Na
INNOCENT KANSHA - Mahakama
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ameungana na Familia, Ndugu,
Jamaa, Marafiki na Waumini wa Kanisa la Anglikana kushiriki katika Ibada Maalum
ya kumuaga Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa
Mahakama ya Rufani Tanzania ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Ibada hiyo imefanyika katika
Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es Salaam leo tarehe 16 Mei, 2025.
Akitoa
Salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania, Jaji Mkuu Mhe.
Prof. Juma amemuelezea Marehemu Jaji Mandia kama mtu mwandilifu na mzalendo
aliyeitumikia jamii yake na ni miongoni mwa watu walioijenga Tanzania ya sasa
kwa nguvu kubwa.
“Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na fadhila kwa kutujalia siku ya leo ambayo
tumekusanyika hapa kusherehekea maisha na utumishi uliotukuka wa ndugu yetu, Jaji wa Rufani Mstaafu William Stephen Mandia ambaye ametutoka kimwili lakini
kiroho tunajua yuko upande upi wa maisha…
Kwa
niaba ya Mahakama ya Tanzania nawasilisha salamu za pole na faraja kwa watoto
wa Marehemu, Ndugu, Jamaa na wajukuu wote, majirani, marafiki na kwetu sisi
watumishi wa Mahakama ambao tuko kazini na wengine wastaafu walioko hapa. Aidha
tunamkubuka sana kwa utumishi uliotukuka,” amesema Jaji Mkuu.
Aidha,
Jaji Mkuu amesema Marehemu Jaji Mandia alifanya kazi yake kwa uaminifu mkubwa
kwa ueledi na alikuwa msaada mkubwa kwa watumishi wenzake. Mara nyingi
tunapozungumzia historia ya nchi huwa tunasahau kwamba historia ya nchi ni watu.
Kwa hiyo ukitaka kujua historia ya Tanzania unaweza kuchukua maisha ya Jaji William
Stephen Mandia na kaweza kujua historia ya Tanzania.
Vilevile,
Mhe. Prof. Juma amesema tangu Jaji Mandia alipozaliwa tarehe 06 Januari, 1949
imepita miaka mingi sana wakati huo ulikuwa ni wakati wa ukoloni na sina
uhakika kama alizaliwa hospitali, na sina uhakika hali ya afya ilikuwaje wakati
huo, lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu alimjalia maisha ambayo ni maisha yenye
manufaa makubwa sana kwa Taifa.
Jaji
Mkuu ameongeza kuwa, ukiangalia kwenda kwake shule hadi Chuo Kikuu inatokana na
historia ya nchi ya Tanzania, kwamba nchi ilipata uhuru bila ya kuwa na
watumishi wa kutosha wa sekta ya sheria, nchi ilipata uhuru bila kuwa na Majaji
na Mahakimu wazalendo.
Jaji
Mkuu amefafanua kwamba, wakati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipoamua
kuanzisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ukiangalia orodha ya wanafunzi wa
Chuo hicho, Jaji Mandia yupo kwenye kundi la 10 ambalo lilipata bahati ya kusoma
Chuo Kikuu na kazi ilikuwa moja tu lazima ikumbukwe wao ndiyo walipewa jukumu
la kujenga nchi mpya ambayo inafahamika kama Tanzania. Nchi ambayo ilikuwa
haina wataalam, haina watumishi wazalendo lakini hao watu ambao walikuwa na
uwezo wa kwenda kutafuta kazi nje ya nchi, waliweza kutulia wakakaa wakajenga
nchi ambayo ni Tanzania ya sasa.
“Na
ukiangalia Jarada lake ofisini huwezi kukuta sehemu ambayo ameomba kazi, siku
hizi tukiomba kazi tunaandika maneno mazuri mazuri lakini yeye alikuwa
anakabidhiwa kazi haombi na hayo ndiyo yalikuwa maisha ya watumishi wengi ambao
wamejenga nchi hii. Kwa hiyo tunakila sababu ya kushukuru maisha yake kwamba
yamesaidia kujenga nchi ambayo tunaifahamu na kuisaidia sana Mahakama ya
Tanzania…
Mimi
binafsi nilipojiunga na Mahakama ya Rufani 2012 nilimkuta Jaji Mandia tayari ni
Jaji wa Rufani na alikuwa amenitangulia kwa miaka minne, sasa kwa kawaida kila
unapokwenda sehemu kuna utamaduni wake hata katika nyumba hii Takatifu kuna
taratibu zake. Jaji Mandia ndiye aliyenipokea akanipa taratibu za Mahakama ya
Rufani ambazo huwezi kukuta zimeandikwa popote kwa hiyo unaweza kuona ni mtu wa
aina gani kwani siku zote alipenda kuwasaidia watu wengine,” amesema Jaji Mkuu.
Naye,
Mchugaji wa Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es
Salaam. Rev. Fr. Vinncent Kiondo akitoa mahuri wakati wa Ibada hiyo ametoa rai
wa waumini kumcha Mungu wakati wote kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuupokea
ufalme wa Mungu kwa hakuna ajua saa dakika wala siku kifo ni fumbo.
“Niwaombe
wanafamilia mzidi kumuombea Marehemu Jaji Mandi kwani ni mtu aliyekuwa mcha
mungu na shime niwatie moyo muendelee kushikamana kama familia na kumtegemea
mungu huku mkisherekea maisha ya mpendwa wetu aliyetangulia mbele za haki nasi
kwake siku moja tutarejea na tuzidi kumuomba Mungu hasa katika kipindi hiki cha
majonzi ya kupotelewa na mpendwa wao,” amesema Mchungaji Kiondo.
Mara
baada ya shughuli za Ibada kukamilika na kutoa heshimu za mwisho kwa kuaga mwili wa Marehemu Jaji Mandia, msafara wa waombolezaji ukaelekea kwenda kumpumzisha katika nyumba yake ya milele katika Makaburi ya kwa Kondo Ununio jijini Dar es salaam.
Itakumbukwa Marehemu Jaji Mandia alifikwa na umauti mnamo tarehe 13 Mei, 2025 katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Katika Ibada hiyo maalum ya kumuaga Marehemu Jaji Mandia iliyohudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mhimili wa Mahakama na Serikali wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu, Majaji Wastaafu pamoja na Wasajili, Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwaongoza Majaji wengine kutoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam katika Ibada Maalum ya kumuaga Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati Ibada ya kumuaga Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam katika Ibada Maalum ya kumuaga Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiweka shada la maua kwenye Kaburi la Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Wanafamilia wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania wakitoa heshima kwa mpendwa wao katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Mama Mzazi wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania wakitoa heshima kwa mpendwa mwanae katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam.
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwaongoza Majaji wengine kutoa heshima ya mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam katika Ibada Maalum ya kumuaga Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati Ibada ya kumuaga Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam katika Ibada Maalum ya kumuaga Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati Ibada ya kumuaga Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam katika Ibada Maalum ya kumuaga Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.