Alhamisi, 2 Machi 2017

MAHAKAMA YAKUTANA NA WADAU KUJADILI UANZISHWAJI WA KITUO CHA KUSHUGHULIKIA MIRATHI


 Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu  uanzishaji   Kituo  kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin  Mugeta  akisalimiana  na  Ofisa  wa Mahakama   mara baada ya kuingia kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam  kwa ajili ya kuendesha mkutano huo. Anayefuatia ni   Mtendaji wa Mahakama za Mwanzo   Humphrey Paya Mkutano huo umefanyika tarehe  Machi 02,  mwaka 2017.
Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu uanzishaji  wa  Kituo   kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin  Mugeta (kushoto)  akizungumza  jambo  na  Jaji wa Mahakama  Kuu Kanda ya Mbeya,Mhe. Atuganile Ngwala(kulia)  wakati  wa  akiendesha  majadiliano  ya mkutano huo  uliofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umefanyika tarehe  Machi 02,  mwaka 2017.
Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu uanzishaji  wa  Kituo   kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin  Mugeta (kushoto)  akizungumza  jambo  na  Jaji wa Mahakama  Kuu Kanda ya Mbeya,Mhe. Atuganile Ngwala(kulia)  wakati  wa  akiendesha  majadiliano  ya mkutano huo  uliofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umefanyika tarehe  Machi 02,  mwaka 2017. 
 Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu uanzishaji   wa  Kituo cha  kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin  Mugeta (kushoto)  akiendesha  mkutano huo. Ngwala  wakati  wa  akiendesha  majadiliano  ya mkutano huo  uliofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam. Kulia ni  Jaji wa Mahakama  Kuu Kanda ya Mbeya,Mhe. Atuganile. Mkutano huo umefanyika tarehe  Machi 02,  mwaka 2017.


Meneja  wa  Usimamizi Mafao,  Amin  Laban(katikati) kutoka  katika Mfuko wa  Hifadhi ya Jamii (PSPF) akichangia hoja  wakati  wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu  Kituo cha  kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi   Mkutano huo  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam  Machi 02,  mwaka 2017.
Picha ya Pamoja  ya wadau wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu uanzishaji  wa   Kituo cha  kimoja cha kushughulikia masuala ya mirathi uliofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umefanyika tarehe  Machi 02,  mwaka 2017.


Na Magreth Kinabo – Mahakama ya Tanzania.
MAHAKAMA ya Tanzania, ina mpango wa kuanzisha  Kituo  maalum   kitakachoshughulikia  masuala ya mirathi ili kuweza kusogeza   huduma za masuala ya mirathi  kwa wananchi, ikiwa ni hatua ya kuwapunguzia gharama za fedha  wanazozitumia na muda wanaoutumia.
Kutokana  na  eneo la mirathi limeonekana  kuwa na changamoto nyingi na hivyo kuhitaji mtazamo wa pekee Mahakama  inaanzisha,  Mpango huo ili kuongeza  ufanisi na  katika kushughulikia  mirathi na mambo ya kifamilia.,
Aidha  hatua  hiyo, itasaidia  kuwawezesha   makundi maalum ambayo  wanawake na watoto wakiwemo na wasimamizi wa mirathi  wanaohitaji  huduma hiyo kuendelea  kushiriki katika shughuli za maendeleo na kukuza uchumi wa nchi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu  uanzishaji   Kituo  Maalum  cha  kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin  Mugeta kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam.
“Tuna  mapango wa kuanzisha  kituo hicho cha  huduma  za Mahakama   kuhusiana  na masuala  ya mirathi, ambacho  kitakuwa na wadau  mbalimbali wa Mahakama  ya Tanzania ili  kuhakikisha  huduma za mirathi  zinatolewa kwa wakati  bila kupoteza muda  na gharama,” alisema Mwenyekiti huyo.
Aliongeza kwamba kituo hicho kitaanzishwa   katika jiji la Dar es Salaam, ikiwa ni mradi wa mfano, lakini  baadae  vitaanzishwa katika mikoa mingine.
 Aidha   Mhe. Mugeta   ambaye pia alikuwa mgeni rasmi  katika mkutano huo, alisema kituo hicho, kitaanzishwa  katika jiji hilo kwa  sababu  tatizo hilo, kubwa kwa sababu   lina wakazi wengi.
Aliitaja  sababu  ya kuanzishwa kituo hicho, kimetokana  kwamba Mahakama ya Tanzania huwa inapokea maoni 3,000 kila siku  kuhusiana na masuala hayo.
“Kituo hicho kitakuwa na huduma za Mahakama za Mwanzo, Wilaya na Mahakama Kuu, ili kuweza kuondoa vipingamizi  katika utoaji wa huduma hizo.
Alisema  katika kituo hicho,  kinatarajiwa  kuwa  na  huduma za  utoaji wa vyeti vya kuzaliwa na cheti kifo,  huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii  na kibenki.
Baadhi ya wadau  wa mkutano huo, walipendekeza kwamba elimu zaidi  itolewe kuhusiana na masuala ya mirathi.
Mkutano huo, ambao umeandaliwa na Mahakama ya Tanzania, umewashirikisha  baadhi ya viongozi wa Mahakama  na wadau mbalimbali  ambao ni  Chama  cha Wanasheria Wanawake  Tanzania, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, ambayo ni (NSSF), (PSPF),  Mamlaka  ya Usimamia  Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Chama  cha Mawakili Tanganyika(TLS) na Baraza Kuu la Waislaamu Tanzania(BAKWATA).
 
 
 

 

 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni