Jumatano, 8 Julai 2026

TANZIA; HAKIMU MKAZI MFAWIDHI MAHAKAMA YA WILAYA KALIUA-TABORA AFARIKI DUNIA

 
Marehemu Anna Eliya Chilongola enzi za uhai wake.

Ratiba ya mazishi ya aliyekuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kaliua, Marehemu Anna Eliya Chilongola.

TANZIA

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake aliyekuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kaliua- Tabora, Mhe. Anna Eliya Chilongola.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora, Bw. Emmanuel Munda, marehemu Anna alifariki dunia tarehe 03 Julai, 2026 katika Hospitali ya Mtakatifu Gemma mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.Amesema, msiba upo nyumbani kwa marehemu Chang'ombe ‘Extension’- Dodoma.

Bw. Munda amesema kuwa, mazishi yanatarajia kufanyika tarehe 08 Julai, 2026 leo saa 7 Mchana katika Makaburi ya Chang’ombe jijini Dodoma.

Mahakama ya Tanzania inaungana na Ndugu, Jamaa na Marafiki katika kipindi hiki cha majonzi ya kuondokewa na Mpendwa wetu Anna Eliya Chilongola.

BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE.

 

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni