Na Waandishi Wetu-Dodoma
Mahakama ya Tanzania inao
mpango wa kutumia Mahema kusikiliza mashauri na kuongeza idadi ya Mahakama
zinazotembea (Mobile Court) ili kuongeza ufanisi na kasi ya kusikiliza mashauri
mahakamani.
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe
11 Januari, 2022 na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel wakati akizungumza na
Viongozi wa Mahakama wakiwemo Watendaji, Wasajili na Maafisa Bajeti kutoka kanda
na mikoa yote nchini kwenye mkutano wa kutathimini utekelezaji wa bajeti.
Alisema Mahakama ya
Tanzania inatarajia kuongeza magari sita ya Mahakama zinazotembea (Mobile
Courts) na kuyasambaza maeneo mengine mbali na mikoa ya Dar es salaam na Mwanza
ambapo huduma hiyo inapatikana hivi sasa, lengo ni kusogeza huduma za Mahakama
karibu zaidi na wananchi.
Prof. Ole Gabriel alisema
sanjari na hilo, Mahakama inatarajia kuanzisha huduma ya kimashauri kupitia
ujenzi wa Mahema katika maeneo ambayo yana msongamano na hakuna huduma za kimahakama.
Alisema lengo ni kuhakikisha wananchi wengi wanapata huduma ya kusikilizwa kwa
mashauri katika mazingira ambayo yako karibu na wanapoishi.
Kwa
upande wake, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Chuma amewataka
Mahakimu kutumia njia na namna bora ya kuondoa mrundikano wa mashauri ya muda
mrefu ili Mahakama isiwe sehemu ya ucheleweshaji wa utoaji wa haki kwa
wananchi.
Alisema kumalizika kwa mashauri
mapema mahakamani kutasaidia kuongeza imani ya wananchi kwa Mhimili wa
Mahakama. Aidha, Msajili Mkuu aliwataka Viongozi hao kuongeza kasi kwenye matumizi
ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kupunguza mrundikano wa
mashauri mahakamani.
Mhe. Chuma aliwataka viongozi hao kuongeza matumizi ya mikutano Mtandao (video conference) katika kusikiliza mashauri, jambo litakalowawezesha Majaji na Mahakimu kusikiliza idadi kubwa ya mashauri kwa muda mfupi.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa rai kwa Watendaji, Naibu Wasajili na
Maafisa Bajeti kutoka Mahakama za mikoa mbalimbali hapa nchini walipokuwa
katika kikao cha kupitia bajeti leo mjini Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati waliokaa), Msajili Mkuu wa
Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Chuma(
kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Mahakama wa
Kanda na mikoa baada ya kufunguliwa mkutano wa Naibu Wasajili wa Kanda, Watendaji na Maafisa Bajeti kutoka Mahakama za mwao.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati waliokaa) na Msajili Mkuu wa
Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Chuma (
kushoto waliokaa) akiwa kaika picha ya pamoja na Naibu Wasajili kutoka kwenye Kanda mbalimbai nchini .
Msajili Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania Mhe. Wilbert Chuma akitoa rai kwa Watendaji, Wasajili na Maafisa Bajeti
kutoka Mahakama za mikoa mbalimbali hapa nchini walipokuwa katika kikao cha
kupitia bajeti leo mjini Dodoma.
Kazi nzuri, hongera mtendajimkuu wa mahakama professor Elisante Ole Gabriel
JibuFuta