Na Mohamed Kimungu-Mahakama, Songwe.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim amewahimiza
watumishi wote kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu, nidhamu, weledi na
ushirikiano wanapotekelea majukumu yao ya utoaji haki kwa wananchi.
Mhe.
Ebrahim alitoa wito huo jana tarehe 30 Machi, 2022 baada ya kuhitimisha ziara
yake ya kikazi ya siku mbili aliyoifanya kuanzia tarehe 29 Machi, 2022 ambapo alitembelea Mahakama ya Wilaya Ileje na Mahakama ya Wilaya
Momba Mkoa wa Songwe na kuzungumza na watumishi.
Jaji
Mfawidhi huyo ameupongeza Mkoa huo kwa kutokuwa na malalamiko katika utendaji
wa kazi na katika matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Amewashauri watumishi wa kada zingine kujifunza TEHEMA kwa kuwa ndio uelekeo wa
Mahakama kwa sasa kama inavyosisitizwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof
Ibrahim Hamisi Juma.
Katika
ziara hiyo, Mhe. Ebrahim alitembelea pia mradi wa wa ujenzi Mahakama ya Hakimu
Mkazi Songwe na kumuelekeza mkandarasi kumaliza mradi huo ifikapo tarehe 31 Mei,
2022 kama ilivyopangwa.
Aidha,
Jaji Mfawidhi huyo amemtembelea Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Mhe Ana Gidarya na
kupongeza uongozi wake kwa umoja na ushirikiano unaotoa kwa Mahakama katika Wilaya
hiyo. Kadhalika, Mhe. Ebrahim alitembelea Gereza la Wilaya ya Mbozi ambapo ameahidi
kufanyia kazi changamoto kadhaa alizoziona.
Vile
vile, Jaji Mfawidhi huyo amewapongeza Waendesha Mashtaka na Ofisi ya Upelelezi katika Mkoa wa Songwe kwa
kazi nzuri wanayofanya, hususani katika kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani.
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim (wa pili kulia) akipokea maelezo kutoka
kwa mtendaji wa Mahakama, Bw. Sostenes Mayoka (wa pili kushoto) alipotembelea mradi wa ujenzi wa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim (wa pili kulia) akitambulishwa kwa
watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Momba na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe.
Timothy lyon Hakimu (wa tatu kulia).
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim (wa pili kulia mstari wa mbele) akitambulishwa kwa
watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Ileje na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo,
Mhe. Desdery Magezi (wa tatu kulia mstari wa mbele).
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim (katikati) akiwa katika picha
ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ileje. Mhe Ana Gidarya (wa tatu kulia) na watumishi wengine).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni