Ijumaa, 18 Septemba 2026

JAJI MTULYA AHITIMISHA ZIARA YA UKAGUZI WA MAHAKAMA ZA CHINI

Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya amekamilisha ziara ya siku 14 ya kukagua na utambuzi wa Mahakama za Wilaya na Mwanzo kwa lengo la kutathmini utendaji kazi, kubaini mafanikio, changamoto katika utoaji wa huduma za haki pamoja na kuangalia hali ya miundombinu na mazingira ya kazi.

Ziara hiyo iliyoanza tarehe 03 Septemba, 2026 na kuhitimishwa tarehe 16 Septemba, 2026 imehusisha kutembelea vituo vya Mahakama vilivyopo katika Wilaya za Kyela, Rungwe, Mbarali, Chunya na Mbeya, ambapo jumla ya vituo 48 vilitembelewa, vikiwemo vinavyotoa huduma na vile ambavyo kwa sababu mbalimbali havitoi huduma kwa sasa.

Katika ziara hiyo, Viongozi hao walifanya ukaguzi wa majengo, viwanja, mali za ofisi, mazingira ya kazi na upatikanaji wa huduma za Mahakama, pia walitembelea maeneo mbalimbali yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Mahakama.

Aidha, ukaguzi huo umewezesha kubaini hali halisi ya vituo mbalimbali, ikiwemo baadhi ya majengo chakavu, vituo ambavyo majengo yake hayatumiki au yameharibika, pamoja na maeneo yenye viwanja pekee bila majengo ya Mahakama.

Ziara imebaini hatua mbalimbali zinazochangia kuboresha utoaji wa huduma za haki ikiwemo usikilizwaji wa mashauri kwa wakati, matumizi ya mfumo wa ‘Primary Court App’ katika Mahakama za Mwanzo, upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, ukarabati mdogo wa majengo na vifaa vya Ofisi, pamoja na kuimarika kwa ushirikiano kati ya Mahakama na wadau mbalimbali.

Katika baadhi ya vituo, ziara imebaini mafanikio katika kufunga mirathi kwa wakati, utoaji wa nakala za hukumu na mienendo kwa wakati, utoaji wa elimu kwa umma, pamoja na kuendelea kwa jitihada za kuimarisha mazingira ya utoaji wa huduma za haki.

Hata hivyo, ukaguzi umebaini changamoto zinazohitaji hatua za kimkakati, zikiwemo uchakavu wa baadhi ya majengo yanayotumika kutoa huduma za kimahakama, upungufu wa watumishi, ukosefu wa huduma muhimu kama maji katika baadhi ya vituo, upungufu wa Samani za ofisi, pamoja na baadhi ya viwanja vya Mahakama kutokuwa na hati miliki na alama za kudumu za mipaka.

Viongozi hao kupitia ziara hiyo, walitoa maelekezo mbalimbali kwa uongozi wa vituo husika, yakilenga kuharakisha hatua za upatikanaji wa hati na alama za mipaka ya viwanja, kuboresha miundombinu, kuongeza kasi ya usikilizwaji na ukamilishaji wa mashauri, kutoa nakala za hukumu kwa wakati, pamoja na kuimarisha usimamizi wa karibu wa utendaji kazi wa Mahakama.

Aidha, katika vituo ambavyo huduma za Mahakama hazipatikani, viongozi walifanya tathmini ya sababu za kutokuwepo kwa huduma hizo na kutoa maelekezo yanayolenga kuweka mazingira wezeshi ya kurejesha au kuimarisha huduma, ikiwemo kuhamasisha ushirikiano na Serikali za Vijiji na wadau wengine katika ujenzi wa majengo ya Mahakama.

Uongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya utaendelea kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa katika vituo mbalimbali, kwa lengo la kuhakikisha maboresho yaliyobainika yanatekelezwa na huduma za haki zinaendelea kutolewa kwa ufanisi, kwa wakati na katika mazingira yanayokidhi mahitaji ya wananchi na watumishi wa Mahakama.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Madibira alipotembelea Mahakama hiyo alipokuwa ziarani wilayani Mbarali.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Watoto Mbeya.


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa ndani ya Ofisi ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Rungwe, alipotembelea alipokuwa katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kulia), akikagua miundombinu ya TEHAMA katika Chumba cha TEHAMA Mahakama ya Mwanzo Madibira.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakipokelewa na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Chunya na Mahakama ya Mwanzo Chunya Mjini. 

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Chunya na Mahakama ya Mwanzo Chunya Mjini wakimsikiliza Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani), ndani ya ukumbi wa Mahakama ya Wilaya Chunya.


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wengine alioambatana nao na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Rungwe alipotembelea Mahakama hiyo  

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo pamoja na viongozi wa Mahakama ya Wilaya Chunya na Diwani wa Kata ya Makongorosi (watatu kushoto) wakiwa mbele ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Mkongorosi linalojengwa na nguvu ya Wananchi na wadau mbalimbali wakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni