Alhamisi, 18 Machi 2021

MAHAKAMA KUANDAA WARAKA WA KUISAIDIA TUME

Na Innocent kansha – Mahakama.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ahaidi kutoa waraka kwa Maafisa wote wa Mahakama ya Tanzania kutoa taarifa za wazi zitakazosaidia   kurahisisha shughuli za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini kushughulikia masuala baina ya Tume na Mahakama.

Akizungumza na ujumbe wa tume hiyo iliyomtembelea ofisini kwake Jijini Dar es salaam Machi 17, 20201 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Juma alisema, nawakikishia kutao ushirikiano kwa masuala yahusuyo Mahakama katika kushughulikia kero za wananchi.

“Tuishukuru serikali kwa kutambua changamoto za Mahakama na kwa kiasi kikubwa zimefanyiwa kazi, maboresho haya makubwa yaliyofanyika ni kutokana na mpango mkakati wetu wa miaka mitano 2015/16 hadi 2020/2021 umesaidia kuainisha sehemu zenye changamoto kubwa zaidi na kuzifanyia kazi”, aliongeza Jaji Mkuu.

Aidha, Prof. Juma alieleza kuwa amepokea ombi la tume lakutaka kupewa mafunzo na elimu kuhusiana na mabadiliko na maboresho makubwa yanayoendelea mahakamani ili iweze kuwasaidia Tume kuwashauri wateja wao ipasavyo.

Jaji Mkuu aliongeza kuwa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika shughuli za utoaji haki imeonyesha mafanikio makubwa hususani kipindi cha mwaka wa jana 2020 wakati wa ugojwa wa Corona Mahakama iliweza kusikiliza kesi nyingi za jinai kushinda wakati wowote wa usikilizwaji wa mashauri hayo. 

“Ndoto yangu nikuona tunatumia teknolojia ya TEHAMA ili mahakama zetu zitumimike kutoa taarifa zote muhimu zinazohusu mashauri na huduma zitolewazo kumsaidia mwananchi anaefika kupata huduma mahakamani bila kubabaika kwani mfumo huu ni huru na wawazi zaidi”, alisisitiza Jaji Mkuu.

 Alikadhalika, Jaji Mkuu aliueleza ujumbe wa tume kuwa, Mahakama inautaratibu wake wa kujitathimini kupitia taasisi binafsi kama REPOA kila baada ya miaka mitano ili kutathini utendaji kazi na kiwango cha kuridhishwa watumiaji wa huduma za Mahakama.

Jaji Mkuu pia, aliwapongeza Mwenyekiti wa Tume na Makamishina wote kwa kuteuliwa kwao kushika nyadhifa hizo.

Naye, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu ameipongeza Mahakama kwa jitihada zake za kuimarisha mfumo wa utoaji haki nchini matharani kuongeza idadi ya majengo ya mahakama kwa ngazi zote za kimahakama, matumizi ya TEHAMA katika utoaji haki,Uandaaji wa miongozo mbalimbali inayotumika katika uendeshaji wa mashauri mahakamani, matumizi ya Mahakama inayotembea ili kuwahudumia wananchi kwa kusogeza huduma karibu zaidi pamoja na utoaji wa elimu kwa umma juu ya shughuli za Mahakama kupitia vyombo vya habari.

Pia, Mwenyekiti wa Tume Mhe. Mwaimu aliipongeza serikali kwakuongeza idadi ya rasilimali watu mahakamani kama vile Majaji, Mahakimu na watumishi wa kada zingine hii ni kutokana na ushauri wa busara wa Tume ya Utumishi wa Mahakama.

Aidha, Mwenyekiti aliipongeza Mahakama kwa hatua zinazoendelea za ujenzi wa makao makuu ya Mahakama Jijini Dodoma ili kuhamishia shughuli zake rasmi.

Kwa upande mwingine, Mwenyekiti huyo aliishukuru Mahakama kwa kushirikiana na Tume katika kuisaidia serikali kuwahudumia wananchi wake mathalani utoaji wa nakala za hukumu na mienendo ya mashauri bure, kuweka mipango mathubuti ya kutocheleweshwa kwa mashauri mahakamani na malipo ya mafao kwa watumishi wa Mahakama.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (aliyenyoosha mkono) akifanya mazungumzo na ujumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ulipomtembelea Ofisini kwake Jijini Dar es salaam, pamoja na mambo mengine Tume hiyo ilifika kujitambulisha ikiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Msataafu Mhe. Mathew Mwaimu.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Msataafu Mhe. Mathew Mwaimu (kushoto) mara baada ya kumtembelea ofisini kwake, kulia ni Kamishna wa Tume hiyo Mohamed Khamis.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi.Amina Ali (kushoto) mara baada ya kumtembelea ofisini kwake, kulia ni Kamishna wa Tume hiyo Bi. Dkt. Fatma Khalfan.

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni