Jumamosi, 5 Juni 2021

JAJI MASSATI AFUNGA RASMI MAFUNZO YA MAJAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI.

 Na Innocent Kansha – Mahakama Lushoto.

Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Salum Massati amefunga rasmi mafunzo elekezi ya wiki moja kwa Majaji saba wa Mahakama ya Rufani na kuwataka wakatumie ujuzi na maarifa waliojengewa na wakufunzi wakayatumie kufanya kazi kwa weledi na uadilifu watakapokuwa wanatekeleza majukumu yao mapya.

Akizungunza wakati wa kufunga mafunzo elekezi hayo katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto mnamo Juni 4, 2021 Jaji Massati alisema, wengi wenu mmepitia changamoto nyingi na mafanikio, mkajenga historia zenu za nyuma kiutendaji kwa mafanikio hicho ndicho kimekuwa kigezo cha kuteuliwa kwenu kwenda Mahakama ya Rufani.

“Rudini mkatumie ujuzi huu kule mtakapokwenda kufanya kazi zenu za kila siku, mnatakiwa kutumia muda wenu kurejea hadidu za rejea ili ziwajengee uwezo wa kutoa maamuzi ya busara mara zote mtakapotekeleza majukumu yenu”, alisema Jaji Massati.

Aidha, aliongeza kuwa siku tano walizokaa darasani Majaji hao zinatosha kwa kupata muelekeo wa kutekeleza majukumu yenu mapya kwani mambo mazuri hujitokeza mwishoni naamini mmepikwa na kuiva vizuri kulingana na ratiba yenu na pia madhumuni ya mafunzo hayo elekezi mmeyahitimisha kwa ufasaha.

Jaji Mstaafu Massati alisema uwepo wenu kwenye mafunzo elekezi hayo sio tu umewajengea udugu mtakao kuwa nao kwa muda mrefu muwapo kazini bali yamewajengea hekima na busara mtakayo itumia wakati wote mtakapokuwa mkifanya maamuzi kwa mustakabali wa ustawi wa Taifa.

Naye, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Patricia Fikirini alisema mafunzo haya elekezi ni muhimu sana yametuelekeza mambo mengi na muhimu sana yametuvusha daraja muhimu kutoka ngazi ya Mahakama Kuu na kutupeleka Mahakama ya Rufani.

“Wengi wetu tulipoona uteuzi tulijiuliza maswali mengi sana na hata tulipokutana na Jaji Mkuu wa Tanzania kwa mara ya kwanza baada ya uteuzi hatukujua tunakwenda kujadili mambo gani, sasa tumetambua kupitia mafunzo haya elekezi yametuvusha vema kutoka kujua majukumu ya Mahakama Kuu na kutambua majukumu mapya ya Mahakama ya Rufani”,

Jaji Fikirini amewaomba waandaaji wa mafunzo hayo kuyafanya kuwa endelevu hata kama sio hapo Chuoni yaendelee kutolewa ili kuendelea kuwajengeza uwezo zaidi kuimarisha uwezo wao zaidi kiutendaji, na wasisite kutoa ushirikianao pale watapowahitaji kufanya hivyo.

Wakati huo huo, Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama ya Lushoto yalipokuwa yakiendeshwa mafunzo elekezi hayo Mhe. Dkt. Paul Faustine Kihwelo alisema anawashukuru Majaji kwa kuonyesha utulivu, mshikamano, kuchangia majadiliano na kujitoa kwao muda wote wa mafunzo.

“Kama mkufunzi unapofundisha watu ukaona wamekaa kimya utajiuliza mengi, kama je? watu hao wamekuelewa au hawajakuelewa kwenu Mhe. Majaji ilikuwa tofauti kabisa mafuzo yamekuwa ya ushirikishwaji wa hali ya juu na hoja zote mmechangia kwa kiwango cha juu nawapongeza sana”, aliongeza Mhe. Dkt. Kihwelo.

Jaji Dkt. Kihwelo aliwataka radhi kwa mapungufu yaliyojitokeza hasa katika kipindi chote cha siku tano kwa mapungufu yaliyojitokeza na kuwafanya kutokuwa watulivu muda wote wa mafunzo elekezi hayo.

Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Salum Massati akizungumza na Majaji wa Mahakama ya Rufani (hawapo pichani) wakati alipofunga rasmi mafunzo elekezi ya siku tano ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto mnamo Juni 4,2021

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Patricia Fikirini akitoa nasaa zake wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku tano ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Patricia Fikirini akitoa nasaa zake wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku tano ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania

Baadhi ya Jaji wa Mahakama ya rufani wakifurahia jambo wakati wa kufunga mafunzo elekezi ya siku tano Chuoni Lushoto 

Jaji wa Mahakama Rufani ya Tanzania na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama - Lushoto akipokea Cheti wakati wa kufunga Mafunzo elekezi ya Majaji wa Mahakama ya Rufani yaliyoendeshwa kwa siku tano mnamo Juni 4, 2021 kwa mgeni rasmi Jaji Mstaafu wa Mahakam ya Rufani Jaji Salum Massati


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lucia Kairo akipokea cheti kama ishara ya kuhitimu mafunzo ya siku tano yaliyofanyika Chuo cha Uongozi wa Mahakama wa Mahakama Lushoto. 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Mhe. Dkt. Paul Kihwelo akitoa nasaa zake wakati wa kufunga mafunzo elekezi hayo.

Picha na Ibrahim Mdachi na Innocent Kansha 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni