Jumapili, 21 Juni 2026

JAJI KIONGOZI ZIARANI MKOANI RUVUMA

  • Kukagua Mahakama, Magereza
  • Kuteta na Mkuu wa Mkoa, kuzungumza na Watumishi

Na FAUSTINE KAPAMA na Noel Daud-Mahakama, Songea

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, amewasili mkoani Ruvuma leo tarehe 21 Juni, 2026, kufanya ziara ya kimahakama ya siku tano, kukagua Mahakama na Magereza.

Mhe. Dkt. Siyani amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Songea majira ya saa 5.00 asubuhi akiwa ameambatana na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Songea, Mhe. James Karayemaha, na kupokelewa na Viongozi wa Mahakama.

Viongozi waliokuwa Uwanja wa Ndege kumpokea Jaji Kiongozi ni Jaji wa Mahakama Kuu Songea, Mhe. Dkt. Emmanuel Kawishe, Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa, Naibu Wasajili wa Mahakama Kuu Songea, Mhe. Elizabeth Nyembele na Mhe. Asha Waziri.

Wengine ni Mtendaji wa Mahakama Songea, Bw. Allan Mwela, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Songea, Mhe. Lilian Rugarabamu, Mahakimu na Watumishi wengine wa Mahakama Songea.

Ratiba iliyotolewa mjini hapa inaonesha kuwa JaJi Kiongozi ataanza ziara yake kwa kutembelea Mahakama ya Wilaya Nyasa na kufanya kikao na Watumishi, kabla ya kuelekea Wilaya ya Mbinga na kuongea na Watumishi na kukagua Gereza la Wilaya ya Mbinga.

Kesho yake, kwa mujibu wa ratiba hiyo, Mhe. Dkt. Siyani ataelekea kwenye Gereza la Mkwaya kufanya ukaguzi na baadaye kugagua Gereza lingine la Kitai, yote yakiwa katika Wilaya ya Mbinga.

Siku ya tatu, Jaji Kiongozi atamtembelea Mkuu wa Mkoa, Mhe. Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, na kufanya naye mazungumzo mafupi na baadaye kufanya ukaguzi katika Gereza Kuu Songea.

Siku hiyo hiyo, Mhe. Dkt. Siyani atatembelea Mahakama Kuu Songea na kufanya mazungumzo mafupi na Jaji Mfawidhi na kisha kuongea na Watumishi wa Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama ya Wilaya pamoja na Mahakama zote za Mwanzo Songea mjini.

Siku ya nne, Jaji Kiongozi atatemebelea Mahakama ya Wilaya Namtumbo na kuzungumza na Watumishi na kisha kuelekea Wilaya ya Tunduru kufanya ukaguzi kwenye Gereza la Tundura, kabla ya kufanya kikao na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Tunduru na Mahakama za Mwanzo katika Wilaya hiyo.

Siku ya tano, Mhe. Dkt. Siyani atafanya kikao cha majumuisho ya ziara katika Mahakama ya Wilaya Tunduru, kikihusisha Watumishi wote kutoka maeneo tofauti mkoani Ruvuma.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akisalimiana na Jaji wa Mahakama Kuu Songea, Mhe. Dkt. Emmanuel Kawishe, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege Songea kuanza ziara ya kimahakama mkoani Ruvuma.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akisalimiana na Meja Jenerali wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kamanda Brigedi ya Kusini, Charles Feruzi, walipokutana uwanjani hapo.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani akisamiana na Naibu Msajili, Mhe. Asha Waziri.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akisalimiana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Songea, Mhe. Lilian Rugarabamu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Songea, Mhe. James Karayemaha akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Mahakama kwenye Uwanja wa Ndege Songea.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Songea, Mhe. James Karayemaha, akisalimiana na Mtendaji wa Mahakama Songea, Bw. Allan Mwela.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akisaini kitabu cha wageni kwenye Chumba cha Wageni Mashuhuri kwenye Uwanja wa Ndege Songea. Picha chini akiwa kwenye mapumziko uwanjani hapo.


Picha na Noel Daud-Mahaama, Songea.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni