Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Watumishi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya, wamefanya ziara ya kitalii
katika Hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya kuwapa fursa ya
kupumzika, kujifunza, kutambua na kuthamini urithi wa asili na utamaduni wa
Tanzania.
Ziara
hiyo ya kitalii katika hifandhi ya Ngorongoro imeongozwa na Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya, akiwa
Pamoja na viongozi wengine wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya.
Akiongoza
ziara hiyo, Mhe. Mtulya amesisitiza umuhimu wa watumishi kupata fursa za
kujifunza na kutembelea maeneo mbalimbali, akieleza kuwa shughuli hizo zina
nafasi katika kujenga mahusiano mazuri, kuimarisha mshikamano na kuongeza ari
ya watumishi katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Viongozi
walioshiriki katika ziara ya kitalii ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo, Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe.
Zawadi Laizer, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Festo
Chonya, Mahakimu wakiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya
Mhe. Tedy Mlimba na watumishi wengine kutoka vituo mbalimbali vya Masjala Ndogo
ya Mbeya.
Watumishi
hao walipata fursa ya kutembelea na kujifunza kuhusu vivutio vya kiutalii
vilivyopo katika eneo la Ngorongoro na kujionea wanyama na Ndege wa aina
mbalimbali wanaopatikana katika hifandhi hiyo maarufu Duniani inayopatikana Tanzania.
Miongoni
mwa maeneo yaliyotembelewa ni Bonde la Ngorongoro, eneo linalojulikana kwa
utajiri wake wa wanyamapori na mandhari ya kipekee ya kijiolojia. Eneo la
Ngorongoro pia ni miongoni mwa maeneo yenye hadhi ya urithi wa dunia kutokana
na umuhimu wake wa asili, kiikolojia na kiutamaduni.
Watumishi
hao pia walitembelea Ziwa Manyara pamoja na Makumbusho ya Ngorongoro–Lengai
UNESCO Global Geopark, ambako walipata fursa ya kujifunza kuhusu historia,
jiolojia, mazingira, utamaduni na namna ambavyo urithi wa asili unavyohifadhiwa
na kutumika kwa ajili ya elimu na utalii.
Mbali
na shughuli za utalii, ziara hiyo pia iliwawezesha watumishi hao kutembelea
Mahakama Kuu ya Tanzania Kituo Jumuishi cha utoaji haki Arusha, hatua
iliyolenga kuwapa fursa ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuimarisha
mahusiano ya kikazi baina ya watumishi wa Mahakama kutoka Masjala hizo.
Ziara
hiyo ya kiutalii imekuwa pia fursa ya kuwapa watumishi nafasi ya kujenga
mshikamano, kuimarisha mahusiano baina yao na kupata muda wa kupumzika nje ya
mazingira ya kawaida ya kazi, jambo linaloweza kuchangia kuongeza ari, morali
na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Ziara
hiyo imehitimisha kwa kuwa fursa muhimu kwa watumishi wa Mahakama ya Tanzania Masjala
Ndogo ya Mbeya kujifunza zaidi kuhusu utajiri wa asili, historia, utamaduni na
vivutio vya utalii vilivyopo nchini, huku wakijenga kumbukumbu na uzoefu ambao
utachangia kuimarisha mshikamano na mahusiano yao ya kikazi.
Watumishi
wa Mahakama ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa mbele ya lango Kuu la
kuingilia hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.
Picha na matukio mbalimbali ya Viongozi na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo y a Mbeya wakiwa katika ziara hiyo ya utalii katika hifadhi ya Ngorongoro.
Picha na matukio mbalimbali ya Viongozi na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo y a Mbeya wakiwa katika ziara hiyo ya utalii katika hifadhi ya Ngorongoro.
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa katika
eneo la ziwa Manyara ambapo ilikuwa sehemu ya ziara hiyo ya kitalii.
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa mbele
ya Jengo la Mahakama Kuu ya Tanzania, Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki jijini Arusha.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), Naibu
Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo (kushoto) na Mtendaji
wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya (kulia) wakiwa mbele
ya lango la kuingilia hifadhi ya ngorongoro walipotembelea katika hifadhi hiyo.
Watumishi
wa Mahakama ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya wakipewa maelekezo na historia
ya Hifadhi ya Ngorongoro kutoka kwa Mwongoza watalii (wa kwanza kushoto)
Picha
na matukio mbalimbali ya Viongozi na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo y
a Mbeya wakiwa katika ziara hiyo ya utalii katika hifadhi ya Ngorongoro.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpg)
.jpeg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni