Ijumaa, 30 Novemba 2018

JAJI MKUU AZUNGUMZA NA WAJUMBE WA ARINSA



 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim  Juma akiwa catlike picha ya pamoja na wageni hao kutoka Taasisi ya  Urejeshaji wa Mali zilizotoroshwa na Utakatishaji  Fedha ARINSA.Watatu kutoka kushoto ni Mkurugenzi  wa Mashtaka Nchini (DPP) ,Biswalo Mganga.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim  Juma  akimkabidhi  nakala ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania,  Fitz Roy Drayton  ambaye  ni  Mshauri wa  Taasisi ya  Urejeshaji wa Mali zilizotoroshwa na Utakatishaji  Fedha ARINSA.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim  Juma  akizungumza na wageni  kutoka Taasisi ya  Urejeshaji wa Mali zilizotoroshwa na Utakatishaji  Fedha ARINSA.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim  Juma  akizungumza na wageni  kutoka Taasisi ya  Urejeshaji wa Mali zilizotoroshwa na Utakatishaji  Fedha ARINSA.

   Na mwandishi wetu
    
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe, Profesa  Ibrahim Juma  amesema Mahakama ya Tanzania iko tayari kushiki na Taasisi ya Urudishaji wa Mali zilizotoroshwa na Utakatishaji wa Fedha (ARINSA).
 Akizungumza na ujumbe wa watu watano kutoka nchi mbalimbali, ukiongozwa na Mshauri,Fitz -Roy  Drayton Jaji Mkuu alisema  Mahakama iko tayari kushiriki na taasisi hiyo  katika mafunzo ili kupata uzoefu kutoka nje katika  maeneo hayo.
Aidha Jaji Mkuu aliwashukuru wageni hao kwa kazi kubwa wanazozifanya katika nchi hizo, kwani ni muhimu  kwa sasa  kukuza uchumi ambao  keki  ya mataifa haya iwe  kwa manufaa ya watu wote na sio kwa wajanja wachache.
Hivyo utekelezaji  wa sheria  hizi ni muhimu    kwa maendeleo  ya wananchi wenyewe.
Jaji Mkuu alimwelezea Msajili wa Mahakama ya Rufani (RCA), Mhe. John Kahyoza kuangalia  namna bora katika  kalenda  ya Mahakama ili ARINSA iweze kutoa mafunzo kwa majaji na mahakimu.
Awali  akizungumzia kuhusu ujio wa wageni hao, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini(DPP) Biswalo Mganga alisema  kazi yao kubwa  kushirikisha nchi za Kusini mwa Afrika katika kuhusu sheria za kila nchi katika kurudisha mali zilitoroshwa, kuchukua au kufilisi fedha zilizotakaswa.
Naye Mshauri wa ARINSA, Fitz -Roy  Drayton alisema   kazi nyingine  watatoa  taarifa ripoti za sheria  kuonyesha mataifa yanayofanyakazi katika eneo hilo.  





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni