Jumanne, 4 Novemba 2025

JAJI MKUU WA MAHAKAMA YA TANZANIA AMUAPISHA MHE.DKT. SAMIA NA MAKAMU WAKE

·       Rais Samia asisitiza amani, umoja na mshikamano kwa Watanzania

·       Azitaka Kamati za Ulinzi na Usalama nchini kurejesha amani na utulivu ili maisha ya Watanzania yaendelee kama kawaida

·       Marais wa Burundi na Zambia nao wawasihi Watanzania kudumisha sifa ya amani ya Tanzania

Na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju amemuapisha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Awamu ya Sita ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  katika kipindi cha pili.

Kadhalika, Mhe. Masaju amemuapisha Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hafla ya uapisho ilifanyika tarehe 03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma na kushuhudiwa na wageni mbalimbali akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Marais na Viongozi kutoka Nchi mbalimbali za Afrika akiwemo Rais wa Burundi, Rais wa Zambia, Rais wa Msumbiji, Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na kadhalika.

Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Mabalozi kutoka Nchi mbalimbali, Viongozi wa Serikali, Bunge, Mahakama, Viongozi wa Dini na Wananchi kwa ujumla.

Akizungumza mara baada ya uapisho, Mhe. Dkt. Samia aliwasihi Watanzania kuendelea kulinda itikadi ya umoja, amani na mshikamano ambapo alisema, “ndugu zangu wote tunaoitakia mema Nchi hii ‘Tanzania’ tumesikitishwa na vitendo vya uvunjifu wa amani, upotefu wa maisha na uharibifu wa mali za umma na mali za watu binafsi kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini hasa kwenye Majiji na Miji, kilichotokea hakiendani na taswira na sifa za Kitanzania na sio Utanzania.”

Rais Samia alisema, Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini vinaendelea kufuatilia na kuchunguza kwa undani zaidi kilichotokea na kuirudisha nchi katika hali iliyozoeleka kwa haraka.

Aidha, Mhe. Dkt. Samia alizitaka Kamati ya Kitaifa ya Ulinzi na Usalama na Kamati za Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuanzia jana tarehe (03 Novemba, 2025) maisha ya wananchi yanarejea katika hali ya kawaida mara moja.

“Amesema hapa Rais wa Zambia na Rais wa Burundi, machafuko ndani ya nchi si mema hayana thamani na sifa eidha kwa yeyote yule, kwahiyo ndugu zangu niwaombe sana, tuzingatia umoja, amani na utulivu wa nchi yetu,” alisisitiza Rais Samia.

Kadhalika, Mhe. Dkt. Samia alitoa onyo kwa wote waliochochea uvunjifu wa amani, ambapo alisema, “nitumie fursa hii kutoa onyo kama mama kwa wale wote waliochochea uvunjifu wa amani na nawataka watambue kuwa, vurugu na uvunjifu wa amani huishia kupimana nguvu na uwezo wa kujihami ila mazungumzo huzaa mshikamano sasa tuchague lenye manufaa kwetu kwani usalama wa Taifa lolote hulindwa na wote kwa nguvu zote na gharama zozote.”

Katika hatua nyingine, Rais Samia aliwashukuru Watanzania kwa kumpigia kura zilizompa ushindi na kuahidi kuwa, yeye, Makamu wa Rais pamoja na Wabunge na Madiwani waliochaguliwa watalitumikia Taifa la Tanzania kwa maarifa na nguvu zao zote ili kuleta maendeleo katika Taifa hilo.

“Nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuturuzuku uhai na kutuwezesha kushiriki sherehe hizi za kihistoria kwa Taifa letu, pili niwashukuru Watanzania wote kwa imani yao kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na kwa mapenzi makubwa na kutupa mimi na Makamu wa Rais fursa hii adhimu ya kuwatumikia,” alisema Rais Samia.

Aidha, Mhe. Dkt. Samia aliipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa kuratibu na kusimamia mchakato mzima wa uchaguzi kwa ufanisi usiotiliwa shaka.

Kadhalika, Rais Samia alikipongeza Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa namna walivyoendesha kampeni zao.

“Katika uchaguzi huu tulikuwa wagombea 17 kutoka Vyama mbalimbali nchini tukiwania nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kuwashukuru sana wagombea wenzangu 16 ambao kwa hakika wameonesha ukomavu wa kidemokrasia kwa kuendesha kampeni ambazo tulishindana kwa hoja na kuonesha kuwa siasa sio vita,” alisema Rais Samia.

Aliongeza kwa kuwasisitiza Watanzania kuendelea kudumisha umoja, upendo na mshikamano sambamba na kuheshimu sheria za nchi.

“Ndugu wananchi sifa moja ya mwanadamu ni kutokukamilika, aliyekamilika kabisa kabisa bila kasoro yoyote ni Mwenyezi Mungu peke yake, ndio maana katika shughuli au harakati za wanadamu tunaunganishwa na mawasiliano, mazungumzo na maelewano au kwa maneno mengine tunaungwanishwa na suluhu ya mambo katika jamii zetu,” alisisitiza Mhe. Dkt. Samia.

Alisema, Serikali ya awamu ya sita itaendelea na falsafa yake ya kuzingatia (four Rs’) ikiwemo maridhiano na kuwataka wananchi kuchagua upendo badala ya chuki, umoja badala ya mgawanyiko, huruma badala ya hasira, hekima badala ya kiburi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe.  Evariste Ndayishimiye amempongeza Rais Samia kwa ushindi alioupata, kumtakia heri sambamba na kuwasihi Watanzania kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano.

Kwa upande wake Rais wa Zambia akizungumza katika hafla ya Uapisho, Mhe. Hakainde Hichilema naye amempongeza Rais Samia kwa ushindi aliopata na kutoa rai kwa Watanzania kuendelea kudumisha na kuilinda amani waliyonayo kwa muda mrefu.

“Sisi sote tunatakiwa kufanya kazi bila kuchoka kulinda amani na usalama wa nchi zetu ili kuleta maendeleo, tuchague kufanya mazungumzo ya amani ili kushughulikia changamoto ya aina yoyote inayoikabili nchi,” alisisitiza Rais Hichilema.

Kadhalika, Mhe. Hichilema ameahidi kuwa, Zambia itaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanzania katika sekta mbalimbali ili kuendelea kukuza Uchumi wa nchi hizo mbili.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliibuka Mshindi wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata asilimia 97.66 katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika nchini tarehe 29 Oktoba, 2025.  



Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kushoto) akimuapisha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha pili cha Awamu ya Sita. Hafla ya Uapisho ya Rais na Makamu wa Rais wa Tanzania ilifanyika  tarehe 03 Novemba, 2025  katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akila kiapo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha pili cha Awamu ya Sita ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hafla ya uapisho ilifanyika tarehe 03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kushoto) akimuapisha Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa tayari kwa ajili ya kukagua Gwaride maalum mara baada ya kuapishwa kushika nafasi hiyo tarehe 03 Novemba, 2025 
katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.
Rais Samia akikagua gwaride maalum la Vikosi vya Jeshi la Ulinzi na Usalama lililoandaliwa maalum wakati wa hafla ya uapisho wa Rais wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais wa Tanzania tarehe 03 Novemba, 2025 
katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (wa kwanza mbele) akisindikizwa na sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Jaji Mkuu wa Zanzibar kuelekea kwenye jukwaa la Uapisho lililoandaliwa kwa ajili ya uapisho wa Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 03 Novemba, 2025
katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) pamoja na wageni mbalimbali wakiimba Wimbo wa Taifa la Tanzania wakati wa hafla ya uapisho wa Rais na Makamu wa Rais wa Tanzania tarehe 03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia Taifa mara baada ya kula kiapo cha kushika nafasi hiyo tarehe 03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Rais wa Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye akizungumza jambo wakati wa sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais wa Tanzania tarehe 
03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Rais wa Zambia, 
Mhe. Hakainde Hichilema
  akizungumza jambo wakati wa sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais wa Tanzania tarehe 03 Novemba, 2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.

Picha mbalimbali za matukio ya Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi tarehe 03 Novemba,    2025 katika Uwanja wa Chamwino Ikulu jijini Dodoma.                                         


JUDICIARY OF TANZANIA CHIEF REGISTRAR PARTICIPATES IN FRUITFUL MEETING WITH WIPO IN GENEVA

By UPENDO NGITIRI, Judiciary of Tanzania

In October 2025, a delegation from the Judiciary of Tanzania, led by Principal Judge of the High Court of Tanzania and Member of WIPO Advisory Board of Judges, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani, visited the World Intellectual Property Organization (WIPO) Headquarters in Geneva, Switzerland. During the visit, the delegation participated in the 2025 Annual WIPO Judges Forum. In addition, the Principal Judge attended the WIPO Advisory Board of Judges meeting, which took place after the Forum.

As part of this important visit, the Judiciary of Tanzania and WIPO also held   a series of meetings on 16 October 2025. The discussions focused on progress made under the Memorandum of Understanding (MoU) signed in 2021 and key areas of collaboration for implementation in 2026.

The meetings were attended by Ms. Altaye, Director of IP Learning and Internal Training Program; Ms. Ines Ferdinandez, Legal Officer, WIPO Judicial Institute; Victor Owade, Counsellor, WIPO Academy; Ms. Manuela Rotolo Araujo, Consultant, Distance Learning Program, Ms. Laura Para Gonzalez, Training Officer, Ms.  Carolina Tobar, Associate Programme Officer, and Ms. Isha Singh, Legal Case Manager – IP Disputes Section, WIPO Arbitration and Mediation Centres. On the   side of the Judiciary, the meetings were attended by Hon. Eva Nkya, Chief Registrar of the Judiciary of Tanzania and Upendo Ngitiri, Deputy Registrar and Focal Person for the Collaboration between the Judiciary of Tanzania and WIPO.

 

In her remarks, Hon. Eva Nkya expressed Judiciary of Tanzania appreciations to WIPO for its continued partnership and invaluable support. She commended the significant achievements realized through the collaboration, particularly in enhancing judicial capacity. The Achievement includes development of customized judicial training materials, participation of more than 1,450 Tanzanian judicial officers in judicial capacity-building programs such as Judicial Colloquiums, General Distance Learning Course for Judges, and the WIPO Annual Judges Forum, establishment of WIPO depository library in the Judiciary of Tanzania Library, publication of Tanzanian judicial decisions on WIPO Lex and adoption of WIPO’s online mediation tools. 

Productive Meetings were held with WIPO Judicial Institute, WIPO Academy and WIPO Arbitration and Mediation Centre. Discussions with the WIPO Judicial Institute included plans to organize the Judicial Colloquium for Tanzanian Judges and Magistrates. The Colloquium will provide a platform for dialogue, experience sharing, and engagement between Tanzanian judicial officers and international IP experts.  During the meeting it was also agreed to finalize the Bench Book on Intellectual Property, which will serve as a key reference and guide for judges and magistrates.

In tandem, WIPO commended the publication of Tanzanian IP decisions on the WIPO Lex–Judgments Database, as it enhances accessibility of national jurisprudence and promotes transparency. Another key activity deliberated is the WIPO Annual Judges Forum. The next Annual WIPO Intellectual Property Judges Forum is scheduled to take place on 13–14 October 2026.  The Forum will continue to serve as an important platform for Tanzanian judges to gain valuable insights and learn best practices from other jurisdictions.

Discussions with the WIPO Academy focused on judicial education. The Academy reaffirmed its commitment to continue providing scholarships for Tanzanian judges and magistrates to pursue the General Distance Learning Course on Intellectual Property. To date, 505 judges and magistrates have successfully completed the course.  Additionally, A special session on the Arbitration and Mediation Procedure under the WIPO Rules has been organized for the judiciary, with over 170 participants.

WIPO Academy also confirmed its support for the ongoing project to customize the General Distance Learning Course on Intellectual Property for the Tanzanian judiciary by aligning its content with the country’s legal framework, judicial practices, and emerging IP challenges.

The Academy further extended opportunities for Tanzanian judicial officers to apply for the Master’s Program in Intellectual Property, offered in partnership with 18 universities across 17 countries, including the University of Turin in Italy, Queensland University of Technology in Australia, Universidad de San Andrés in Argentina, Ankara University in Türkiye, Maqsut Narikbayev University in Kazakhstan, IE Foundation in Spain and Jagiellonian University in Poland, among others.   As of now eight Judicial Officers have benefited from WIPO Academy’s University Partnership programme.  The possibility of partnering with an accredited university in Tanzania under this program was also discussed.

An Executive Training Program, aimed at providing intensive, in-person training for judicial officers, was also proposed to be conducted in 2026. 

 Apart from that, Updates were shared on the establishment of the Intellectual Property Training Institute (IPTI) coordinated by the National IP Office.  The initiative supports member states in setting up self-sustaining IP training institution that address national priorities. Establishment of IPTI aims at strengthening national IP capacity. Under this programme, five Tanzanian judicial officers were nominated in 2024 as official trainers, and discussions were held on providing opportunities for additional judges to join.

Discussions with the WIPO Arbitration and Mediation Centre highlighted plans to strengthen the use of Alternative Dispute Resolution (ADR) mechanisms within the Judiciary of Tanzania. The WIPO Mediation Center will offer additional opportunities for Tanzanian judges and qualified judicial officers to apply for accreditation as WIPO Mediators.

Up to now, eight Tanzanian judges have received this accreditation. The Center also reaffirmed its commitment to supporting the judiciary through specialized capacity-building programmes designed to strengthen mediation and arbitration skills among judges and magistrates. Furthermore, the judiciary will continue to benefit from WIPO’s Online Mediation Tools, which support efficient, accessible, and technology-enabled dispute resolution processes.

The series of meetings concluded with a reaffirmation of the strong partnership and shared commitment to strengthening judicial capacity, with the goal of ensuring the effective delivery of justice, protecting intellectual property rights, fostering national economic growth, and safeguarding public health and societal wellbeing.


The third from left is Ms. Altaye, Director of IP Learning and Internal Training Program; the fourth from left  is Hon. Eva Nkya, Chief Registrar of the Judiciary of Tanzania , the  first from left  is Mr. Victor Owade, Counsellor, WIPO Academy, the second from left  is   Ms. Carolina Tobar, Associate Programme Officer, WIPO Academy , the first from right is  Ms. Manuela Rotolo Araujo, Consultant, Distance Learning Program,  the second from right is Ms. Laura Para Gonzalez, Training Officer; WIPO Academy  and the third  from left   is Upendo Ngitiri,  Deputy Registrar and Focal Person for the Collaboration between the Judiciary of Tanzania and WIPO.

 

The third from right is Hon. Eva Nkya, Chief Registrar of the Judiciary of Tanzania , the fourth   from left is Ms. Altaye, Director of IP Learning and Internal Training Program; the first from right is Ms. Ines Ferdinandez, Legal Officer, WIPO Judicial Institute; the second from right is Mr. Victor Owade, Counsellor, WIPO Academy; the first from right is Ms.  Manuela Rotolo Araujo, Consultant, Distance Learning Program and the second from left is Upendo Ngitiri, Deputy Registrar and Focal Person for the Collaboration between the Judiciary of Tanzania and WIPO.

Jumatano, 29 Oktoba 2025

JAJI MKUU MAHAKAMA YA TANZANIA ASHIRIKI ZOEZI LA UPIGAJI KURA UCHAGUZI MKUU 29 OKTOBA, 2025

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 29 Oktoba, 2025 ameungana na Watanzania wengine nchini kutimiza haki yake ya Kikatiba kwa kushiriki katika zoezi la upigaji kura wa Rais, Wabunge na Madiwani katika Kituo cha kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Mhe. Masaju aliwasili katika viwanja vya Kituo hicho majira ya Saa 2 Asubuhi na kupokelewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ambaye pia ni Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk.

Yafuatayo ni matukio katika picha, Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akishiriki katika zoezi la Upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akiwa katika zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akidumbukiza karatasi ya kupigia kura mara baada ya kushiriki katika zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akiendelea na zoezi la upigaji kura katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akipakwa wino maalum kama ishara ya kumaliza zoezi la upigaji kura leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma.

Wasimamizi wa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani katika Kituo cha Kupigia kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma wakimhudumia Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju katika hatua za awali alipowasili kushiriki katika zoezi la upigaji kura.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akipokelewa na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk alipowasili kupiga kura katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma leo tarehe 29 Oktoba, 2025.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kushoto) akifurahia jambo na na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk mara baada ya kukamilisha zoezi la upigaji kura katika Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma leo tarehe 29 Oktoba, 2025.

(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)


 

Jumanne, 28 Oktoba 2025

FEDHA ZA MATUMIZI ZIELEKEZWE KWENYE MABORESHO YA MIUNDOMBINU NA USIKILIZWAJI WA MASHAURI; JAJI RWIZILE

Na AIDAN ROBERT, Mahakama-Kigoma

Mwenendo wa matumizi ya fedha za kuendeshea shughuli za Mahakama imeelezwa kuwa, zitumike vema katika shughuli za Mahakama Kanda ya Kigoma kupitia vipaumbele muhimu vilivyowekwa katika Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania (2020/2021-2024/2025) kwenye Nguzo ya Pili ya Mpango huo inayosema ‘Upatikanaji na Utoaji Haki kwa wakati.’

Hayo yalibainishwa hivi karibuni kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Kigoma wakati wa Kikao cha Bajeti ya Kanda ya Kigoma kilichoongozwa na Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay.

Akitoa neno la ufunguzi wa kikao hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile alisema kuwa, “Viongozi na Maafisa Bajeti wa Mahakama zote muhakikishe usikilizwaji wa mashauri na vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) pamoja ukarabati wa Mahakama za mwanzo vinapewa kipaumbele zaidi katika bajeti zao ili kuendana na Mpango wa maboresho ya Mahakama na usikilizwaji wa mashauri sambamba na usimamizi wa haki za watumishi pamoja na kutunza samani za ofisi zilizopo.”

Bw. Matotay aliwasisitiza wajumbe wa Kamati ya Bajeti kuwa wabunifu katika kutekeleza bajeti zao zinazopatikana bila kutoka nje ya utaratibu sahihi uliowekwa katika matumizi ya fedha za Serikali ili kuhakikisha kazi za Mahakama yeyote hazikwami kwa namna yeyote ile.

Aidha, aliwasisitiza wajumbe wa kikao hicho kuhakikisha fedha za mirathi zilizopo katika akaunti ya Mahakama zinalipwa kwa wadaawa na kwamba imebainishwa kwamba zoezi la utambuzi wa fedha za mirathi unaendelea ili kumaliza kabisa fedha za mirathi zilizopo katika akaunti ya Mahakama Kanda ya Kigoma.

Kwa upande wake, Naibu Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa aliwapongeza Maafisa Bajeti wa Mahakama za Wilaya kwa taarifa nzuri za utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 kwani imegusa vipaumbele vya Mahakam,  imetekelezwa kwa ufanisi mkubwa kwa usikilizwaji wa mashauri na utatuzi wa changamoto kutumia rasilimali fedha  inayopatikana.

Mhe. Mbelwa alitumia fursa hiyo kuwasisitiza Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Wilaya zote ndani ya Mkoa huo kuendelea kusimamia vema bajeti zao ili zifanye shughuli muhimu za Mahakama kama Mpango Mkakati wa Mahakama huo unavyoelekeza.

Wajumbe wa kikao hicho walikuwa Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Wilaya, Wakuu wa Idara za Mahakama Kuu Kigoma na Maafisa Tawala kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mahakama za Wilaya Kigoma, Kibondo,  Uvinza, Kasulu, Buhigwe na  Kakonko.


Wajumbe Kikao cha Bajeti ya Kanda ya Kigoma kilichofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma wakifuatilia kwa makini maneno ya ufunguzi kutoka kwa  Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile akisisitiza jambo wakati akitoa neno la ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Bajeti Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma.

Mtendaji wa Mahakama Kuu  ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Kikao cha Kamati ya Bajeti ya Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma kilichofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la Mahakama Kuu Kigoma.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibondo, Mhe. Maira Makonya akichangia mjadala wa bajeti ya Mahakama ya Wilaya Kibondo wakati wa kikao cha 
Kamati ya Bajeti ya Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma kilichofanyika hivi karibuni.

Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Festo Sanga akifafanua jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Bajeti ya Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa mikutano -Mahakama Kuu Kigoma.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na 
wajumbe wa kikao cha Kamati ya Bajeti ya Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika hivi karibuni. Wa pili kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe.Fadhili Mbelwa, wa pili kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay, wa kwanza kushoto ni Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Eva Mushi na wa kwanza kulia ni Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Festo Sanga.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

VIONGOZI WA MAHAKAMA KIGOMA WAKUTANA KUTATHIMINI NA KUJIPANGA KUBORESHA UTENDAJI KAZI WA KANDA

  • Wajipanga kushughulikia na kudhibiti mashauri ya mlundikano

Na AIDAN ROBERT, Mahakama-Kigoma

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile ametoa rai kwa viongozi wa Mahakama za Wilaya zilizopo ndani ya Kanda hiyo kuongeza mikakati pamoja na ushirikiano katika uamuzi wa mashauri na kuzuia mashauri ya mlundikano sambamba na kuwa na usimamizi mzuri wa rasilimali fedha zinazoletwa  kwa ajili ya kuendeshea shughuli za Mahakama.

Mhe. Rwizile alitoa rai hiyo tarehe 25 Oktoba 2025 katika ukumbi wa mikutano Mahakama Kuu Kigoma kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi cha Tathmini ya shughuli za Mahakama kwa robo ya pili ya mwaka kilicholenga kuweka mikakati wa kutekeleza Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania wa mwaka 2025/2026 hususani nguzo ya pili ya Upatikanaji na Utoaji Haki kwa wakati. 

Jaji Mfawidhi huyo vilevile, alitoa pongezi kwa juhudi za kila mtumishi katika eneo lake kwa kuwa na ushirikiano akieleza kuwa, ushirikiano ndio unaleta matokea mazuri ya utendaji. Aidha, pongezi zingine alizitoa kwa Mahakama za Wilaya Buhigwe na Uvinza kwa uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti ya matunda na mbao na kuleta mandhari nzuri na hewa safi.

Aidha, aliongeza kusema, “tuongeze weledi wa kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao (virtual Court) ili kuhakikisha mashauri ya Ardhi, Benki na yale ya biashara yanasikilizwa na kumalizika mapema ipasavyo ikiwa ni sambamba na fedha za mirathi zilizopo katika akaunti ya mirathi zinalipwa kwa wanufaika kwa wakati.”

Pamoja na hayo, Mhe. Rwizile aliwaongoza Viongozi hao katika zoezi la upandaji miti Mahakama ya Wilaya Kigoma na kufanya mazoezi ya viungo ikiwa ni utamaduni wa Mahakama Kanda Kigoma ili kuimarisha afya za watumishi katika utendaji wa kila siku wa shughuli za Mahakama.

Kwa upande wake Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay alisema, umeandaliwa mpango maalum wa kusikiliza mashauri yanayokaribia kuingia katika mlundikano na kuendelea kusimamia vizuri rasilimali zilizopo ili zilete tija na kuhakikisha inafikiwa ili kuendeleza mpango wa kuongeza vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) hususani Kompyuta Mpakato.

Bw. Matotay alisema lengo la Kanda hiyo ni kuendeleza ushirikiano na wadau na kuimarisha maslahi ya watumishi na maadili ya kazi katika kuendeleza programu ya kupanda miti ya mbao na matunda katika maeneo ya majengo yote ya Mahakama Kanda ya Kigoma na kukamilisha programu ya Mahakama bila matumizi ya karatasi (Paperless Court).

Naye Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa alisema kuwa, Mahakimu Wakazi Wafawidhi waainishe maeneo ambayo watumishi na wadau wa Mahakama wanaweza kupewa mafunzo ya ndani katika kuboresha shughuli za Mahakama pamoja na Kwenda na  na kasi ya usikilizwaji wa mashauri mapema ipasavyo na kwa njia ya Mahakama Mtandao.

Hata hivyo, Mhe. Mbelwa aliwakumbusha Wafawidhi hao kuongeza usimamizi katika eneo la mashauri ili kuzuia mlundikano wa mashauri katika vituo vyao.

Wajumbe waliohudhuria kikao hicho walikuwa Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya mkoani Kigoma, Wakuu wa Idara za Mahakama Kuu Kigoma na Maafisa Tawala kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mahakama za Wilaya Kigoma, Kibondo,  Uvinza, Kasulu, Buhigwe na  Kakonko.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile akisisitiza jambo hivi karibuni wakati wa Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.

Wajumbe wa kikao wakifuatilia kwa makini taarifa ya utendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma wakati wa Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay akifafanua jambo kwa msisitizo wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo la Mahakama hiyo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile akipanda mti wa mchikichi katika eneo la wazi lililopo Mahakama ya Wilaya Kigoma mara baada ya kumaliza cha kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika  hivi karibuni kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. John Francis Nkwabi akipanda mti wa mchikichi katika eneo la wazi lililopo Mahakama ya Wilaya Kigoma mara baada ya kumaliza kikao  cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika  hivi karibuni kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa kikao  cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma. Wa pili kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. John Francis Nkwabi, (kulia) ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, wa pili kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma,  Mhe. Projestus Kahyoza, wa kwanza kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Fadhili  Mbelwa  na wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay na waliosimama ni wajumbe wengine wa kikao hicho.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

Jumatatu, 27 Oktoba 2025

JAJI MKUU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAANGALIZI WA UCHAGUZI MKUU 2025 KUTOKA 'EAC'

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 27 Oktoba, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Misheni ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections). Mazungumzo hayo yamefanyika kwenye ukumbi wa mikutano-Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Matukio katika picha ya mazungumzo kati ya Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju na Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections).


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akizungumza na Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) waliomtembelea Jaji Mkuu leo tarehe 27 Oktoba, 2025 Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akizungumza jambo na Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) waliomtembelea Jaji Mkuu leo tarehe 27 Oktoba, 2025 Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections), Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe akizungumza jambo wakati wa mazungumko katika ya Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (hayupo katika picha) na Waangalizi hao wa Uchaguzi Mkuu, 2025.


Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo wakati wa kikao cha mazungumzo kati ya Jaji Mkuu na ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) waliomtembelea Jaji Mkuu leo tarehe 27 Oktoba, 2025 ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) na Msajili Mkuu Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya wakifuatilia mazungumzo kati ya Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju na Ujumbe wa Waangalizi 
wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) leo tarehe 27 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na 
Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) leo tarehe 27 Oktoba, 2025 walipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Aliyeketi kushoto ni Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections), Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Viongozi wa Mahakama walioshiriki katika mazungumzo kati ya Jaji Mkuu na 
Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections) leo tarehe 27 Oktoba, 2025  Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Aliyeketi kushoto ni Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections), Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na 
Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections), Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe (kushoto). Aliyeketi kulia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Observers for 2025 General Elections), Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe (kushoto). Aliyeketi kulia ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya.

(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)