya kutumiwa kwa shughuli za Mahakama Mtandao katika Gereza Musoma.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma
.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni