Magreth Kinabo –
Mahakama
Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania (JMAT) tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Shaban Lila amewataka wanachama wa tawi hilo kuendelea kuwa na ushirikiano na viongozi wapya waliochaguliwa ili kuwezesha chama hicho kutekeleza majukumu yake.
Akizungumza mara baada
ya kuibuka mshindi kuwa Mwenyekiti wa JMAT wa tawi hilo katika uchaguzi
uliofanyika leo tarehe 12 Agosti, mwaka 2022 kwenye ukumbi namba moja wa Mahakama ya Rufani Tanzania,uliopo
Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujaza
nafasi tano zilizo kuwa wazi Jaji Lila aliwashukuru wanachama JMAT kwa
kumpa kura.
‘‘Ninaombeni
ushirikiano ili kuweza kutekeleza majukumu yetu ipasavyo na kulifanya tawi hili
kuendelea kuwa hai,” amesema Jaji Lila, ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya
Rufani.
Viongozi wengine
walioibuka kuwa washindi katika nafasi nyingine zilizokuwa wazi ni Makamu Mwenyekiti
chama hicho ni Mhe. Charles Magesa ambaye pia ni Naibu Msajili wa Mahakama
hiyo. Nafasi ya Katibu ilijazwa na Mhe.
Kifungo Mrisho, nyingine ni Mweka Hazina ambapo ilijazwa na Mhe. Lukengelo Deda
na Mwanachama Mwakilishi Mhe. Jonas Lyakundi aliibuka mshindi wa kiti hicho.
Awali Jaji Lila akitoa
taarifa fupi ya maendeleo ya tawi hilo, amesema limeanzishwa kwa mujibu wa
Ibara ya 18 (a) (i) ya Katiba ya JMAT ya 2017. Ambapo mwaka 2018 tawi hilo
lilikuwa na wanachama 59, idadi hiyo ya wanachama iliundwa na Majaji wa Mahakama hiyo, Msajili
Mkuu pamoja na Katibu wake, Wasaidizi wa Sheria wa Majaji, Mahakimu na Wasajili
waliokuwa katika Kurugenzi ya Maadili(DJSIE)
Kurugenzi ya Usimamizi wa Mashauri(DCM) na Kitengo cha Uboreshaji wa
Mahakama(JDU).
Ameongeza kuwa hadi
kufikia tarehe 1 Agosti, mwaka 2022 tawi
hilo lilikuwa na wanachama 91, lakini kutokana na uteuzi na uhamisho wa
wanachama wengine idadi ya wanachama
hadi kufikia tarehe 12 Agosti mwaka 2022 limekuwa na wanachama 86. Hivyo
ongezeko la wanachama kutoka 59 mpaka 91
limechangiwa na kuongezeka kwa Majaji, Wasaidizi wa Sheria wa Majaji, Wasajili wa Mahakama ya
Rufaa na kuongezeka kwa baadhi ya vitengo.
Amevitaja vitengo hivyo
kuwa ni Kituo cha Huduma kwa Mteja, Maktaba na Baraza la Rufaa za Kodi. Hivyo
idadi ya wanachama imeongezeka kwa asilimia 35 kwa kipindi cha miaka mine kuanzia
mwaka 2018.
Jaji Lila ameongeza
kwamba tawi hilo la JMAT limekuwa likishiriki katika hafla mbalimbali, ikiwemo
vikao, warsha, makongamano na mikutano. Mathalan ,baadhi ya vikao ambavyo tawi
hilo limeshiriki ni kikao cha Baraza Tendaji la JMAT cha tarehe 22Septemba ,
mwaka 2018 kilichofanyika kwa njia ya whatApp.
Tawi hilo pia limeshiriki katika Mkutano Mkuu wa Majaji na Mahakimu wa Afrika Mashariki( EAMJA) uliofanyika Mombasa nchini Kenya mwaka 2018.Mwaka 2021 lilitoa wanachama 10 kuhudhuria mkutano mkuu wa JMAT uliofanyika Jjini Dodoma na Julai mwaka 2022 lilitoa mwakilishi kuhudhuria kikao cha Baraza Tendaji la JMAT kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa JMAT tawi
la Mahakama hiyo aliyemaliza muda wake, akitoa taarifa ya maendeleo ya tawi
hilo.
Baadhi ya wanachama wa
JMAT wa tawi hilo walifuatilia taarifa hiyo.
Mwenyekiti wa kikao cha
uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) tawi la Mahakama ya
Rufani Tanzania, Mhe. Jaji Augustine Mwarija (katikati) akifungua kikao hicho
leo tarehe 12 Agosti mwaka 2022. (Kushoto) ni Mwenyekiti wa JMAT wa tawi hilo
aliyemaliza muda wake, Mhe. Jaji wa Mahakama hiyo, Shaban Lila na kulia ni
Makamu Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Jaji wa Mahakama hiyo Mhe. Rehema
Mkuye.
Makamu Mwenyekiti
aliyemaliza muda wake Jaji wa Mahakama hiyo Mhe. Rehema Mkuye akitoa neon la
shukurani.
Mwenyekiti wa JMAT wa tawi hilo, Mhe. Jaji wa Mahakama hiyo Mhe, Jaji Shaban Lila akizungumza jambo mara baada kuchaguliwa.
Baadhi ya wanachama wa JMAT wa tawi hilo wakichambua kura.
Picha ya pamoja ya
viongozi waliochaguliwa katikati ni Mwenyekiti wa kikao cha uchaguzi wa
viongozi wa Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) tawi la Mahakama ya Rufani
Tanzania, Mhe. Jaji Augustine Mwarija, wa (tatu kushoto)ni Mwenyekiti wa Chama
cha Majaji na Mahakimu Tanzania (JMAT) tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Shaban
Lila na wa pili kushoto ni wakala wa uchaguzi huo na wa kwanza kushoto ni
Katibu wa JMAT tawi hilo, Mhe. Kifungo Mrisho. (Wa tatu kulia wa Makamu Mwenyekiti chama hicho ni Mhe.
Charles Magesa, wapili kulia Mwanachama Mwakilishi Mhe. Jonas Lyakundi na wa kwanza kulia ni Mweka Hazina wa
JMAT tawi hilo Mhe. Lukengelo Deda.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni