Jumatatu, 11 Aprili 2022

WATUMISHI MAHAKAMA KUU KANDA YA MOSHI WAPATIWA MAFUNZO YA OFISI MTANDAO

 Na. Paul Paschal-Mahakama, Moshi.

Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi wa kada mbalimbali wanaohudhuria mafunzo ya Ofisi Mtandao wamehimizwa kwenda na mabadiliko ya kisasa yanayoendelea ndani ya Mahakama ya Tanzania.

Akifungua mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoanza leo tarehe 11 April 2022, Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu wa Kanda hiyo, Bw Paul Mushi amesema Mahakama ya sasa ni ya kisasa, hivyo amewaomba watumishi hao kuhakikisha nao wanakuwa wa kisasa kwa kujifunza kwa bidiii kadiri wanapopata fursa hizo.

 “Sote ni mashahidi, Mahakama inaboreka kwa kasi na tumshukuru Mungu tumepata watendaji wenye spidi ya hali ya juu, hivyo ni jukumu letu pia kuunga mkono juhudi za uboreshaji kuelekea Mahakama mtandao,” Bw. Mushi amesema

Mafunzo hayo yamejumuisha watumishi 29 wakiwemo Mahakimu, Wasaidizi wa Kumbukumbu ,Wakaguzi wa Hesabu za Ndani, Maafisa Utumishi na Utawala na Wahasibu kutoka Wilaya zote sita za Mkoa wa Kilimanjaro.

Mwezeshaji, ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka Mahakama Kuu, Arusha, Bi. Angel Meela akiendesha mafunzo kwa watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi wa kada mbalimbali (hawapo katika picha) kuhusu Ofisi Mtandao.
Sehemu ya watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi wa kada mbalimbali (picha ya juu na chini) wakifuatilia mafunzo kuhusu Ofisi Mtandao yaliyokuwa yakitolewa na mwezeshaji, Afisa TEHAMA kutoka Mahakama Kuu, Arusha, Bi. Angel Meela.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni