Ijumaa, 14 Desemba 2018

JAJI MSTAAFU WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA STEPHEN ERNEST IHEMA AFARIKI DUNIA

                                              TANZIA

                                   

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Stephen Ernest Ihema kilichotokea tarehe 11/12/2018 katika hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es salaam.


Msiba uko nyumbani kwa marehemu MbweniJKT/Ndege Beach na Mazishi yatafanyika kesho Jumamosi Tarehe 15/12/2018 saa 10 jioni katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.

Marehemu Jaji Mstaafu Ihema alizaliwa mwaka1943 mkoani Shinyanga. Aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania kama Hakimu tarehe 6 May, 1969.

Aidha, Marehemu Ihema aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Tume ya Kurekebisha Sheria (The Law Reform Commission of Tanzania) ambapo alifanya kazi mpaka alipostaafu kwa mujibu wa sharia tarehe 30 Juni, 1998.

Aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania tarehe 3 Machi mwaka 1999. Aidha, tarehe    1 mwezi Julai mwaka 2003 alistaafu rasmi wadhifa wa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Mwezi Julai 18, mwaka 2005, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alimteua Marehemu Jaji Ihema kuwa Kamishna wa Secretariet ya Maadili ya Viongozi wa Umma wadhifa ambao alikaa nao mpaka mwaka 2010. 

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi.

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni