Na Magreth Kinabo -Mahakama
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Amir Mruma ametoa maoni kuwa ni wakati wa muafaka kwa mihimili ya Bunge na Serikali kuangalia upya baadhi ya sheria zifanyiwe marekebisho ili mtuhumiwa aweze kukamatwa upelelezi ukishakamilika kwa kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa mlundikano wa mahabusu katika magereza.
Akizungumza leo
Februari 2, mwaka 2122 katika kilele cha Siku ya Sheria Nchini kwa Kanda ya
Dare s Salaam, kilichofanyika kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu Mhe. Mruma, ambaye ni mgeni rasmi alisema kuna baadhi ya washtakiwa
wanaletwa mahakamani ili upelelezi ukamilike wakiwa mahakamani.
‘‘Hii si haki na ni kucheza na haki za watu. Ukiondoa
mashauri machache mfano yale ya mauaji ambayo hata usalama wa mtuhumiwa unaweza
kuwa hatarini, na yale yanayohatarisha usalama wa nchi,’alisema Jaji Mruma huku
akihoji kwamba kuna haraka gani kumkamata mtuhumiwa na kumfungulia kesi kabla
ya upelelezi kukamilisha upepelezi dhidi yake? Je, kama baada ya upelelezi
kukamilika na akaonekana hana hatia nani atamfidia?
Alisema kama
wadau wote watafanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo hakutokuwepo
na mlundikano wa mahabusu katika magereza na hakutakuwa na mashauri yaliyokaa
muda mrefu.
Jaji Mruma aliongeza kwamba sasa Mahakama inatoa
nakala za bure ndani ya siku 21 na mwenendo wa shauri unatakiwa kupatikana
ndani ya siku 30. Hivyo katika kipindi cha Januari hadi Desemba, mwaka 2021 kanda hiyo imeweza kutoa nakala za
hukumu zipatazo 3,615.
Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
imewezesha maisha kuwa mepesi zaidi kwani kwa sasa wanapata takwimu sahihi na
kwa wakati sahihi, ambapo awali walikuwa wanategemea karatasi na kutuma posta.
Alifafanua kuwa kwamujibu wa taarifa kutoka Masjala
Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2021 mashauri
yaliyofunguliwa ni 1,594, yaliyomalizika ni 2,356 na yanayoendelea ni 2,896.
Aidha kwa upande wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya mashauri yaliyofunguliwa
kipindi hicho ni 1,1790, yaliyomalizika 5,594 na yanayoendelea ni 2,997.
Alisema taarifa ya Mahakama za Mwanzo zinasema mashauri yaliyofunguliwa ni 11,790, yaliyomalizika ni 12,813 na yanayoendelea ni 2,997.
‘‘Nachukua fursa hii kuwapongeza Mahakimu wa Mahakama
za Mwanzo kwani hawana mlundikano wa mashauri na wamemaliza mashauri yao zaidi
ya asilimia 100,’’alisisitiza.
Aliitaja changamoto uliyopo katika Mahakama Kuu ni ni
kuwepo kwa mashauri yenye umri mrefu kutokana na uchache wa majaji, kwa kuwa
mahakama hiyo ina majaji saba. Hivyo mashauri yaliyopo hayaendani na idadi ya majaji
waliopo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe.Amos
Makala ambaye alikuwa mgeni maalum alisema aliipongeza Mahakama kwa hatua
iliyofikia ya Mahakama Mtandao kile kisingizio faili limepotea hakuna. Hivyo
changamoto iliyopo kwa wananchi ni kuwepo kwa elimu ndogo ya sheria, ambapo alisema
ataendelea kushirikiana na mahakama kutoa elimu hiyo kwa kuwa ni jambo la
muhimu.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria (TLS) mkoa wa Dar es Salaam Mzizima, Bw.James Marenga alisema chombo hicho kina kazi ya kutatua migogoro bila malipo ili kupunguza migogoro inayoletwa mahakamani.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Amir Mruma akijiandaa kugakugua gwaride ikiwa ni ishara za kuanza shughuli za mahakama na kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini, kilichofanyika kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Amir Mruma akitoa hotuba yake katika maadhimisho hayo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe.Amos Makala ambaye alikuwa mgeni maalum katika maadhimisho hayo, akizungumza jambo.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria (TLS) mkoa wa Dar es Salaam Mzizima, Bw.James Marenga akizungumza jambo.
Baadhi ya wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na watumishi wa Mahakama ya Tanzania wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.
kupunguza migogoro inayoletwa mahakamani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni