Jumatano, 6 Desemba 2017

WIKI YA MSAADA KISHERIA YAENDELEA VIWANJA VYA MNAZIMMOJA

Mzee  Dawood   Athuman  akionyesha  baadhi ya vilelezo vyake kwa ajili ya kupata  msaada wa kisheria  kutoka   Mwanasheria  Anna Henga  wa Kituo  cha Haki za Binadamu(LHRC) wakati  wa Wiki  ya Msaada wa Kisheria inayondelea  kwenye Viwanja Mnazi Mmoja jijini Dar es Saalam. Wiki  hiyo imeanza rasmi kuanzia  Desemba  4, mwaka  huu na inatarajia  kumalizika Desemba  8, mwaka  huu.


     Baadhi ya Wasaidizi wa kisheria  wakichambua  vielelezo mbalimbali  katika  Wiki ya Msaada wa  Kisheria  inayoendelea  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

 Mwakili  wa kujitegemea  Job  Kerario (kulia ) akitoa  msaada wa kisheria  kwa Mama  Riziki   Shah ambaye anataka msaada  wa kisheria  baada ya kufika kwenye Wiki ya  Msaada  wa Kisheria inayoendelea  kwenye  Viwanja  vya Mnazi  Mmoja , jijini Dar es Salaam  baada ya kukosa  Matunzo kwa Mumewe.

    Baadhi  ya wananchi wakipata  Msaada wa Kisheria kwenye Viwanja Mnazi Mmoja jijini Dar es Saalam.  Msaada  huo  wa kisheria  hutolewa  bure  katika Wiki  ya Msaada  wa Kisheria  iliyoanza rasmi kuanzia  Desemba 4, mwaka  huu na inatarajia  kumalizika Desemba  8, mwaka  huu.

Na Magreth Kinabo – Mahakama
Kituo cha Msaada wa Kisheria  kijulikanacho  kwa jina  la Paralegal kimewashauri wananchi wenye nia ya kununua viwanja kufika katika Manispaa husika  ili kuweza kuepukana na  tatizo la migogoro  ya Ardhi  na kuepusha upotevu wa rasilimali  fedha  wanazozitumia.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 6, Desemba  2017 na  Katibu  wa kituo hicho,   Antony  Isakwi katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam ambapo Maonesho ya Wiki ya  Msaada  wa Kisheria yanaendelea. 

“Wananchi  wanapaswa kuelewa kwamba  wanatakiwa kununua ardhi     baada  ya  kupata  maelekezo  sahihi  kutoka katika  Manispaa husika  badala  ya kununua  ardhi  kiholela, kwa kuwa  kwa kufanya  hivyo itasaidia  kuepusha  kupoteza fedha kwa  kununua  ardhi  kwenye maeneo  yasiyo  sahihi,”alisema  Isakwi.

Wiki hiyo ya kisheria   iliyoanza rasmi Desemba 4, na inatarajiwa  kumalizika Desemba 8, mwaka  huu, ambapo Katibu  huyo alisema  bado kuna umuhimu mkubwa wa kuwaelimisha wananchi ili kuweza kuepukana na tatizo hilo, pamoja na matatizo mengine kama vile ukatili wa kijinsia, mirathi na matunzo kwa  watoto.

Alisema kituo  chake kimeweza kuwapokea  wananchi zaidi ya 50  waliokuwa  wakihitaji  msaada wa kisheria tangu walipoanza huduma  hiyo, ambayo wanaitoa  bure kwenye viwanja hivyo. Aidha kituo hicho pia kimeshawapatia wananchi wanaohitaji  huduma ya kisheria wapatao 360,000  katika kipindi  cha mwaka   mwaka  huu. Aliongeza kuwa idadi kubwa ya watu walijitokeza  katika  kituo hicho ni  wale wenye matatizo ya migogoro ya ardhi, kijinsia, mirathi na matatizo ya matunzo kwa watoto.

Kwa  upande wake  Msaidizi wa kisheria  Athuman  Maghembe  aliviasa vyombo  vya habari nchini  kutumia nafasi hiyo kwa kuelimisha watanzania umuhimu  wa wiki  hiyo ili waweze kuepukana na matatizo hayo.
                                                             

    Baadhi  ya wananchi wakipata  Msaada wa Kisheria kwenye Viwanja Mnazi Mmoja jijini Dar es Saalam.  Msaada  huo  wa kisheria  hutolewa  bure  katika Wiki  ya Msaada  wa Kisheria  iliyoanza rasmi kuanzia  Desemba 4, mwaka  huu na inatarajia  kumalizika Desemba  8, mwaka  huu.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni