Na. Muksini Nakuvamba-Mahakama, Mbeya
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Said Kalunde ameongoza
kikao cha Menejimenti ya Kanda ya Mbeya inayojumuisha mikoa ya Mbeya na Songwe shughuli
hiyo ilichofanyika tarehe 09 Oktoba, 2025 Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya.
Akiwasilisha
taarifa ya utawala na ushughulikiaji wa mashauri kwa robo ya kwanza ya mwaka
2025/2026 kwa Mahakama za Mkoa wa Mbeya Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama Kuu
na Mahakama ya Wilaya Rungwe Bw. Alintula Ngalile alifafanua kuwa taarifa hiyo
inaainisha uwajibikaji, usimamizi wa rasilimali, utoaji na upatikanaji wa haki
kwa wakati.
Taarifa
hiyo pia, ilieleza maendeleo ya matumizi ya mifumo ya TEHAMA, hali ya majengo, viwanja
na miradi ya maendeleo inayoendelea katika mkoa wa Mbeya pamoja na ushirikishwaji
wa wadau katika utoaji wa elimu kwa umma na ushirikishwaji wa sekta binafsi
katika mnyororo wa utoaji haki.
Vilevile,
taarifa hiyo ilieleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho cha robo ya
kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026, changamoto pamoja na mikakati waliyojiwekea
katika kupambana na chanagamoto hizo.
Afisa
Utumishi huyo akatoa shukurani “Mhe. Mwenyekiti tunashukuru kwa uongozi wako
ambao unasisitiza katika uwajibikaji na utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia
uweledi, kanuni na taratibu katika utumishi wa Umma, ili kufanikisha haya yote
msisitizo mkubwa unawekwa kwa watumishi na viongozi kuwa waadilifu wakati wa
kutekeleza wajibu wao kiuweledi na kufanya kazi kwa umoja.”alisema Bw. Ngalile.
Aidha,
iliwasilishwa taarifa ya kiutendaji na usimamizi wa mashauri katika robo ya
kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 kwa Mahakama za Mkoa wa Songwe.
Akiwasilisha
taarifa hiyo Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Bw. Sostenes mayoka,
alifafanua hali ya rasilimali watu, usimamizi wa rasilimali fedha, hali ya
majengo, viwanja na miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Songwe, vyombo vya
usafiri hali ya mashauri na ziara za kutembelea Magereza Wilaya ya Mbozi na
Ileje.
Aidha,
taarifa hiyo pia ilieleza mafanikio, changamoto, mikakati waliyojiwekea katika
kupambana na chanagamoto hizo na mipango ya baadae
“Tuna
mipango kazi ya baadae ikiwemo kuanza zoezi la kupima maeneo yote ya viwanja
vinavyomilikiwa na Mahakama za Mkoa wa Songwe ili kupata hati. Pia tunalenga
kupunguza mlundikano wa mahabusu katika magereza yetu kwa kupunguza masharti ya
dhamana ili wale wanaodhaminika waweze kuwekewa dhamana.” alisema Bw. Mayoka.
Aidha,
taarifa za mirathi na malipo ya mirathi ilikuwa sehemu ya utekelezaji ikimtaka
kila Hakimu wa Mahakama za Wilaya na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Songwe
aliwasilisha taarifa za Mirathi kwenye wilaya yake.
Kwa
upande wa Mahakama za Mkoa wa Mbeya taarifa ya jumla kuhusu malipo ya mirathi
kwa Mahakama zote za Mkoa wa Mbeya iliyowasilishwa na Msaidizi wa Hesabu
Mahakama Kuu Mbeya Bw. Nassir Upete.
Mhe.
Kalunde akatoa shukurani kwa wajumbe wote kwa kushiriki na kusisitiza kuwa, viongozi
wawe na desturi ya kushirikisha watumishi wa chini katika kujadili mambo
mbalimbali ya kiofisi ili kuboresha utendaji kazi.
.JPG)
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde (Kulia) akiongoza
kikao cha Menejimenti Kanda ya Mbeya, Kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda
ya Mbeya Bi. Mavis Miti.
Sehemu ya wajumbe wa menejimenti kanda ya Mbeya
Afisa
Utumishi Mwandamizi (wa kwanza kushoto) akiwasilisha taarifa ya kiutendaji na
ushughulikiaji wa mashauri kwa robo ya kwanza ya mwaka 2025/2026 kwa Mahakama
za Mkoa wa Mbeya.
Msaidizi
wa Hesabu Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bw. Nassir Upete akiwasilisha taarifa ya
mirathi katika kikao hicho
Mtendaji
wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Bw.
Sostenes Mayoka (kulia) akiwasilisha taarifa ya utawala na uendeshaji wa
mashauri kwa robo ya kwanza ya mwaka 2025/2026 kwa Mahakama za Mkoa wa songwe.
Hakimu
Mkazi Mfawidhi mahakama ya wilaya Mbozi Mhe. Nemes Chami akiwasilisha taarifa
za Mirathi Mahakama ya Wilaya ya Mbozi -Songwe.