Ijumaa, 16 Mei 2025

MKURUGENZI 'ILO' AFRIKA MASHARIKI AAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA MAHAKAMA YA TANZANIA

  • Afurahishwa na ushiriki wa dhati na mijadala yenye tija ya Majaji Wafawidhi na Wadau wa haki madai

Na MARY GWERA, Mahakama-Arusha

Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Ukanda wa Afrika Mashariki, Bi. Caroline Mugala amekiri kufurahishwa na Ushirikiano uliopo kati ya Shirika la Kazi Duniani na Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Tanzania huku akionesha furaha yake kufuatia mafanikio yaliyopatikana katika Kikao cha Haki Kazi baina ya Shirika hilo na Majaji Wafawidhi na wadau wa haki kazi.


Bi. Mugala amebainisha hayo leo tarehe 16 Mei, 2025 alipokuwa akifunga kikao kazi cha siku mbili kilichohusisha Majaji Wafawidhi pamoja na Wadau wa haki kazi kilichofanyika katika Hoteli ya ‘Corrridor Springs’ jijini Arusha.

 

“Mafunzo haya ni hatua nyingine muhimu katika ushirikiano wa Shirika la Kazi Duniani na Mahakama ya Tanzania katika kuimarisha haki za kazi na kuendeleza kazi zenye staha kwa maadili ya uongozi hadi mageuzi ya kidijitali kutoka viwango vya kimataifa vya kazi hadi mijadala ya kijamii,” amesema Mkurugenzi huyo.

Bi. Mugala amesema kuwa, amefurahishwa hasa na wingi wa mitazamo na madhumuni madhubuti iliyowasilishwa na kujadiliwa  wakati wote wa kikao kazi hicho na kwamba ana imani elimu hiyo ya pamoja itaendelea kuunda Mahakama ya Kazi yenye ufanisi zaidi na yenye kuzingatia haki.

Ameongeza kwa kuahidi kuwa, Shirika la Kazi Duniani litaendelea kutoa ushirikiano kwa Mahakama ya Tanzania hususani Divisheni ya Kazi ili kuendelea kuboresha haki kazi.

Kadhalika, ametoa shukrani zake kwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani kwa kufungua kikao kazi hicho pamoja na uongozi wa Mahakama ya Kuu Divisheni ya Kazi chini ya Jaji Mfawidhi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina kwa kufanikisha uratibu wa kikao hicho.

Awali akizungumza wakati akitoa majumuisho ya Kikao Kazi hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina amelishukuru kwa dhati Shirika la Kazi Duniani (ILO) kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa Mahakama hiyo unaolenga kuboresha haki kazi.  


Mhe. Mlyambina amewakumbusha washiriki wa kikao kazi hicho kuwa ni  muhimu kuzingatia kaulimbiu ya kikao hicho isemayo; ‘Uboreshaji wa Uongozi kwa Ufanisi na Tija katika Utoaji wa Haki Kazi’.

Kadhalika, amewakumbusha pia yaliyosisitizwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani wakati wa ufunguzi wa kikao hicho ambapo alisisitiza juu ya kuhakikisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yanaimarishwa ili kuboresha huduma, kuongeza uwazi na uwajibikaji katika kushughulikia mashauri yote, yakiwemo yanayohusu migogoro ya kazi mahakamani.

Aidha, Mhe. Dkt. Mlyambina aliwadokeza washiriki wa kikao hicho kuhusu mada zilizowasilishwa na Wawezeshaji na kuzielezea kwa ufupi kila moja. Miongoni mwa mada zilizotolewa ni pamoja na Uongozi (Leadership); Motisha kwa watumishi na kujenga ujasiri (motivating employees and building confidence); Kanuni za Maadili za uongozi na Uadilifu (Leadership Code of ethics and Integrity); Utatuzi Mbadala wa Migogoro ADR, kupitia Upatanishi, na Usuluhishi (ADR, through Mediation, and Arbitration) na kadhalika.

Aidha, Majaji Wafawidhi pamoja na wadau wa haki kazi walioshiriki katika kikao hicho walipatiwa vyeti ikiwa ni ishara ya kushiriki ipasavyo katika kikao kazi hicho.

Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Ukanda wa Afrika Mashariki, Bi. Caroline Mugala (kulia) akifurahia zawadi anayopatiwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi wakati wa hafla ya kufunga kikao kazi cha haki kazi kilichoshirikisha Majaji Wafawidhi na Wadau kilichofanyika jijini Arusha tarehe 15 na 16 Mei, 2025.  



Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina akiwasilisha majumuisho ya kikao kazi cha Majaji Wafawidhi pamoja na wadau wa haki kazi leo tarehe 16 Mei, 2025 jijini Arusha.
   

Sehemu ya Washiriki wa kikao kazi hicho wakifuatilia kinachojiri katika hafla ya kufunga.

(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Arusha)








 

 

JAJI MKUU AUNGANA NA WAOMBOLEZAJI KATIKA SAFARI YA MWISHO YA KUMUAGA JAJI MANDIA

Na INNOCENT KANSHA - Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ameungana na Familia, Ndugu, Jamaa, Marafiki na Waumini wa Kanisa la Anglikana kushiriki katika Ibada Maalum ya kumuaga Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Ibada hiyo imefanyika katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es Salaam leo tarehe 16 Mei, 2025.

Akitoa Salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania, Jaji Mkuu Mhe. Prof. Juma amemuelezea Marehemu Jaji Mandia kama mtu mwandilifu na mzalendo aliyeitumikia jamii yake na ni miongoni mwa watu walioijenga Tanzania ya sasa kwa nguvu kubwa.

“Tunamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na fadhila kwa kutujalia siku ya leo ambayo tumekusanyika hapa kusherehekea maisha na utumishi uliotukuka wa ndugu yetu, Jaji wa Rufani Mstaafu William Stephen Mandia ambaye ametutoka kimwili lakini kiroho tunajua yuko upande upi wa maisha…

Kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania nawasilisha salamu za pole na faraja kwa watoto wa Marehemu, Ndugu, Jamaa na wajukuu wote, majirani, marafiki na kwetu sisi watumishi wa Mahakama ambao tuko kazini na wengine wastaafu walioko hapa. Aidha tunamkubuka sana kwa utumishi uliotukuka,” amesema Jaji Mkuu.   

Aidha, Jaji Mkuu amesema Marehemu Jaji Mandia alifanya kazi yake kwa uaminifu mkubwa kwa ueledi na alikuwa msaada mkubwa kwa watumishi wenzake. Mara nyingi tunapozungumzia historia ya nchi huwa tunasahau kwamba historia ya nchi ni watu. Kwa hiyo ukitaka kujua historia ya Tanzania unaweza kuchukua maisha ya Jaji William Stephen Mandia na kaweza kujua historia ya Tanzania.

Vilevile, Mhe. Prof. Juma amesema tangu Jaji Mandia alipozaliwa tarehe 06 Januari, 1949 imepita miaka mingi sana wakati huo ulikuwa ni wakati wa ukoloni na sina uhakika kama alizaliwa hospitali, na sina uhakika hali ya afya ilikuwaje wakati huo, lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu alimjalia maisha ambayo ni maisha yenye manufaa makubwa sana kwa Taifa.

Jaji Mkuu ameongeza kuwa, ukiangalia kwenda kwake shule hadi Chuo Kikuu inatokana na historia ya nchi ya Tanzania, kwamba nchi ilipata uhuru bila ya kuwa na watumishi wa kutosha wa sekta ya sheria, nchi ilipata uhuru bila kuwa na Majaji na Mahakimu wazalendo.

Jaji Mkuu amefafanua kwamba, wakati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipoamua kuanzisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ukiangalia orodha ya wanafunzi wa Chuo hicho, Jaji Mandia yupo kwenye kundi la 10 ambalo lilipata bahati ya kusoma Chuo Kikuu na kazi ilikuwa moja tu lazima ikumbukwe wao ndiyo walipewa jukumu la kujenga nchi mpya ambayo inafahamika kama Tanzania. Nchi ambayo ilikuwa haina wataalam, haina watumishi wazalendo lakini hao watu ambao walikuwa na uwezo wa kwenda kutafuta kazi nje ya nchi, waliweza kutulia wakakaa wakajenga nchi ambayo ni Tanzania ya sasa.

“Na ukiangalia Jarada lake ofisini huwezi kukuta sehemu ambayo ameomba kazi, siku hizi tukiomba kazi tunaandika maneno mazuri mazuri lakini yeye alikuwa anakabidhiwa kazi haombi na hayo ndiyo yalikuwa maisha ya watumishi wengi ambao wamejenga nchi hii. Kwa hiyo tunakila sababu ya kushukuru maisha yake kwamba yamesaidia kujenga nchi ambayo tunaifahamu na kuisaidia sana Mahakama ya Tanzania…

Mimi binafsi nilipojiunga na Mahakama ya Rufani 2012 nilimkuta Jaji Mandia tayari ni Jaji wa Rufani na alikuwa amenitangulia kwa miaka minne, sasa kwa kawaida kila unapokwenda sehemu kuna utamaduni wake hata katika nyumba hii Takatifu kuna taratibu zake. Jaji Mandia ndiye aliyenipokea akanipa taratibu za Mahakama ya Rufani ambazo huwezi kukuta zimeandikwa popote kwa hiyo unaweza kuona ni mtu wa aina gani kwani siku zote alipenda kuwasaidia watu wengine,” amesema Jaji Mkuu.

Naye, Mchugaji wa Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es Salaam. Rev. Fr. Vinncent Kiondo akitoa mahuri wakati wa Ibada hiyo ametoa rai wa waumini kumcha Mungu wakati wote kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuupokea ufalme wa Mungu kwa hakuna ajua saa dakika wala siku kifo ni fumbo.

“Niwaombe wanafamilia mzidi kumuombea Marehemu Jaji Mandi kwani ni mtu aliyekuwa mcha mungu na shime niwatie moyo muendelee kushikamana kama familia na kumtegemea mungu huku mkisherekea maisha ya mpendwa wetu aliyetangulia mbele za haki nasi kwake siku moja tutarejea na tuzidi kumuomba Mungu hasa katika kipindi hiki cha majonzi ya kupotelewa na mpendwa wao,” amesema Mchungaji Kiondo.

Mara baada ya shughuli za Ibada kukamilika na kutoa heshimu za mwisho kwa kuaga mwili wa Marehemu Jaji Mandia, msafara wa waombolezaji ukaelekea kwenda kumpumzisha katika nyumba yake ya milele katika Makaburi ya kwa Kondo Ununio jijini Dar es salaam.

Itakumbukwa Marehemu Jaji Mandia alifikwa na umauti mnamo tarehe 13 Mei, 2025 katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Katika Ibada hiyo maalum ya kumuaga Marehemu Jaji Mandia iliyohudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mhimili wa Mahakama na Serikali wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu, Majaji Wastaafu pamoja na Wasajili, Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwaongoza Majaji wengine kutoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam  katika Ibada Maalum ya kumuaga  Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati  Ibada ya kumuaga  Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam  katika Ibada Maalum ya kumuaga  Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiweka shada la maua kwenye Kaburi la Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.


Wanafamilia wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania wakitoa heshima kwa mpendwa wao katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam

Mama Mzazi wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania wakitoa heshima kwa mpendwa mwanae katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam.


Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 

Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 

Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 
Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 


Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania wakitoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam 
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwaongoza Majaji wengine kutoa heshima ya mwisho wakati  wa kuaga mwili wa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam  katika Ibada Maalum ya kumuaga  Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.




Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati  Ibada ya kumuaga  Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam  katika Ibada Maalum ya kumuaga  Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  akitoa salamu fupi za rambirambi kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania wakati  Ibada ya kumuaga  Marehemu Mhe. William Stephen Mandia aliyekuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania  katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga jijini Dar es salaam  katika Ibada Maalum ya kumuaga  Jaji huyo ambaye alifariki Dunia tarehe 13 Mei, 2025 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.