Ijumaa, 16 Machi 2018

WATENDAJI, NAIBU WASAJILI NA MAHAKIMU WAJADILI NAMNA YA KUMALIZA MASHAURI YA MLUNDIKANO

  Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akiwa kwenye Mkutano wa Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini unaojadili namna ya kumaliza mashauri ya Mlundikano leo jijini Arusha. Jaji Kiongozi alifungua rasmi Mkutano huo.  

 Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini wakiwa kwenye Mkutano wao unaojadili namna ya kumaliza mashauri ya Mlundikano leo jijini Arusha.
 Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Bwn. Leonard Magacha akiwa kwenye Mkutano unaojadili namna ya kamaliza Mashauri ya Mlundikano Mahakamani uliowakutanisha Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini jijini Arusha.
  Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bwn. Hussein Kattanga akifuatilia jambo kwenye Mkutano unaojadili namna ya kamaliza Mashauri ya Mlundikano Mahakamani uliowakutanisha Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini jijini Arusha.
  Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mashauri wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya akitoa Mada kwenye Mkutano wa Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini unaojadili namna ya kamaliza Mashauri ya Mlundikano Mahakamani.
 Mtaalamu wa Tehama Bwn. Alfred Mwita akiwasilisha Mada kuhusu Kanzidata (Database) ya Mashauri  kwenye Mkutano wa Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini unaojadili namna ya kamaliza Mashauri ya Mlundikano Mahakamani.
 Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini wakiwa kwenye Mkutano huo. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa  Utawala wa Mahakama ya Tanzania Bibi Wanyenda Kutta.

  Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akifafanua jambo kwenye Mkutano huo. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bwn. Hussein Kattanga.


 Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi Mhe. Charles Magesa akifafanua jambo wakati wa majadiliano ya vikundi ya namna ya kumaliza mashauri ya Mlundikano.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Pwani Mhe. Elizabeth Nyembele (katikati) akizungumza wakati wa madiliano ya vikundi ya namna ya kumaliza mashauri ya Mlundikano.
 Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi Mhe. Joachim Tiganga akiwasilisha Mada kwenye Mkutano huo.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bwn. Hussein Kattanga akifafanua jambo kwenye Mkutano unaojadili namna ya kamaliza Mashauri ya Mlundikano Mahakamani uliowakutanisha Watendaji, Naibu Wasajili na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi nchini jijini Arusha. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni