Na. Christopher Msagati – Mahakama, Manyara
Mahakama
Kuu Kanda ya Manyara imewapokea Majaji wanne kutoka Mahakama Kuu Zanzibar kwa
ajili ya ziara ya mafunzo ya wiki moja ili kubadilishana uzoefu katika shughuli
za uendeshaji wa mashauri mbalimbali yakiwemo mashauri ya uhujumu uchumi
yatayaoanza kusikilizwa Mahakamani hapo hivi karibuni.
Akizungumza
wakati wa mapokezi ya Majaji hao, Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya
Manyara Mhe. Devotha Kamuzora aliwapongeza wageni hao kwa kuichagua Mahakama
Kuu Manyara kwa ajili ya kujifunza kwa kuwa Mkoa wa Manyara una mashauri ambayo
katika Kanda nyingine huwa hayasikilizwi kwa wingi kama ilivyo katika Kanda ya
Manyara.
“Waheshimiwa
Majaji karibuni sana Manyara na ninawapongeza kwa kuichagua Kanda yetu kwa
ajili ya kujifunza, Kanda yetu ina mashauri mengi sana yanayohusu Uhujumu
Uchumi, Madawa ya Kulevya na Nyara za Serikali. Hivyo ninaamini kuwa mmechagua
Kanda sahihi kwa ajili ya mafunzo yenu” alisema Mhe. Jaji Kamuzora.
Majaji
ni Mhe. Fatma Hamidi Mahmoud, Mhe. Said Hassan Said, Mhe. Salma Ali Hassan pamoja
na Mhe. Khadija Shamte Mzee. Katika ziara hiyo wameambatana pia na Naibu
Mrajisi wa Mahakama Kuu ya Zanzibar Mhe. Hussein Makame Hussein.
Akiongea
wakati wa mapokezi hayo, Mhe Fatma Mahmoud Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar
aliushukuru uongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara kwa kuwapokea na
kuwawezesha kupata mafunzo hayo.
“Viongozi
na watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara tunawashukuru kwa kutupokea na
kutuwezesha kuyapata mafunzo haya. Tunaamini katika wiki nzima hii ambayo
tutakaa pamoja tutajifunza mengi kutoka kwenu na tukirudi Zanzibar yatakuwa
tija katika utendaji kazi wetu” alisema Mhe. Fatma Mahmoud.
Mahakama
Kuu Manyara imeanza kikao cha wiki moja cha kusikiliza mashauri ya Uhujumu
Uchumi ambacho kinaongozwa na Mhe. Jaji Devotha Kamuzora kuanzia tarehe 22
Septemba 2025 mpaka tarehe 26 Septemba 2025. Kikao hiki ndicho kinachotumiwa na
Majaji hao kutoka Zanzibar kwa ajili ya kujifunza mienendo ya mashauri ya
Uhujumu Uchumi.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara Mhe. Devotha Kamuzora (wa nne kutoka kushoto) akiwa pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu
Zanzibar waliofika Manyara kwa ajili ya Mafunzo ya Uendeshaji wa Mashauri ya
Uhujumu Uchumi.
Waheshimiwa
Majaji wakiwa wanaangalia ukumbi wa Wazi wa Mahakama Kuu Manyara ambao
ungetumika kabla ya kuanza mafunzo ya Uendeshaji wa Mashauri ya Uhujumu Uchumi.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara Mhe. Devotha Kamuzora akiwatembeza na kuwaonesha miundombinu ya Mahakama Kuu Manyara kabla ya kuanza
kwa mafunzo.
Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar Mhe. Khadija Shamte Mzee akiangalia chumba
cha kuhifanyia nyaraka mbalimbali kinachotumiwa na Mahakama Kuu Manyara, akimeambatana na Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar Mhe. Salma Ali Hassan.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara Mhe.
Devotha Kamuzora akiwakaribisha waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu Zanzibar ambao wametembelea
Mahakama Kuu Manyara kwa ajili ya Mafunzo ya Uendeshaji wa Mashauri ya Uhujumu
Uchumi.

.jpg)

.jpg)
.jpg)
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni