Jumatano, 22 Januari 2020

TCRA YAIUNGA MKONO MAHAKAMA KWA MATUMIZI YA TEHAMA


 Na  Magreth  Kinabo- Mahakama

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo imekabidhi   vifaa vya  mbalimbali  vya kisasa  vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano  (TEHAMA)  kwa ajili  kuiunga mkono  Mahakama ya Tanzania  kutokana na juhudi zake za matumizi ya   teknolojia hiyo.

Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria  wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), Bw. Johannes  Karungura  alikabidhi vifaa hivyo, kwa  Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,  Mhe. Eliezer Feleshi  kwa niaba ya  Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kwenye hafla fupi iliyofanyika mahakamani hapo, jiji Dar es Salaam, ambapo  aliipongeza Mahakama kwa juhudi  inazozifanya katika  matumizi ya  teknolojia hiyo.

‘Tumetoa vifaa hivyo ili kuendeleza gurudumu la matumizi  ya TEHAMA,’ alisema Karungura.

Kwa  upande  wake Jaji Kiongozi , alisema  anaishukuru mamlaka hiyo kwa niaba ya Jaji Mkuu  na Mahakama ya Tanzania, kwa kuwa vifaa hivyo, vitasaidia Mahakama hiyo  kuendelea  kutekeleza majukumu yake kwa wakati.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni kompyuta 15, kompyuta mpakato 20,  mashine 5, mashine ya uchapaji 15 na  mashine za kudurufu tano na vitambaza vitano.

Hii ni mara ya pili kwa TCRA kutoa msaada huo, kwa  Mahakama hiyo, ambapo mara ya kwanza ilitoa kompyuta 30.



 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi  (katikati) akizungumza  jambo wakati makabidhiano ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano  (TEHAMA)  kwa ajili kusaidia kuendeleza  teknolojia  hiyo  katika  utendaji kazi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.Hafla  hiyo imefanyika  leo mahakamani hapo, jijini Dar es Salaam.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe.  Dkt. Eliezer Feleshi  (katikati) akizungumza na  baadhi ya viongozi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  (waliokaa upande wa kushoto)  jambo wakati makabidhiano ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano  (TEHAMA)  vya  kisasa  kwa ajili kusaidia kuendeleza  teknolojia  hiyo  katika  utendaji kazi wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Hafla  hiyo imefanyika  leo mahakamani hapo, jijini Dar es Salaam. Kulia ni baadhi ya viongozi ya Mahakama ya Tanzania.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi (wa tatu kushoto) akipokea  moja  kompyuta mpakato, ikiwa miongoni mwa vifaa viliyokabidhiwa kutoka  Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Johannes  Karungura (wa  nne kulia), ambaye alikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TCRA.

Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria  wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Johannes  Karungura (wa pili kushoto) akizungumza jambo na  Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,  Mhe. Dkt.  Eliezer Feleshi (kushoto).

Baadhi ya vifaa hivyo.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni