Ijumaa, 4 Februari 2022

JAJI MDEMU ATOA SOMO KWA WAJUMBE TUME WALIOAPISHWA

 Na Tiganya Vincent – Mahakama, Dodoma

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu amewataka wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji kuhakikisha wanaisoma na kuielewa sheria inayosimamia majukumu ya chombo hicho.

Mhe. Mdemu ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Februari, 2022, Jijini Dodoma mara baada ya kuwaapisha wajumbe wa Tume hiyo.

Alisema watumishi wa Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji ni vema wakapewa elimu kuhusu sheria na taratibu ili utekelezaji wa majukumu ya Tume hiyo yafanyike vizuri na kuepeka kwenda nje kutafuta suluhu.

“Elimu hii ya majukumu ya Tume ishiishie kwa viongozi na wakuu wa vyombo ambavyo viko ndani ya Tume , bali iende kwa watumishi ambao wanawajibika kwenye Tume, kwani wao ndio wanaojua taratibu za nidhamu wanazotakiwa kuzingatia ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu,”alisisitiza.

Mwenyekiti wa Tume hiyo ambaye ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni (Mb) amemwakikishia Jaji Mfawidhi huyo kuwa wajumbe watahakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu na weledi wa juu kwa ajili ya maendeleo ya vyombo vinavyosimamiwa Tume na Taifa kwa ujumla.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni (Mb) akila kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari, 2022 . Anayemwapisha ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu.    

1.    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni (Mb) akisaini  kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari , 2022. 

1  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe Jumanne Sagini (Mb) akila kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari , 2022. 

  Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga  akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari , 2022. 

1.     Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga  akipokea hati za kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari , 2022. 

1. Kamishna wa Polisi(CP) Awadhi Juma Haji akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari , 2022. 

Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza Mbaraka Semwanza akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji tarehe 3 Febuari, 2022. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni