Alhamisi, 7 Desemba 2017

NAIBU JAJI MKUU WA NAMIBIA ATEMBELEA MAHAKAMA YA TANZANIA


Jaji Kiongozi Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali (kulia) akimuonyesha Naibu Jaji Mkuu wa Namibia (katikati anayetazama juu),  Mhe. Petrus Damaseb moja ya Kumbi za Mahakama Kuu, Naibu huyo Jaji Mkuu pamoja na ujumbe alioambatana nao wametembelea Mahakama ya Tanzania kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa uendeshaji wa Mahakama hususani Suala la utoaji haki ambalo ndio jukumu kuu la Mahakama. Aidha Naibu Jaji Mkuu huyo atatembelea pia Mahakama Kuu-Divisheni ya Biashara mapema Desemba 08.

Jaji Kiongozi-Mahakama Kuu ya Tanzania (kushoto) akimuonyesha, Naibu Jaji Mkuu wa Namibia Mhe. Petrus Damaseb Maktaba ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

Picha ya pamoja: Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali (katikati) pamoja na Naibu Jaji Mkuu wa Namibia (wa nne kushoto) wakiwa katika picha mara baada ya kumaliza maongezi. 

Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Mradi wa Maboresho ya Mahakama (JDU) Mhe. Zahra Maruma, akiwasilisha Mada mbele ya Naibu Jaji Mkuu wa Namibia na Ujumbe alioambatana nao, Mhe. Maruma aliwasilisha mada ya jinsi Mahakama inavyotekeleza Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (5) (2015/2016-2019/2020), ikiwa ni pamoja na mafanikio na changamoto.

Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akichangia mada, kushoto ni Naibu Jaji Mkuu wa Namibia Mhe. Petrus Damaseb akimsikiliza kwa makini Mhe. Jaji Kiongozi.

Naibu Jaji Mkuu wa Namibia, Mhe. Petrus Damaseb akichangia: Mhe. Damaseb ametoa uzoefu wa Mahakama- Namibia hususani katika Suala la hukumu zinazotolewa na Wahe. Majaji ambapo amesema kuwa pindi Jaji husika anapomaliza kesi hutakiwa kuwasilisha ‘summary’ ya hukumu aliyoitoa ili iweze kuwekwa katika tovuti kwa ajili ya kuwezesha Wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mawakili kupata elimu/rejea.

Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revokati akichangia jambo katika kikao hicho, Mhe. Revokati aliuomba Ujumbe huo kutoka Namibia kutoa uzoefu wao katika masuala mbalimbali hususani ni jinsi gani wanafanya katika utoaji wa ‘Law Reports’ na masuala mengineyo, kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu,  Mhe. Amir R. Mruma.

Baadhi ya Wajumbe wakifuatilia na kusikiliza kwa umakini mada iliyokuwa ikitolewa, wa kwanza kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Amir Mruma, (wa pili kushoto) ni Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga, wa kwanza kushoto ni Msajili-Mahakama ya Rufani (T), Mhe. John Kahyoza, wa tatu ni Mtendaji-Mahakama ya Rufani (T)- Mhe. Sollanus Nyimbi na wa pili kulia ni Msajili Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revokati na wa tatu kulia ni Mhe. Ndunguru, Katibu wa Mhe. Jaji Kiongozi. 
(Picha na Mary Gwera)






 
 
 
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni