Jumamosi, 9 Mei 2026

BSAAT YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Kisutu

Mradi wa Mfumo Endelevu wa Kupambana na Rushwa Tanzania (BSAAT), hivi karibuni umekabidhi vifaa mbalimbali vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Hakimu Mkazi Mkuu na Afisa Mwambata wa BSAAT, Mhe. Richard Kabate, alikabidhi vifaa hivyo kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mhe. Franco Kiswaga, huku zoezi hilo likishuhudiwa na   Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Bi. Athanasia Kabuyanja.

Watumishi wengine wa Mahakama waliokuwepo wakati wa makabidiano hayo ni Ofisa Utumishi Mwandamizi, Bw. Nkruma Katagira, Mhasibu Mwandamizi, Bi. Prisca Gideon na Ofisa TEHAMA wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Bw. Winfred Nzilano.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni Kompyuta Mpakato tano (5) aina ya HP Omnibook X Flip, Begi za Kompyuta Mpakato (Laptop bag) tano (5), Adapta (Type C to HDTV 11 in 1 Adapter) na Vipanya vya Kompyuta (wireless mouse) tano (5) na Vipanga Njia (Portable router) tano (5).

Akizungumza waakati wa zoezi hilo, Mhe. Kabate aligusia umuhimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi katika mapambano dhidi ya rushwa na kwamba Mahakama ya Kisutu imekuwa ikipokea kesi nyingi ambazo zinahusiana na maswala ya rushwa.

Hivyo, alibainisha kuwa makabidhiano hayo ni katika kuhakikisha uondoaji wa mianya ya rushwa katika mifumo ya Mahakama na kuongeza wigo wa kushughulikia mashauri ya rushwa.

Naye Hakimu Mfawidhi aliushukuru uongozi wa Mahakama ya Tanzania kwa kuona kwamba inafaa kuwaletea vitendea kazi. Alisema watavitumia vifaa hivyo kuhakikisha mashauli yanamalizika kwa haraka iwezekanavyo kama kauli mbiu ya Mahakama inavyosema.


Hakimu Mkazi Mkuu na Afisa Mwambata wa Mradi wa Mfumo Endelevu wa Kupambana na Rushwa Tanzania, Mhe. Richard Kabate (kushoto), alikabidhi vifaa hivyo kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mhe. Franco Kiswaga (katikati). Picha chini, Mhe. Kiswaga akizungumza baada ya makabidhiano hayo.


Picha ya pamoja baada ya makabidhiano hayo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Njombe.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni