Jumatano, 21 Machi 2018

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA KUU MKOANI MARA



Na Sheiba Bulu, Wizara ya Katiba na Sheria
Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi ametembelea Mradi wa Ujenzi wa Mahakama Kuu mkoani Mara na kujionea ujenzi huo unavyoendelea .

Akizungumza baada ya kupata taarifa fupi kuhusu ujenzi wa Mahakama hiyo mapema Machi 20, 2018, Prof. Kabudi amewataka Wasimamizi wa Mradi huo kuutangaza kwani uwepo wa  Mahakama Kuu Mkoani Mara utaleta ahueni kubwa kwa wananchi wa mkoa huo ambao walikuwa wanalazimika kwenda Mwanza kutafuta haki zao.

Mhe. Waziri amesema Mahakama hiyo itakapokamilika wananchi wa mkoa wa Mara watapata haki zao kwa wakati ndani ya mkoa wao bila ya kulazimika kwenda umbali mrefu kutafuta haki.

Ujenzi wa Mahakama Kuu mkoani Mara unatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama wa 2015/2016-2019/2020 ambao unatoa kipaumbele kwa ujenzi wa miuundombinu ya Mahakama nchini ili kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi.
 Waziri wa Katiba wa Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, akisaini kitabu cha Wageni pindi alipowasili eneo la Mradi wa Ujenzi wa Mahakama Kuu lililopo Bweri Manispaa ya Musoma.

 Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma, Bi. Zilliper Geke akisoma taarifa ya maendeleo ya Mradi mbele ya Mhe. Waziri Prof. Palamagamba Kabudi.
 Mhe. Waziri akielekea kukagua jengo la Mahakama Kuu-Kanda ya Musoma linaloendelea kujengwa na Kampuni ya Ujenzi ya ‘DF-MISTRY COMPANY LTD’

Mafundi wakiendelea na kazi

Mhe. Waziri akiwa na Makarandasi wanaojenga jengo hilo pindi alipokuwa anakagua.
 Ukaguzi ukiendelea.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni