Jumatano, 8 Machi 2017

MAHAKAMA YA TANZANIA KUANZISHA KITUO KIMOJA CHA MIRATHI



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAHAKAMA 
                                                 TAARIFA KWA UMMA
Mahakama ya Tanzania kupitia Mpango Mkakati wake wa Miaka Mitano 2015/16 – 2019/20 imepanga kupanua wigo wa huduma kwa makundi yenye mahahitaji maalum. Katika Mpango huo Mahakama inatarajia kujenga Kituo cha Pamoja Kitakachoshughulikia masuala ya Mirathi. Katika Kituo hicho kutakuwa na huduma za Mahakama ya Mwanzo, Mahakama ya Wilaya na Mahakama Kuu.

Aidha Huduma za Kibenki pamoja na Huduma za Mafao kutoka Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Huduma za Msaada wa Kisheria, Usajili wa Vizazi na Vifo n.k zitapatikana katika kituo hicho ili kurahisisha huduma na kupunguza usumbufu kwa walengwa. 

Kituo hicho cha huduma hii kinatarajiwa kuanza kufanya kazi mwaka 2019 Mkoani Dar es salaam katika Wilaya ya Temeke karibu na Kituo cha Polisi Chang’ombe ilipo Mahakama ya Mwanzo Temeke.

Hii ni taarifa ya awali kwa umma kuhusu utekelezaji wa mpango huu.

IMETOLEWA NA
MSAJILI MKUU 
MAHAKAMA YA TANZANIA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni