Alhamisi, 3 Juni 2021

MAHAKIMU KANDA YA MUSOMA WANOLEWA KWA KAZI

Na Francisca Swai, Musoma

Mahakimu Wakazi Kanda ya Musoma wanolewa kikamilifu katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mhe. Jaji. Mfawidhi wa Kanda ya Musoma Mhe. Jaji, John Kahyoza ambapo, Mahakimu hao walikumbushwa kuzingatia maadili ya kazi pamoja na taratibu mbalimbali katika usikilizaji wa Mashauri mbalimbali.

Katika kikao kazi hicho kilichofanyika hivi karibuni, Mahakimu hao walipewa jukumu la kuandaa na kuwasilisha mada tofauti tofauti na kisha kufanyika majadiliano ya pamoja.

Mada zilizowasilishwa ni pamoja na Tabia na mwenendo wa Maadili kwa Maafisa wa Mahakama, Hatua muhimu za kuzingatia katika uendeshaji wa Mashahuri ya Jinai tangu kufunguliwa hadi kufikia hukumu, Ufunguaji wa kesi katika Mahakama za Mwanzo.

Nyingine ni hatua za utekelezaji wa hukumu katika Mahakama za Mwanzo, Jinsi ya kushughulikia mapingamizi katika mashauri ya mirathi Mahakama za Mwanzo na Uendeshaji wa Mashauri ya Jinai katika Mahakama za Mwanzo.

Washiriki wa kikao kazi hicho walimpongeza Mhe. Jaji. Kahyoza kwa kuandaa kikao hicho kwani kimesaidia kuwakumbusha mambo muhimu ya kuzingatia katika utendaji kazi wa kila siku na pia kimekuwa msaada kwa Mahakimu ambao ndio wameanza kazi.

Picha ya pamoja ya washiriki wote wa kikao kazi cha Waheshimiwa Mahakimu Mahakama Kanda ya Musoma.  Waliokaa katikati ni Mhe, Jaji. John  Kahyoza, Jaji Mfawidhi Mahakama Kanda ya Musoma, kulia kwake ni Mhe, Jaji. Ephery Sedekia Kisanya, Jaji wa Mahakama Kuu Musoma. Kushoto kwake ni Naibu Msajili Mhe. Mary  Moyo na kushoto kwake ni Mhe. Tumaini Marwa, Kaimu Hakimu Mkazi Mahakama ya Mkoa, na mwisho kushoto ni Bw. Festo Chonya, Mtendaji wa Mahakama Kuu Musoma.

Mhe. Jaji. JohnKahyoza akielezea jambo katika kikao kazi hicho.

 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni