Ijumaa, 30 Novemba 2018

JAJI KIONGOZI AONGOZA HAFLA YA KUWAAGA KITAALUMA MAJAJI WASTAAFU WATATU WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA


Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi (wa kwanza kushoto) pamoja na baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu-Dar es Salaam wakiwa katika hafla ya kuwaaga Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, kulia ni mmoja wa Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu, Mhe. Regina Rweyemamu, Majaji wengine waliostaafu kwa mujibu wa Sheria ni Mhe. Jaji Frederick Werema na Mhe. Jaji Ibrahim Mipawa.

Pichani ni Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu-Divisheni ya Biashara, Mhe. Jaji Frederick Werema akiwa katika hafla ya kuagwa kwao Kitaaluma katika Ukumbi namba moja (1) wa Mahakama Kuu ya Tanzania-Dar es Salaam mapema Novemba 30, 2018. Wahe. Majaji Wastaafu kwa ujumla wao wameishukuru Mahakama kwa kushirikiana nao vyema katika kipindi cha utumishi wao na vilevile kuwaasa Watumishi wa Mahakama waliopo kazini kujiepusha na Vitendo vya Rushwa.

Baadhi ya Wageni waalikwa na Watumishi wa Mahakama wakiwa katika hafla ya kuagwa rasmi Kitaaluma Majaji watatu Wastaafu wa Mahakama Kuu.

Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akisoma Wasifu wa Wahe. Majaji Wastaafu katika hafla hiyo.

Mtendaji wa Mahakama Kuu, Bw. Leonard Magacha (mwenye suti nyeusi) pamoja na Watendaji wengine wa Mahakama na baadhi ya Watumishi wa Mahakama wakiwa katika hafla hiyo.


Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi (katikati), baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu na sehemu  ya Watumishi wa Mahakama wakiwa katika picha ya pamoja na Wahe. Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu, wa tatu kushoto ni Jaji Mstaafu, Mhe. Jaji Frederick Werema, wa tatu kulia  ni Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Mhe. Jaji Regina Rweyemamu, wa pili kulia ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi, Mhe. Jaji Aisha Nyerere, wa kwanza kulia ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Jaji Beatrice Mutungi na wa kwanza kushoto ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Biashara, Mhe.Jaji Barke Sehel.
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Biashara, Mhe.Jaji Barke Sehel (kushoto) akimpatia shada la maua Jaji Msataafu, Mhe. Frederick Werema aliyesimama na Mhe. Werema ni mkewe.

Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi (kushoto)akimpongeza Jaji Mstaafu, Mhe. Jaji Regina Rweyemamu kwa shada la maua, kulia ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi, Mhe. Jaji Aisha Nyerere.


Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi (kushoto) akimpongeza Jaji Mstaafu, Mhe. Ibrahim Mipawa (kushoto), kulia ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi, Mhe. Jaji Aisha Nyerere.

Picha ya pamoja na ndugu wa Mhe.Jaji Mstaafu, Mhe. Regina Rweyemamu

(Picha na Mary Gwera, Mahakama)
 
 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni