Jumatano, 15 Januari 2020

JAJI MFAWIDHI MAHAKAMA KUU KANDA YA TANGA AFANYA ZIARA

(Na Amina  Ahmad - Mahakama Kuu Tanga)

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Tanga Mhe. Amir R. Mruma, akisaini amefanya ziara ya kikazi kanda hiyo, wiki iliyopita  ambapo amefanya ukaguzi Mahakama za Mwanzo Ngomeni na Mtindiro zilizopo Wilayani Muheza, Mahakama za Mwanzo Duga na Maramba zilizopo Wilayani Mkinga, Viwanja na Majengo ya Mahakama, Ofisi za Wakuu wa wilaya ya Muheza na Mkinga.


Pia  alitembelea Mahakama za Mwanzo Ngomeni na Mtindiro zilizopo Wilayani Muheza, Mahakama za Mwanzo Duga na Maramba zilizopo Wilayani Mkinga, Viwanja na Majengo ya Mahakama, Ofisi za Wakuu wa wilaya ya Muheza na Mkinga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Mhe. Amir R. Mruma akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilindi. Pembeni yake (kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe. Sauda Salim Mtondoo.



Afisa Ardhi wa Wilaya ya Mkinga, Bwana Obedi Katonge(kushoto) akimuonesha Jaji Mfawidhi Mhe. Amir R. Mruma (Aliyeshika nyaraka), mipaka ya kiwanja cha Mahakama ya Wilaya ya Mkinga. Kulia  ni Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Muheza, Mhe. Yusuph Zahoro, akifuatiwa na Afisa Tawala wa Mahakama ya Wilaya ya Muheza, Bw. Muharami Pazzi.
Jengo lililopatikana kwa ajili ya kuanza kutoa huduma za Mahakama ya Wilaya ya Mkinga.
Jengo lililopatikana kwa ajili ya kuanza kutoa huduma za Mahakama ya Wilaya ya Mkinga.

(Picha na Amina  Ahmad - Mahakama Kuu Tanga)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni