Na EUNICE LUGIANA, Mahakama-Kibaha
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe Awamu Mbagwa amefanya ukaguzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha na Mahakama ya Wilaya Kibaha ili kuangalia mwenendo wa mashauri na masuala ya utawala.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo tarehe 17 Septemba, 2026, Mhe. Mbagwa alisema ukaguzi huo ni wa kawaida unaofanyika kila baada ya robo mwaka.
Akitoa taarifa ya utekelezaji ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha-Pwani, Naibu Msajili na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani, Mhe. Joyce Mkhoi alisema Mahakama mkoani humo ina jumla ya Mahakama za Wilaya saba na Mahakama za Mwanzo 40.
Amesema, katika utekelezaji wa maagizo ya Viongozi Wakuu wa Mahakama Mkoa wa Pwani umejitahidi kupanga mashauri kwa kuzingatia muda, pia uondoshaji wa mashauri ya mlundikano inaridhisha kwa kuzingatia maelekezo, wananchi wanapata huduma katika Mhakama ya Hakimu Mkazi kulingana na taratibu.
“Wananchi wanapata huduma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kulingana na taratibu zilizopangwa na pia usikilizwaji wa mashauri kupitia Mahakama Mtandao (Virtual Court) unaendelea kuzingatiwa kipindi cha Julai-Septemba, 2026 yamesikilizwa mashauri saba kwa njia ya mtandao (VC)” amesema Mhe. Mkhoi.
Akizungumzia kuhusu uelewa wa watumishi juu ya Mpango Mkakati na Programu ya Maboresho ya Mahakama, Naibu
Msajili huyo amesema elimu inatolewa
kupitia vikao vya kila wiki ikiwa ni pamoja
na kufanya tathmini ya kazi zillizofanyika ndani ya wiki na kuelimishana.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mahakama ya Wilaya Kibaha, naye Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibaha, Mhe. Emmael Lukumai amesema Mahakama pamoja na Wadau wa Haki wamekuwa na vikao vya mara kwa mara vya kujadiliana namna bora ya uendeshaji wa mashauri na kuondokana na mashauri ya mlundikano ambapo wameweza kuondoa mlundikano wa mashauri mahakamani na vikao hivyo vimekuwa vikizaa matunda.
Mhe Lukumai amesema pia, elimu kwa umma imekuwa ikitolewa kwa ajili ya ufafanuzi wa taratibu za Mahakama na sheria mbalimbali, ambapo Mahakama ya Wilaya Kibaha na Mahakama zake za Mwanzo wametenga muda wa siku moja kwa juma muda wa nusu saa kabla ya kuanza kwa mashauri kwa kuweka ratiba maalum ambayo kila Idara ndani ya Mahakama inakuwa na siku ambayo inatoa elimu kwa wananchi.
Kadhalika, Mfawidhi huyo ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi ya Julai mpaka Septemba ambapo ni pamoja na kutoa huduma kwa wakati na kutoa nakala za hukumu mara baada ya kumaliza kusikiliza shauri, kumaliza na kuzuia mashauri mlundikano, kutoa elimu na mengine.
Katika ziara hiyo, Jaji Mhe. Mbagwa aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Hussein Mushi, Msaidizi wa Sheria wa Jaji, Mhe. Bitulo Magafu na Ofisa Utumishi wa Kanda hiyo, Bi. Winifrida Shirima.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Hussein Mushi akitambulisha msafara wa Jaji Awamu Mbagwa baada ya kuwasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani na Mahakama ya Wilaya Kibaha kwa ajili ya ukaguzi. Aliyeketi kulia ni Msaidizi wa Sheria, Mhe. Bitulo Magafu.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni